STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, January 31, 2015

Bingwa wa Taifa Wanawake kuzoa Mil.3

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhENRxfiE96-KL4ns71WPE2_XM1rUPglyqgf7sij2rgovmDsZi8fpyZJd_YZoswfB67v51e2xA3AoMNgNjzrK728L5tHgcMEVDmQ1vzukkgCK7lD5lb9wuNnWnoNjKAXtEuumAvIqQElrU/s1600/MUKA.jpg
Waziri Dk Fenella Mukangara atakayekuwa mgeni rasmi katika fainali za Kombe la Taifa la Wanawake
Na Boniface Wambura 
BINGWA wa michuano ya Kombe la Taifa Wanawake, inayodhaminiwa na kampuni ya Proin na atapata Kombe na fedha taslimu Sh. Milioni 3. 
Aidha, katika michuano hiyo inayofanyika kwa mara ya kwanza nchini, mshindi wa pili atapata Sh. Milioni 2, wakati mshindi wa tatu atapata Sh. Milioni 1.
Fainali ya Kombe la Taifa Wanawake itazikutanisha Pwani na Temeke kesho Uwanja wa Azam Complex uliopo Chamazi, Dar es Salaam na mashabiki wataingia bure.
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk Fenella Mukangara anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye mechi hiyo itakayoanza Saa 10.15 jioni, ikichezeshwa na refa wa FIFA, Jonesia Rukyaa na kuonyeshwa moja kwa moja na televisheni ya Azam.
Marefa wasaidizi wanatarajiwa kuwa Hellen Mduma, Agnes Alphonce, na Mwanahamisi Matiku wakati Kamisaa atakuwa Ingridy Kimario. Timu za Ilala na Kigoma zitacheza mechi ya utangulizi kutafuta mshindi wa tatu kuanzia saa 8.00 mchana.

Bayern Munich waonja kipigo Bundesliga

Bas Dost scores
Bayern walivyokuwa wakiangamizwa na Wolfsburg
Pep Guardiola
Kocha wa Beyern Munich, Pep Guardiola akiwa haamini kama vijana wake wamemuangusha ugenini
MABINGWA watetezi wa Bundesliga, Bayern Munich jana ilikiona cha moto ugenini baada ya kunyukwa mabao 4-1 na Wolfoburg kikiwa ndicho kipigo cha kwanza kwao kwa msimu huu katika ligi hiyo.
Mabao mawili yaliyofungwa na Bas Dost katika dakika ya nne na 45 na mengine ya Kelvin De Bruyne ya dakika za 53 na 73 yalitosha kuwazima wababe hao wa Ujerumani ambao walipata bao la kufutia machozi katika dakika ya 55 kupitia kwa Juan Bernat.
Licha ya kipigo hicho Bayern wameendelea kukalia kiti cha uongozi wa ligi hiyo wakiwa na pointi 45 na wapinzani wao waliowatoa nishai Wolfsburg waking'ang'ania nafasi ya pili wakiwa na pointi 37.
Ligi hiyo inaendelea jioni hii kwa michezo kadha kabla ya kesho kumalizia michezo mingine ya wikiendi hii.












Newcastle Utd yainyuka Hull City, Man Utd waongoza 3-0 HT

Sammy Ameobi (right) is congratulated after scoring for Newcastle
Wachezaji Newcastle waksihangilia moja ya mabao yao
Ahmed Elmohamady of Hull City punches the ball into the Newcastle net
Hekaheka langoni mwa Newcastle
Sammy Ameobi shoots to score for Newcastle
Sammy Ameobi akifunga bao la pili la Newcastle
KLABU ya Newcastle United ikiwa ugenini imetoa kipigo cha mabao 3-0 kwa wenyeji wao Hull City katika mfululizo wa mechi za Ligi Kuu ya England.
Newcastle walianza kuandika bao la kwanza dakika ya 40 kupitia kwa Remy Cabella kabla ya kuongeza bao la pili dakika tano baada ya kuanza kwa kipindi cha pili kupitia kwa Sammy Ameobi na katika dakika ya 78 Yoan Gouffran alimaliza udhia kwa kufunga bao la tatu na kuipa ushindi muhimu Newcastle United.
Kwa sasa michezo kadhaa ipo mapumziko huku Spurs wakiongoza mabao 2-0 dhidi ya West Bromwich, Everton ikiwa ugenini wanaongoza bao 1-0 dhidi ya Crystal Palace, Liverpool dhidi ya West Ham Utd wapo 0-0, Manchester United wanaongoza 3-0 dhidi ya Leiceister City uwanja wa Old Trafford, Stoke City wakiwa nyumbani wanaongoza 2-1 dhidi ya QPR na Sunderland wakiwa mbele kwa mabao 2-0 nyumbani dhidi ya Burnley.

