STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, March 24, 2014

Golden Bush wachekelea kutoa mmoja timu ya taifa

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjM_enMZwt885hVpN4DNDsO2xLFfCdYaoIdFadOJsGdS73hmKfaQ8fZuX-cFXsmqBpP2SFeiWDVZubmKg_2EXx1PnIG5r33elKJNzCuA8flTadNPHJ0fG59PkLm5lsMhDA0jRcfzbJs5CI/s640/Golden+Bush+FC+Logo.JPG
UONGOZI wa timu ya Golden Bush umesema umefurashwa na kitendo cha mmoja wa wachezaji wake wa timu ya vijana ya Golden Bush FC inayoshiriki Ligi Daraja la Tatu Wilaya ya Kinondoni, Ayoub Lipati kuteuliwa kwenye timu ya Taifa ya Maboresho iliyotangazwa na TFF.
Lipati ambaye ni mashambuliaji ni mmoja wa wachezaji 36 walioteuliwa na jopo maalum la makocha 40 waliokuwa na kazi ya kusaka wachezaji kwa ajili ya kuboresha timu ya taifa, Taifa Stars katika kuelekea kwenye Fainali za Afrika 2015.
Mlezi wa klabu hiyo, Onesmo Waziri 'Ticotico' aliiambia MICHARAZO kuwa Golden Bush umejisikia faraja uteuzi wa Lipati kutokana na ukweli timu yao ndiyo kwanza ina miaka miwili tangu kuundwa kwake.
"Tumefurahia sana kufanikiwa kutoa mchezaji mmoja katika kikosi cha wachezaji 36 walioteuliwa na jopo maalum la kusaka vipaji kwa ajili ya maboresho ya Taifa Stars," alisema Ticotico.
Ticotico alisema imani yake Lipati atakuwa balozi mwema wa Golden Bush katika kikosi kinachotarajiwa kuingia kambini mjini Tukuyu Mbeya mapema mwezi ujao.

Yabainika asilimia 25 ya wanawake Bongo hurukwa 'Ukuta'

 
WAKATI kasi ya wanawake wenye maambukizi ya Virusi vya Ukimwi ikiongezeka, imebainika kuwa asilimia 26.5 ya wanawake nchini Tanzania wanafanya mapenzi kinyume na maumbile. 
Mfumo wa uzazi unaharibika; Watafiti wanabainisha kuwa kitendo hicho licha ya ukweli hakifai kwa vile kinaharibu mfumo wa uzaz.
Pia kina athari kubwa mno kwa mwanadamu, mojawapo ni ikiwemo uwezekano mkubwa wa wahusika kuambukizana virusi vya Ukimwi kwa vile hakuna vilainishi, hivyo kusababisha michubuko ambayo ndio njia kuu ya kuambukiza vijidudu hivyo.


 Mtafiti Mwanasayansi, Irene Mremi kutoka Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu nchini Tanzania (NIMR) alitoa ripoti hiyo hivi karibuni hapa jijini Dar Es Salaam.

Mremi akiwa na jopo la watafiti kutoka NIMR anasema kuwa wanawake hao wamesema chanzo kikubwa kinachowapelekea kufanya ngono kinyume na maumbile ni kujipatia kipato zaidi na Kuogopa kupata Mimba.

Vilevile alizitaja sababu nyingine za wanawake kufanya mapenzi kwa njia hiyo ni kulinda usichana wao na baadhi ya mila na tamaduni za baadhi ya makabila.

Sampuli za utafiti Utafiti huo ulikusanya sampuli kutoka katika mikoa ya Dar es salaam, hasa maeneo ya Kinondoni, Tanga, Makete na Siha. Mremi anasema “Utafiti wetu uliwahusisha wasichana na wanawake wa rika kuanzia miaka 15 na kuendelea na kada tofauti katika jamii kama wanafunzi, wafanyakazi, wahudumu wa bar, wauguzi, makahaba na akina mama wa nyumbani Katika maeneo hayo watu 903 walijitokeza wakiwepo pia wanaume ambao walihusishwa katika utafiti huo.

Imani potofu kwa wanaume Wanaume waliohojiwa wamesema wanafanya kwa ajili ya kupata raha tu na imani ya kuwa huko hakuna maaambukizi ya VVU, kitu ambacho ni uongo, kwani huko ndiko kwenye kuchangia ukimwi kwa haraka zaidi kuliko sehemu nyingine yoyote.
Credit:E.Shiratu

Hizi ndizo mechi za lala salama za VPL


MACHI 26, 2014
Yanga v/s Tanzania Prisons- Taifa, Dar
Mgambo Shooting v/s Azam Fc- Mkwakwani, Tanga

