STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, June 22, 2014

Ureno, Algeria kusuka au kunyoa leo Brazil

Ronaldo kuibeba Ureno leo kwa Wamerekani?
BAADA ya kupokea kipigo cha 'Paka mwizi' cha mabao 4-0 toka kwa Wajerumani timu ya taifa ya Ureno itakuwa na kibarua kingine kigumu usiku wa leo watakapoikabili Marekani katika mechi ya Kundi G.
Ureno ikiongozwa na nahodha wake, Cristiano Ronaldo itahitaji ushindi mbele ya Marekani ambayo iliitambia Ghana kwa mabao 2-1 katika mechi yao ya kwanza ili kufufua matumaini ya kusalia Brazili.
Kipigo cha aina yoyote itakuwa na maana kwamba Ureno itaungana na nchi za Cameroon, Australia, waliokuwa mabingwa watetezi, Hispania na Uingereza kufungasha virago kurudi kwao kujipanga kwa fainali za mwaka 2018.
Pambano hilo Ureno na Marekani zitachezwa usiku wa manane na mashabiki wa Ureno watakuwa wakiomba Mungu nyota wao wapigane kiume kuendelea kuwapa raha kufuatilia fainali hizo.
Hata hivyo kwa namna Marekani iliyoonyesha kandanda tamu siku walipoumana na Ghana na kupata ushindi wa kushtukiza wa 2-1 ni wazi Ureno itakuwa katika kazi kubwa kuliko ilivyokuwa kwa Ujerumani.
Katika mfululizo wa mechi za makundi leo pia itashuhudiwa Ubelgiji ikikabiliana na Russia katika mechi ya saa 1 usiku ya kundi H kabla ya wawakilishi wa Afrika Algeria kupimana ubavu na Korea Kusini.
Katika mechi ya kwanza, Algeria ilijikuta ikipoteza uongozi kwa kulazwa mabao 2-1 na Ubelgiji, hali inayoifanya katika mchezo wao wa leo kuhitaji ushindi iwapo haitaki kufungashwa virago mapema.
Wapinzani wao Korea Kusini nayo siyo timu ya kubeza kwani katika mechi yao ya kwanza dhidi ya Russia ililazimishwa sare na kuwapa tumaini la kuweza kutinga 16 Bora iwapo itashinda mechi ya leo.
Vinara wa kundi hilo Ubelgiji watakuwa wakisaka ushindi mwingine mbele ya Russia ili kujiandikishia nafasi ya kucheza 16 Bora, ingawa wafuatilia wa soka wanashindwa kutabiri matokeo ya mchezo huo.
Mpaka sasa timu zikiwa zimeshacheza mechi mbili mbili za makundi imeshuhudiwa matokeo yasiyotegemewa ikiwamo ya watetezi Hispania kufurushwa michuano ikiwa haijapata hata pointi moja.
Hispania iliyotwaa taji hilo katika fainali zilizopita nchini Afrika Kusini ilianza kwa kipigo cha aibu cha mabao 5-1 toka kwa wanafainali wenzao wa 2010 Uholanzi kabla ya kulala tena mabao 2-0 kwa Chile.
Kuondoshwa kwa watetezi wao kumelifanya taji hilo kukosa mwenyewe hivyo kuzipa urahisi nchi nyingine kupigana kiume ili kutawazwa kuwa mabingwa wapya kwa fainali hizo za Brazili.
Kundi G
                    P  W  D  L  F  A PTS
Ujerumani    2    1   1  0  6  2   4  
Marekani     1    1   0  0  2   1   3
Ghana          2    0   2  1  3   4   1
Ureno          1    0   0  1   0  4   0
Kundi H:
                    P  W  D  L  F  A  PTS
Ubelgiji       1    1   0  0  2  1   3
Korea         1    0   1  0  1  1   1
Russia         1    0   1  0  1  1   1
Algeria        1    0   0   1  1  2  0
===========

No comments:

Post a Comment