Mnyama 'yaua' Taifa, Mbeya City yalala Moro 1-0

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhQw0Q6Z99EoVWkyx9Yf4-SQu6v6ms0PaPb_sKenOOroi-QKbRnmecjHWsCkMjBGp9Gme9kVSLBI6loRiDVMNpxjyOidGhsx9k3uN8L4NzFcmC9SUT8cQrLUnJwL2a4pbDoK4TypzmK_ig/s1600/_HMB7014.JPG
Simba
JKT Ruvu
http://shaffihdauda.co.tz/wp-content/uploads/2015/01/IMG-20140920-WA005311.jpg
Mbeya City iliyolala Morogoro

BAADA ya kuwaweka roho juu mashabiki wao, Simba jioni ya leo imezinduka mbele ya JKT Ruvu baada ya kuifunga JKT Ruvu mabao 2-1 na kupanda hadi nafasi ya saba.
Mabao mawili ya mshambuliaji wa kimataifa wa Uganda, Dan Sserunkuma yameisaidia Simba kupata ushindi wake wa tatu katika Ligi Kuu Tanzania Bara kwenye uwanja wa Taifa na Simba walianza kuandika bao mapema kabla ya JKT Ruvu kurejesha na kwenda mapumziko matokeo yakiwa bao 1-1.
Bao la Simba lililofungwa na Sserunkuma liliwekwa kimiani katika dakika ya pili tu ya pambano hilo akiunganisha krosi pasi ya Emmanuel Okwi.
Hata hivyo JKT Ruvu walikuja kusawazisha bao hilo dakika ya 19 kwa George Minja kuunganisha kwa kichwa mpira wa Jabir Aziz na kufanya timu ziende mapumziko zikiwa nguvu sawa.
Sserunkuma aliihakikishia Simba ushindi baada ya kufunga bao la pili katika dakika ya tatu baada ya kuanza kwa kipindi cha pili kewa kichwa akiwahi mpira wa krosi ya Okwi na kusaidia Simba kulipa kisasi kwa maafande hao ambao waliwafunga mabao 3-2 walipokutana mara ya mwisho.
Kwa ushindi huo Simba imefikisha pointi 16 na kuchupa kutoka nafasi ya 11 hadi nafasi ya saba.
Katika mchezo mwingine wa ligi hiyo Mtibwa Sugari imejikuta ikichupa hadi nafasi ya pili ya msimamo ikiziengua Yanga na JKT Ruvu baada ya kupata suluhu ya bila kufungana dhidi ya Coastal Union.
Mtibwa Sugar ilipata sare hiyo uwanja wa Mkwakwani Tanga na kufikisha pointi 18 sawa na ilizonazo Yanga waliokuwa wa pili ambao wanashuka hadi nafasi ya tatu japo kesho itashuka dimbani kuumana na Ndanda na kuwa na nafasi ya kukwea kileleni.
Nayo timu ya Polisi Moro imefanikiwa kuinyuka Mbeya City bao 1-0 ikiwa ni sikui chache tangu Mbeya City kutoka  kuilaza Simba 2-1 katikati ya wiki kwenye mechi yao ya kiporo kilichochezwa uwanja wa Taifa.
Mjini Mbeya wenyeji Prisons ililazimishwa sare ya 1-1 na wageni wao Kagera Sugar katika mchezo unaodaiwa ulikuwa mkali na wa kusisimua wenyeji walianza kuzinguliwa kwa bao la Rashid Mandawa kabla ya kuchomoa dakika 15 kabla ya kumalizika kwa pambano hilo kupitia Nurdin Chona..
Katika mfululizo wa ligi hiyo kesho, Yanga itaikaribisha Ndanda kwenye uwanja wa Taifa wakati Ruvu Shooting wataialika Stand United ya Shinyanga kwenye uwanja wa Mabatini, Mlandizi, Pwani.