STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, February 12, 2015

RATIBA YA MECHI ZA LIGI KUU VPL NDIZO HIZI

JKT Ruvu
Mtibwa Sugar

Ndanda Fc

Ruvu Shooting
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjsiSMyuzw8Scaz_WXLWA8zexyBWABhGV6CxMyERHknqT5Q43BcmRrLvHUNE4oKs2G0hzOPiau9RUA7-sUr7pys-pddVf-7IGaefiwHsTshpDCGxRvAxh3L-kL2Ok3ZtNfCb9E2HTfhftye/s1600/S1.jpg
Simba
Feb 14, 2015
Ndanda vs Mtibwa Sugar
Coastal Union vs Mbeya City
Stand United vs Mgambo Shooting
Feb 15, 2015
Polisi Morogoro vs Simba
Kagera Sugar vs JKT Ruvu
Feb 21, 2015
Mbeya City vs Yanga
Kagera Sugar vs JKT Ruvu
Ndanda vs Coastal Union
Mgambo Shooting vs Mtibwa Sugar
Feb 22, 2015
Stand United vs Simba
Azam vs Tanzania Prisons
Feb 25, 2015
Mbeya City vs Ruvu Shooting

HIVI NDIVYO TFF ILIVYOPANGUA KAMATI ZAKE NDOGO ZA SHERIA

 
JUDICIAL AND STANDING COMMITTEES.

Kamati ya Utendaji iliyoketi tarehe 19 Disemba 2014, ilifanya mabadiliko katika kamati ndogo ndogo na zile za kisheria. Kamati hizo ni kama ifuatavyo

KAMATI YA NIDHAMU
1.   Tarimba Abbas (Mwenyekiti)
2.   Advocate Jerome Msemwa ( Makamu mwenyekiti)
3.    Kassim Dau
4.   Nassoro Duduma
5.   Kitwana Manara 

KAMATI YA RUFANI YA NIDHAMU
1.   Advocate Mukirya Nyanduga (Mwenyekiti)
2.   Advocate Revocatus Kuuli (Makamu mwenyekiti)
3.   Abdala Mkumbura
4.   Dr. Francis Michael
5.   Advocate Twaha Mtengela
 
KAMATI YA MAADILI
1.   Advocate Wilson Ogunde (Mwenyekiti)
2.   Advocate Juma Nassoro (Makamu mwenyekiti)
3.   Advocate Ebenezer Mshana
4.   Geroge Rupia
5.   Mh. Said Mtanda

KAMATI YA RUFANI YA MAADILI
1.   Advocate Walter Chipeta (Mwenyekiti)
2.   Magistrate  George Kisagenta (Makamu-M'Kiti)
3.   Lilian Kitomari
4.   Advocate Abdala Gonzi

KAMATI YA UCHAGUZI
1.   Advocate Melchesedeck Lutema
2.   Advocate Adamu Mambi (Makamu mwenyekiti)
3.   Hamidu Mahmoud Omar
4.   Jeremiah John Wambura
5.   John Jambele

KAMATI YA RUFANI TA UCHAGUZI
1.   Advocate Julius Lugaziya (Mwneyekiti)
2.   Advocate Machare Suguta (Makamu Mwenyekiti)
3.   Idrisa Nassor
4.   Paschal Kihanga
5.   Benister Lugora

KAMATI YA FEDHA NA MIPANGO
1.   Wallace Karia (Mwenyekiti)
2.   Yahya Mohamed (Makamu mwenyekiti)
3.   Goodluck Moshi
4.   Omar Walii
5.   Ellie Mbise
6.    Deo Lubuva

KAMATI YA MASHINDANO
1.   Geofrey Nyange (Mwenyekiti)
2.   Ahmed Mgoyi (Makamu mwenyekiti)
3.   James Mhagama
4.   Stewart Masima
5.   Steven Njowoka
6.   Said Mohamed

KAMATI YA UFUNDI
1.   Kidao Wilfred (Mwenyekiti)
2.   Athumani Kambi (Makamu mwenyekiti)
3.   Vedastus Rufano
4.   Dan Korosso
5.   Pelegriunius Rutahyugwa

KAMATI YA MPIRA WA MIGUU YA VIJANA
1.   Ayoub Nyenzi (Mwenyekiti)
2.    Khalid Abdallah (Makamu mwenyekiti)
3.    Ali Mayay
4.   Mulamu Ngh’ambi
5.   Said Tully

KAMATI YA MPIRA WA MIGUU WANAWAKE
1.   Blassy Kiondo (Mwenyekiti)
2.   Rose Kissiwa (Makamu mwenyekiti)
3.   Zena Chande
4.   Amina Karuma
5.   Zafarani Damoder
6.   Beatrice Mgaya
7.   Sofia Tigalyoma
8.   Ingrid Kimario (Katibu wa Kamati)

KAMATI YA WAAMUZI
1.   Saloum Umande Chama (Mwenyekiti)
2.   Nassoro Said (Makamu mwenyekiti)
3.   Charles Ndagala (Katibu)
4.   Kanali Issaro Chacha
5.   Soud Abdi

