STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, September 29, 2014

Vumbi Ligi Mabingwa Ulaya kutimka kesho

http://content.mcfc.co.uk/~/media/Images/Home/News/Team%20News/2014%2015%20season/Home%20Games/Chelsea%2021%20September/Group%20celebration%20close%20up.ashx?h=451&w=800
Manchester City watakuwa kubaruani kesho
https://pbs.twimg.com/media/Byc8SnZIcAAUeg-.jpg:large
http://e0.365dm.com/14/03/768x432/Bayern-Munich-celebrate_3101995.jpg?20140315195810
Bayern Munich kuendeleza ubabe wake Ulaya kesho?

MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu ya England, Manchester City kesho inatarajiwa kutypa karata yake nyingine katika Ligi ya Mabingwa Ulaya wakati itakapowakaribisha As Roma ya Italia kwenye uwanja wa Etihad.
City itashuka nyumbani ikiwa na kumbukumbu ya kichapo cha bao 1-0 toka kwa Bayern Munich katika mechi yao ya raundi ya kwanza ya michuano hiyo.
Ikihanikizwa na ushindi wa ligi ya nyumbani City itahitaji ushinfi katika mechi ya kesho ya Kundi E ili kujiweka katika nafasi nzuri ya kuwa miongoni mwa timu zitakazosonga mbele katika makundi.
Mbali na mechi hiyo inayotarajiwa kuwa na upinzani mkali kesho pia kutakuwa na michezo mingine kadhaa likiwamo pambano la CSKA Moscow ya Urusi itakayokuwa nyumbani kuvaana na Bayern Munich.
Katika mchezo wa kwanza CSKA ilichabangwa mabao 5-1 na Roma, hali inayofanya iwe na kazi ya ziada kama iliyonayo City katika kundi hilo.
Makundi mengine yatashuhudia timu za PSG watakuwa nyumbani kuikaribisha Barcelona katika mechi ya Kundi F, huku APOEL Nicosia ya Cyprus itawakaribisha Ajax ya Uholanzi.
Vinara wa EPL, Chelsea watakuwa ugenini mjini Lisbon kucheza na wenyeji wao Sporting Lisbon, katika mechi ya Kundi G ambalo pia litakuwa na pambano jingine kati ya NK Maribor ya Slovania itakayocheza na Schalke 04 ya Ujerumani.
BATE Borislov ya Belarus watawaialika Athletic Bilbao ya Hispania na Shakhtar Donetsk ya Ukraine wakiwa wenyeji wa FC Porto ya Ureno, hizo zikiwa mechi za kundi H.
Kipute kingine cha michuano hiyo kwa makundi yaliyobakia kitaendelea siku ya Jumatano.

Newz Alert! 200 wanusurika kifo Ruvuma kisa Togwa

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjO_S-l6Wfk0XGytRGNo_z8VxHh86vT54Eo2lXxFx74RVNuBVIyfcU3gfznTlm2molEPd2D4CDYNDyRg-K0THIp1m2ghBqMS87K9tPw0RwdyVvL5OoBAE9PxUnmBqQhJnlv6zBU7lnacT0/s640/DSCN1163.JPG
Picha haihusiani na habari hii, ingawa kinachoonekana pichani ni Togwa zikiwa sokoni

HABARI zilizotufika hivi punde zinasema zaidi ya watu 200 wamenusurika kufa baada ya kunywa Togwa linalosadikiwa kuwa na sumu katika kijiji cha Chitapwasi, mkoani Ruvuma.

Taarifa zaidi zitawajia kadri MICHARAZO itavayozipata kwa usahihi, ila inaelezwa baadhi ya walikumbwa na janga hilo wamekimbizwa katika vituo vya afya kwa ajili ya matibabu, japo haijafahamika kitu gani kilichosababisha watu hao kudhuriwa na togwa hilo, ingawa inahisiwa huenda ikawa na sumu.

Fainali Kombe la Shirikisho ni Al Ahly vs Sewe

http://www.en.beinsports.net/di/library/bein_sports/72/1d/ahly_3h4rvks5v5if1fs1rszi2ulm3.jpg?t=2095839318&w=670
Al Ahly ya Misri
http://en.starafrica.com/football/files/2013/04/615_340_SA_COTE-DIVOIRE_sewe-sport.jpg
Sewe Sports watakaokutana na Al Ahly kwenye fainali za Kombe la Shirikisho
BAADA ya kutemeshwa taji la Ligi ya Mabingwa Afrika, Al Ahly ya Misri imejiweka katika nafasi nzuri ya kujifariji kwa taji la Kombe la Shirikisho baada ya kufanikiwa kutinga Fainali ya michuano hiyo.
Timu hiyo iliyoing'oa Yanga kwenye mechi ya raundi ya pili ya Ligi ya Mabingwa mapema mwaka huu, imetinga hatua hiyo baada ya kuifunga Coton Sports ya Cameroon kwa mabao 2-1 katika nusu fainali.
Katika mechi ya kwanza Al Ahly walishinda ugenini bao 1-0 na ushindi huo wa jana umewafanya kufuzu Fainali kwa jumla ya mabao 3-1.
Kwa maana hiyo wababe hao wa Afrika watavaana na Sewe Sports ya Ivory Coast iliyotangulia mapema kwa kuinyoa AC Leopards ya Congo.
Mechi za hatua hiyo zitachezwa mwishoni mwa Novemba na mwanzoni mwa Desemba na kujulikana bingwa mpya wa michuano hiyo baada ya taji kuwa wazi lililokuwa likishikiliwa na Sfaxien ya Tunisia walioshiriki Ligi ya Mabingwa na kutolewa na AS Vita.