MACHI 29, 2014
Ashant United v/s JKT Oljoro- Chamazi, Dar

MACHI 30, 2014
Mbeya City v/s Tanzania Prisons- Sokoine, Mbeya
Kagera Sugar v/s Ruvu Shooting- Kaitaba, Bukoba
Mtibwa Sugar v/s Coastal Union- Manungu, Morogoro
JKT Ruvu v/s Rhino Rangers- Chamazi, Dar
Azam Fc v/s Simba- Taifa, Dar
Mgambo v/s Yanga- Mkwakwani, Tanga

APRILI 5, 2014
Kagera Sugar v/s Simba- Kaitaba, Bukoba
Ashanti United v/s Mbeya City- Chamazi, Dar

APRILI 6, 2014
Coastal Union v/s Mgambo Shooting-Mkwakwani, Tanga
JKT Oljoro v/s Tanzania Prisons- Sheikh Amri Abeid, Arusha
Rhino Rangers v/s Mtibwa Sugar- Ali Hassan Mwinyi, Tabora
Ruvu Shooting v/s Azam Fc- Mabatini, Pwani
Yanga v/s JKT Ruvu- Taifa, Dar

APRILI 9, 2014
Yanga v/s Kagera Sugar- Taifa, Dar

APRILI 12, 2014
Mtibwa Sugar v/s Ruvu Shooting- Manungu, Morogoro
Coastal Union v/s JKT Ruvu- Mkwakwani, Tanga
Tanzania Prisons v/s Rhino Rangera- Sokoine, Mbeya

APRILI 13, 2014
Mgambo Shooting v/s Kagera Sugar- Mkwakwani, Tanga
Simba v/s Ashant United- Taifa, Dar
Mbeya City v/s Azam Fc- Sokoine, Mbeya
JKT Oljoro v/s Yanga- Sheikh Amri Abeid, Arusha

APRILI 19, 2014
Rhino Rangers v/s Ruvu Shooting- Ali Hassan Mwinyi, Tabora
Mbeya City v/s Mgambo Shooting- Sokoine, Mbeya
Tanzania Prisons v/s Ashant United- Jamhuri, Morogoro
JKT Ruvu v/s Azam Fc- Chamazi, Dar
JKT Oljoro v/s Mtibwa Sugar- Sheikh Amri Abeid, Arusha
Coastal Union v/s Kagera Sugar- Mkwakwani, Tanga
Yanga v/s Simba- Taifa, Dar

Tevez azidi kuipaisha Juve Italia, Milan yadroo

http://e2.365dm.com/14/03/660x350/Catania-v-Juventus-Carlos-Tevez-L-vies-with-C_3106513.jpg?20140323214233
Tevez akichuana na mchezaji wa Catania usiku wa jana kwenye Seria A
http://sport.bt.com/images/juve-grind-out-catania-win-136388712671108302?v=140323221505
Akishangilia bao lao

MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu ya Italia, Juventus imeendelea kutakata kwa kupata ushindi mwembamba ugenini dhidi ya Catania shukrani za pekee ziende kwa Carlos Teves aliyefunga bao hilo la pekee katika dakika ya 59.
Ushindi huo wa Juve umewafanya wafikishe jumla ya pointi 78 baada ya kucheza mechi 29 wakiiacha mbali Roma inayoshuka dimbani  kesho kuumana na Torino ikiwa na pointi zake 64.
Bao alilofunga Tevez nytota wa zamani wa Aston Villa, Manchester Utd na Manchester City, limemfanya afikishe jumla ya mabao 16 katika ligi hiyo na kulingana na nyota wa Torino, Ciro Immobile.
Katika mechi nyingine zilizochezwa usiku wa jana Napoli ilikubali kipigo kwenye uwanja wake wa nyumbani toka kwa Fiorentina, nazo timu za Lazio na AC Milan zikitoshana nguvu kwa kufunga bao 1-1, wanyeji wakijifunga kabla ya kusawazisha katika kipindi cha pili.
Kipute cha pili kinatarajiwa kuendea tena kesho kwa pambano la Roma itakayoikaribisha Torino, kabla ya keshokutwa Chievo kuumana na Bologna, Cagliari dhidi ya Hellas Verona, huku Genoa itaikaribisha Lazio na  Atalanta itaumana na Livorno.
Siku hiyo ya Jumatano pia kutakuw ana mechi nyingine ya kukata na shoka kati ya Fiorentina itakayoikaribisha Ac Milan, huku  Catania itaumana na Napoli, wakati  Juventus watakuwa nyumbani kuwakaribisha Parma na Sassuolo itakuwa mwenyeji wa Sampdoria.
Alhamis kutakuwa na pambano moja tu litakalowakutanisha Inter Milan ambayo jana ilichezea kichapo itakayoumana na Udinese.