KAMATI YA HABARI NA MASOKO
1.   Athuman Kambi (Mwenyekiti)
2.   Alms Kasongo (Makamu Mwenyekiti)
3.   Rose Mwakitangwe
4.   Amir Mhando
5.   Haroub Selemani

KAMATI YA UKAGUZI WA FEDHA
1.   Ramadhan Nassib (Mwenyekiti)
2.   Epaphra Swai (Makamu mwenyekiti)
3.   Jackson Songora
4.   Golden Sanga
5.   Francis Ndulane
6.   Cyprian Kwiyava

KAMATI YA TIBA
1.   Dr. Paul Marealle (Mwenyekiti)
2.   Dr. Fred Limbanga (Makamu mwenyekiti)
3.   Dr. Mwanandi Mwankewa
4.   Dr. Eliezer Ndelema
5.   Asha Mecky Sadik

KAMATI YA FUTSAL NA BEACH SOCCER
1.   Ahmed Idd Mgoyi (Mwenyekiti)
2.   Hussein Mwamba (Makamu mwenyekiti)
3.   Samson Kaliro
4.   Shaffih Dauda
5.   Boniface Pawassa
6.   Apollo Kayugi

PRESIDENTIAL COMMISSION FOR AFFAIRS
1.   Omar Abdulkadir (Mwenyekiti)
2.   Emmanuel Chaula (Makamu mwenyekiti)
3.   Victor Mwandiki
4.   Riziki Majala
5.   Zahra Mohamed
6.   David Nyandu

PRESIDENTIAL COMMISSION ON BUSINESS AND INVESTMENTS
1.   William Erio (Mwenyekiti)
2.   Mbaraka Igangula
3.   Advocate Iman Madega
4.   Lt. Col Charles Mbuge
5.   Philemon Ntalihaja

TIMU ya Taifa ya Beach Soccer kuwafuata Wakenya kesho

TIMU ya Taifa ya Tanzania ya mpira wa ufukweni (beach soccer) inatarajia kurusha karata yake ya kwanza Jumapili kwa kucheza na Kenya katika raundi ya kwanza ya michuano ya Afrika kwa ajili ya fainali za Afrika za michuano hiyo zitakazofanyika Aprili mwaka huu nchini Shelisheli.
Mchezo huo utachezwa Mombasa nchini Kenya na mchezo wa marudiano utachezwa nchini kati ya Februari 20 na 22 mwaka huu
Akizungumza jijini, Kocha wa timu hiyo John Mwansasu, alisema maandalizi ya kwa ajili ya mchezo huo yanaendelea vema na wamecheza michezo miwili ya kirafiki na timu ya Zanzibar na kusema walipoteza mmoja na kushinda mmoja.
 “Maandalizi yanaendelea na kiwango cha wachezaji kinaimarika kila siku na nawaahidi watanzania kurudi na ushindi japo sikupata michezo ya kirafiki ya kimataifa lakini nina imani na timu yangu”, alisema Mwansasu.
Kocha John Mwansasu anasaidiwa na Ali Shariff 'Adolf' kutoka Zanzibar, na Meneja wa timu ni George Lucas na kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania ya mpira wa ufukweni (beach soccer) kinaundwa na wachezaji  15, saba toka Zanzibar na nane Tanzania bara
Iwapo timu ya Tanzania itasonga mbele, katika raundi ya pili itacheza na Misri ikianzia nyumbani kati ya Machi 13 na 15 mwaka huu.
Timu hiyo inayofanya mazoezi kwenye ufukwe wa Escape One inatarajiwa kuondoka nchini kesho Ijumaa.

Mama Muuza wa Shamsa bado kidogo tu

SHAMSA Ford, mmoja wa nyota wa filamu wa kike nchini, amewataka mashabiki wake wakae tayari kuipokea filamu yake mpya ya 'Mama Muuza' ambayo ipo hatua za mwisho ikirekebishwa kabla ya kuachiwa mtaani.
Akizungumza na MICHARAZO, Shamsa alisema filamu hiyo iliyotungwa na kutayarishwa na yeye mwenyewe ikiwa imewashirikisha wasanii kadhaa nyota akiwamo Haji Adam 'Baba Haji', itatoka Aprili.
"Nipo katika marekebisho ya mwishomwisho na nitaiachia 'Mama Muuza' miezi miwili ijayo kulingana na foleni iliyopo kwa wasambazaji," alisema.
Shamsa alisema kama ilivyokuwa kwa 'Chausiku' moja ya filamu iliyofanya vema kwa mwaka 2014, ndivyo 'Mama Muuza' itakavyokuwa kutokana na simulizi lake kubeba uhalisia wa maisha ya uswahili.
"Kama ilivyokuwa 2014 napenda mwaka 2015 uwe wenye raha na burudani kwa mashabiki wangu kupitia 'Mama Muuza'," alisema Shamsa.