Rais JK kuzindua barabara ya Mwenge-Tegeta

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhMk0vSfAt8jHtAhakSB7WvHhsiQsyDQ3FoVsGoT4CpB8NFGVSWDMGy9-1pUHS72qegQZeRSFWebW5m5lv_B4-EU6g2bcOeMM9YVnPkQzhIBcv7Ic0C6xVbuGr8psoDH6RoLFLzsQQfcdGw/s640/Rais+Jakaya+Kikwete+%2528kati%2529+Balozi+wa+Japan+nchini+Hiroshi+Kanagawa+%2528kulia%2529+wakikata+utepe+na+Waziri+wa+Ujenzi+John+Mgufuli+aki.jpg
Rais Kikwete alipozundua ujenzi wa barabara hiyo

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhp1HUk3XqXz8wzRf9snLC3eY5TZp0maO9SMNksDsdurpQID42Ap96Wk5H78DmTjJq-GN6GxnPmCH6i3CQOTvsD6jNZ-P3oe-NWWnqretJxzG4GNmtGesW7yB8TP4w2iT_QRaUDPyfH_Cc/s1600/20140511_123729.jpg
Barabara ya Mwenge Tegeta

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika sherehe za ufunguzi wa barabara ya Mwenge –Tegeta yenye urefu wa kilometa 12.9 katika eneo la Lugalo, jijini Dar es salaam.  

Taarifa iliyotolewa leo jijini Dar es salaa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Muhandisi  Musa Iyombe imeeleza kuwa sherehe za ufunguzi wa barabara hiyo zitafanyika tarehe 1, Oktoba ,2014 katika eneo la Lugalo njia panda ya Kawe kuanzia saa nne asubuhi.
Taarifa  hiyo imeeleza kuwa kukamilika kwa upanuzi wa barabara hiyo yenye urefu wa kilometa 12.9 ni sehemu ya mkakati wa serikali wa kupunguza msongamano wa magari katika jiji la Dar es salaam.
Aron Msigwa –MAELEZO.
29/9/2014.
MWISHO.

TID 'Mnyama' kufyatua na Tumi Molakane

MNYAMA TID, yupo hatua ya mwisho kukamilisha 'ngoma' yake mpya inayoenda kwa jina la 'Bongo' aliyomshrikisha rapa kutoka Afrika Kusini aiywao Tumi Molakane.
Kazi hiyo ya kwanza kwa TID kufanya na msanii huyo maarufu nchini mwake, imerekodiwa katika studio za B Records.
TID alidokeza kuwa kwa kitambo kirefu alikuwa akimwinda rapa huyo na kufanya naye mawasiliano kupitia mitandao ya kompyuta kabla ya kumzukia Dar na kuingia naye studio kufanya wimbo huo.
Staa huyo wa 'Zeze', 'Girlfriend', 'Nyota' na 'Voice of Prison' aliwataka mashabiki wake wajiandae kusikia 'kolabo' hiyo wakati akifanya mchakato wa kwenda Afrika Kusini baadaye ili kutengeneza video yake.
"ViDeo ifanywa Afrika Kusini ili kuleta ladha kulingana na ushiriki wa Tumi," alisema TID..

Tanzia! Side Boy Mnyamwezi Hatunaye

HABARI zilizotufikia hivi punde zinasema kuwa aliyekuwa msanii wa Bongo Fleva aliyewahi kutamba na nyimbo za 'Kua uone', 'Usimdharau Usiyemjua' na Hujafa Hujaumbikam, Side Boy Mnyamwezi amefariki.
Kwa mujibu wa taarifa za mdogo wake Ally Khamis, Side Boy ambaye majina yake kamili ni Said Salum Hemed amefariki nyumbani kwao Lindi.
Taarifa zinasema kuwa marehemu kabla ya mauti yaliyomkuta katika Hospitali ya Mkoa wa Lindi ya Nyangao alikuwa akisubumbuliwa na maradhi ya TB.
MICHARAZO inawapa pole wote walioguswa na msiba huu, hasa ikizingatiwa iliwahi kuandika makala yake ndefu ya kisanii na mipango yake.
Mungu Ailaze Roho ya Marehemu Mahali Pema Peponi.