STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, December 16, 2013

Spurs yamtimua AVB, kipigo cha Liver kinauma

Aliyekuwa kocha wa Spurs, AVB alipokuwa wakiajibika kibaruani kabla ya kusitishiwa mkataba wake

KLABU ya Tottenham Hotspur ya England imetangaza kumtimua aliyekuwa kocha wake mkuu, Andre Villa Boas kutokana na matokeo mabaya iliyopata timu hiyo jana kwenye Ligi Kuu ya nchi hiyyo toka kwa Liverpool.
Timu hiyo ilikung'utwa mabao 5-0 na Liverpool ikiwa nyumbani na kukasirisha mabosi na mashabiki wa timu hiyo ambayo imekuwa ikifanywa asuswa kwenye ligi hiyo tofauti na usajili wa kishindo uliofanya msimu huu.
taarifa ya klabu hiyo imesema kuwa wameafikiana na AVB kuachana naye na kwa sasa wanasaka kocha mkuu mpya wa kuinoa timu hiyo ambayo ilimnyakua Mreno huyo miezi 18 iliyopita baada ya kumtema Harry Redknapp aliyeipaisha barani Ulaya.
Miongoni mwa makocha wa awali wanaotajwa kumrithi AVB aliyeishuhudia vijana wake wakinyukwa mabao 6-0 wiki mbili zilizopita na Manchester City ugenini, ni bosi wa zamani wa timu ya taifa ya England, Fabio Capello anayeinoa timu ya taifa ya Russia.
Pia wanatajwa Glenn Hoddle, kocha wa Swansea City Michael Laudrup na mtu anayetajwa haswa kuchukua nafasi hiyo ni Guus Hiddink.

Tanzanite kuagwa kesho, kurudiana na Wasauzi J'mosi

MECHI ya marudiano ya raundi ya pili kuwania tiketi ya kucheza fainali za Kombe la Dunia kwa wasichana wenye umri chini ya miaka 20 kati ya Tanzania (Tanzanite) na Afrika Kusini (Batsesana) itachezwa Jumamosi, Desemba 21 mwaka huu.
Mechi hiyo itachezwa Uwanja wa Dobsonville ulioko Soweto, Johannesburg kuanzia saa 9.30 alasiri kwa saa za Afrika Kusini. Tanzanite itaondoka Jumatano, Desemba 18 mwaka huu saa 4 asubuhi kwa ndege ya Fastjet ikiwa na msafara wa watu 29 wakiongozwa na mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya TFF, Khalid Abdallah.
Kikosi hicho kitaagwa kesho (Desemba 17 mwaka huu) saa 6 katika ofisi za Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).
Katika pambano la kwanza lililochezwa jijini Dar es Salaam Tanzanite ilikumbana na kipigo cha mabao 4-1 toka kwa wasichana wenzao hao, hivyo kuwa na kazi ya kupata ushindi usiopungua mabao manne iwapo inataka kufuzu hatua ya mwisho kuwania nafasi mbili ya kucheza fainali za Dunia zitakazofanyika Canada mwakani.

Pambano la Stand, JKT Kanembwa kurudiwa


 
MECHI ya Ligi Daraja la Kwanza (FDL) kati ya Stand United na Kanembwa JKT iliyochezwa Novemba 2 mwaka huu Uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga na kuvunjika, sasa itarudiwa Februari 1 mwakani.
Uamuzi huo umefanya na Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) katika kikao chake kilichofanyika jana jijini Dar es Salaam ambapo pamoja na mambo mengine ilipitia ripoti za mchezo huo uliovunika dakika ya 87.
TPLB imefikia uamuzi huo baada ya kujiridhisha kuwa mwamuzi Peter Mjaya alitoa taarifa ambazo si sahihi kuhusu mechi hiyo. Mjaya ameondolewa kuchezesha mechi za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) na FDL.
Mechi hiyo itarudiwa katika Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora ambapo timu zote zimetumiwa uamuzi huo kwa maandishi.
Vilevile wachezaji tisa wa Kanembwa JKT waliompiga mwamuzi katika mechi hiyo suala lao linapelekwa Kamati ya Nidhamu ya TFF kwa ajili ya hatua zaidi kwa mujibu wa Ibara ya 27(g)(3) ya Kanuni za FDL.
Wachezaji hao ni Abdallah Mgonja, Baliki Abdul, Mbeke Mbeke, Mkuba Clement, Mrisho Musa, Mtilakigwa Hussein, Nteze Raymond, Philo Ndonde na Uhuru Mwambungu.