Mengi kumtangaza Mshindi wa Wazo la Biashara 3N leo

http://blogs-images.forbes.com/mfonobongnsehe/files/2014/04/reginald-mengi.jpg
Mfanyabishara maarufu nchini Dk Reginald Mengi
 Na Rahma Junior
MSHINDI wa Januari 2015 wa Shindano la Wazo la Biashara 3N' anatarajiwa kutangazwa leo Alhamisi ya Februari 12 kuanzia saa tano asubuhi jijini Dar es salaam.
Kwa mujibu wa Dk. Reginald Mengi kupitia kurasa wake wa twitter, alitangazia umma kuwa Shindano hilo jipya lijulikanalo kwa kifupi -3N, ikiwa ni kifupisho cha ‘Nitabuni wazo la biashara, Nitatekeleza, na Nitafanikiwa’, ambapo mshindi wa kwanza wa mwezi Januari anatarajiwa kutangazwa siku hiyo ya alhamisi Februari 12.
Dk. Mengi aliweka ujumbe huo twittter : “Kutokana na sababu zisizozuilika mshindi wa Januari wa shindano la 3N atatangazwa Februari 12 saa 5 asubuhi. Samahani kwa usumbufu wowote”.
Kwa mujibu wa Dk. Mengi awali mshind I alitakiwa kutangazwa Jumatano ya leo ya Februari 11, kabla ya kusogeza mbele hiyo Februari 12.
Shindano hilo litakuwa linafanyika kila mwezi kwa muda wa miezi sita kuanzia Januari Mosi 2015, hadi Juni 30, 2015, na mshindi wa kila mwezi atajishindia ruzuku ya shilingi milioni 10 atakazozitumia kutekeleza kwa vitendo wazo lake la biashara.
Shindano hilo, linawashirikisha Watanzania pekee, litaendeshwa kwa njia ya mtandao wa kompyuta ambapo mshiriki atatuma wazo lake la biashara kwa anuani ya twita @regmengi Shindano la Wazo la Biashara. Katika mchujo wa kwanza jopo la wataalamu litateua mawazo 10 bora Zaidi na waliotoa mawazo hayo watafanyiwa usaili kwa njia ya simu ili jopo hilo lijiridhishe kama mawazo waliyoyotuma ni yao binafsi, na kama wamejipanga vizuri kutekeleza kibiashara.
Kutokana na mawazo hayo 10 teule, jopo litachagua wazo moja kuwa mshindi. Hii ni mara ya tatu kwa Dkt. Mengi kuendesha shindano kwa kutumia mtandao wa kompyuta wa twitter kwa kuamini kwake kuwa mitandao ya kijamii ina nguvu kubwa katika kuchochea ujasiriamali hasa kwa kizazi cha sasa.
Shindano la kwanza na la pili lililoendeshwa mwaka jana lilikusudiwa kushawishi mawazo ya kuondoa umaskini katika taifa lenye utajiri mkubwa, lakini watu wake wengi wakiwa bado wametopea katika lindi la umaskini.
Awali akizungumza katika uzinduzi wa shindano hilo, Dkt. Mengi alisema shindano hilo limelenga kuhimiza watu kuwa na upeo mkubwa wa kuona fursa za kibiashara na kuzitumia kujikwamua kiuchumi. Pia alisema shindano hilo ni mchango wake binafsi wa kuunga mkono jitihada za serikali na sekta binafsi za kuwakomboa wananchi kiuchumi kwa njia za ujasirimali, kwani amesema Sera zote mbili za kitaifa za Elimu ya juu na maendeleo ya viwanda vya kati na vidogo zina vipengele vya kuchochea na kuendeleza utamaduni wa ujasirimali wa mtu mmoja mmoja.
“Kwa muda mrefu nimekuwa nikishawishi uwepo wa moyo wa ujasirimali miongoni mwa wa Watanzania na hasa kwa vijana. Ni ndoto yangu kuona uchumi wetu unakua kwa kasi kiasi cha kuzalisha zaidi ya mamilionea 100 kila mwaka wanaoendesha biashara halali,” alisema.
Alisema kuwa na wazo sahihi la biashara, katika muda muafaka na eneo sahihi ni muhimu zaidi kuliko ruzuku ya fedha.
“Nataka vijana watambue kwamba wanaweza kuanza na kitu kidogo na kukua kufikia kampuni kubwa kabisa ya kimataifa unayoweza kufikiria,” alisema na kusisitiza kwamba anaamini siku moja mazingira ya ujasirimali nchini Tanzania yakuwa miongoni mwa mazingira bora kabisa barani Afrika.
Amesisitiza kuwa Shindano hilo liko wazi kwa watanzania wote na wanachotakiwa kufanya ni kuhakikisha wanapeleka wazo lao la biashara kwa Dk Mengi kupitia mtandao wa kompyuta wa twita, kwa kumtag Dk Mengi kwenye @regmengi.
Aidha amesema ni wale tu watakaomtag ndio watafikiriwa na jopo la wataalamu, na kusisitiza kuwa maamuzi ya jopo la Wataalamu yatakuwa ni ya mwisho.
Washindi wa kila mwezi wataarifiwa kwa kutumiwa ujumbe mfupi kwa kupitia akaunti zao za twita (DM) na kupewa ruzuku yao katika sherehe fupi itakayohudhuriwa na waandishi wa habari.