STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, January 31, 2015

Bayern Munich waonja kipigo Bundesliga

Bas Dost scores
Bayern walivyokuwa wakiangamizwa na Wolfsburg
Pep Guardiola
Kocha wa Beyern Munich, Pep Guardiola akiwa haamini kama vijana wake wamemuangusha ugenini
MABINGWA watetezi wa Bundesliga, Bayern Munich jana ilikiona cha moto ugenini baada ya kunyukwa mabao 4-1 na Wolfoburg kikiwa ndicho kipigo cha kwanza kwao kwa msimu huu katika ligi hiyo.
Mabao mawili yaliyofungwa na Bas Dost katika dakika ya nne na 45 na mengine ya Kelvin De Bruyne ya dakika za 53 na 73 yalitosha kuwazima wababe hao wa Ujerumani ambao walipata bao la kufutia machozi katika dakika ya 55 kupitia kwa Juan Bernat.
Licha ya kipigo hicho Bayern wameendelea kukalia kiti cha uongozi wa ligi hiyo wakiwa na pointi 45 na wapinzani wao waliowatoa nishai Wolfsburg waking'ang'ania nafasi ya pili wakiwa na pointi 37.
Ligi hiyo inaendelea jioni hii kwa michezo kadha kabla ya kesho kumalizia michezo mingine ya wikiendi hii.












No comments:

Post a Comment