Arsenal kuivaa Bavarian, City vs Barca Mtoano Ligi Ulaya


RATIBA ya 16 Bora Ligi ya Mabingwa Ulaya imetoka ambapo Arsenal wametupiwa kuanzia nyumbaji dhidi ya mabingwa watetezi, Bayern Munich ya Ujerumani, huku Manchester City wakipewa Barcelona.
Kwa mujibu wa tariba hiyo, Schalke 04 wenyewe wamepangwa kuikaribisha Real Madrid nyumbani katika mechi ya awali kabla ya kurudiana ugenini kuwania kutinga robo fainali ya ligi hiyo ya mabingwa Ulaya.
Ratiba kamili inaoonyesha Manchester United ikipangiwa mchekea sawa na ilivuo kwa Borussia Dotmund ambao waliicheza fainali za mwaka jana na kunyukwa na Baravian.
Ratiba yenyewe ndiyo hii:
Manchester City Vs Barcelona
Olympiakos Vs Manchester United
AC Milan Vs Atletico Madrid
Bayer Leverkusen Vs Paris Saint-Germain
Galatasaray Vs Chelsea
Schalke 04 Vs Real Madrid
Zenit St. Petersburg Vs Borussia Dortmund
Arsenal Vs Bayern Munich

mechi za awali zitachezwa kuanzia  Februari 18 na Machi 10 kujua zitakazoingia Robo Fainali.

Bondia aumia mazoezini akijifua


BONDIA wa ngumi za kulipwa nchini Shafii Ramadhan ameumia akiwa mazoezini  akijiandaa na pambano la Desemba 22 kwenye ukumbi wa Friends Corner Hotel.

Ramadhani alikuwa aumane na Hassan Kiwale 'Moro Best' alikutana na mkasa huo mazoezini kwake kwa mujibu wa taarifa ya kocha wake, Jafari Ndame.

Pambano la wawili hao lilikuwa la kusindikiza pambano la kuwania ubingwa wa Taifa-PST kati ya bingwa mtetezi, Japhet Kaseba na Alibaba Ramadhani.

Kutokana na kuumia kwa bondia huyo hatapanda tena ulingoni kuzipiga na mpinzani wake siku ya Jumapili kama ilivyokuwa imepangwa.

Mratibu wa pambano hilo Ibrahim Kamwe alisema Moro Best sasa atazipiga na Issa Omar 'Nampepeche'.

Kamwe toka Bigright Promotion, tayari wamemalizana na Moro Best kucheza pambano hilo na Nampepeche.

Mbali na pambano hilo la siku hiyo kutakuwa na michezo mingine ukiwano wa ubingwa kati ya Fadhil Awadh atakayepigana na Karage Suba.

Bondia Mbaruku Heri na Lusekelo Daudi nao wataonyeshana kazi, kama itakavyokuwa kwa Adam Yahya atayezipiga na Harman Richard.

Mkongwe Ernest Bujiku 'Tyson' atacheza na Shaha Kassim, Jocky Hamis dhidi ya Mbena Rajabu na Shaban Kitongoji atapigana na Mwinyi Mzengela.

Kamwe alisema pia siku hiyo kutakuwepo na pambano la mateke (kickboxing) la mtanzania anayeishi Canada Kareem Kutchi dhidi ya Said Juma `Tata Boy`.