Barca yaizima Rea kwao, Messi apiga hat trick

Matchwinner: Messi points to the Barcelona support as Gerard Pique (centre) and Alexis Sanchez catch up
Messi akishangilia moja ya mabao yake matatu alipoiangamiza Real Madrid
Flying high: Sergio Ramos celebrates Madrid's third with Ronaldo (left) while the Madrid star jumps for joy (right)
Real Madrid wakishangilia moja ya mabao yao

KLABU ya Real Madrid usiku wa kuamkia leo imechezea kichapo cha mabao 4-3 toka kwa wapinzani wa jadi Barcelona na kutoa baraka kwa mahasimu wao wa jiji la Madrid, Atletico Madrid kukikalia jumla kiti cha uongozi wa Ligi Kuu ya Hispania.
Mshambuliaji nyota wa Argentina, Lionel Messi alidhihirisha yeye ni bora baada ya kufunga hat trick kwenye pambano hilo lililochezwa uwanja wa Santiago Bernabeu, mjini Madrid.
Wageni walianza kuandika bao dakika ya saba kupitia kwa Andres Iniesta kabla ya Mfaransa,  Karim Benzema kusawazisha bao hilo dakika ya 20 na kuongeza jingine la pili dakika ya 24.
Dakika tatu kabla ya mapumziko Messi aliisawazishia bao na timu hizo kwenda mapumziko zikiwa zimefungana mabao 2-2.
Kipindi kilipoanza iliwachukua wenyeji dakika 10 kuandika bao la tatu kupitia kwa Cristiano Ronaldo aliyefunga kwa mkwaju wa penati.
Hata hivyo Lionel Messi alisawazisha hilo dakika ya 65 kwa mkwaju wa penati pia kabla ya kuongeza jingine dakika tano kabla ya pambano hilo kumalizika na kukamilisha hat trick yake na kuipa ushindi wa mabao 4-3 timu yake ya Barcelona.
Ushindi huo umeifanya Barcelona imeendelea kubakia nafasi ya tatu kwa kufikisha pointi 69, moja zaidi ya wapinzani wao Real Madrid na Atletico Madrid waliopo kileleni kwa uwiano wa mabao ya kufunga na kufungwa na matokeo baina yao wawili hao waliopo juu.
Ligi hiyo inatarajiwa kuendelea tena kesho Jumanne hadi Ijumaa kwa mechi ambazo zitaendelea kutoa taswira ya ubingwa wa nchi hiyi.
Jumanne;
Almería vs Real Sociedad
Málaga  vs  Espanyol
Jumatano:
Elche vs Athletic Club
Barcelona vs Celta de Vigo
Rayo Vallecano vs Osasuna
Alhamis:
Atlético Madrid vs Granada
Sevilla vs Real Madrid
Getafe vs  Villarreal
Real Sociedad  vs Real Valladolid
Ijumaa:
Levante vs Real Betis
Almería vs Valencia

TP Mazembe yafa ugenini, Mbwana kama kawa

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiPcbztEZEpnlosWiXEocIS2HDtp7-xxKd2CpOOqJ8ABEqV2R8cXTFSuU-hmbUwOF98KNrE9G8OypEoBHSUDZNvM0YjXWj3qCdILvnjXJ4_j6v_JPdXGMb684Ib7QY1MeKmWxl8feSypeC_/s1600/Samata-Bwana58021.jpgMABINGWA wa zamani wa Afrika, TP Mazembe jana wamekumbana na kipigo cha mabao 2-1 katika pambano lao la mkondo wa kwanza wa hatia ya 16 Bora dhidi ya we nyeji wao, Sewe ya Ivory Coast.
Mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Samatta aliifungia timu yake bao la kufitia machozi baada ya wenyeji kujipatia mabao yake kupitia kwa Roger Assale  katika dakika ya 38 kaba la kuongeza jingine kwa mkwaju wa penati  dakika ya 82 kupitia  Christian Kouame.
Hata hivyo wenyeji wakiamini wameisulubu Tp Mazembe kwa mabao mawili kavu, mtokea benchi Mbwana Samatta aliifunga bao la kufutia machozi ambalo linaweza kuwa msaada kwa vijana hao wa Lubumbashi kwa mechi ya mkondo wa pili wikiendi hii.
Samatta tegemeo la Taifa Stars na Mchezaji Bora wa Mazembe kwa msimu uliopita alifunga bao hilo dakika mbili kabla ya kumalizika kwa pambano hilo.
Katika mechi nyingine za michuano hiyo ya Mabingwa Afrika, Horoya AC ya Guine ilikubali kichapo cha bao 1-0 kwa CS Sfaxien ya Tunisia, huku Cotonsport ya Cameroon ikidonyolewa kidude kimoja na ES Sétif ya Algeria wakiwa ugenini mjini Algers.
Katika michuano ya Kombe la Shirikisho, CS Constatine ya Algeria imeizabua ASEC Memosa ya Ivory Coast kwa bao 1-0.