STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, September 29, 2014

Fainali Kombe la Shirikisho ni Al Ahly vs Sewe

http://www.en.beinsports.net/di/library/bein_sports/72/1d/ahly_3h4rvks5v5if1fs1rszi2ulm3.jpg?t=2095839318&w=670
Al Ahly ya Misri
http://en.starafrica.com/football/files/2013/04/615_340_SA_COTE-DIVOIRE_sewe-sport.jpg
Sewe Sports watakaokutana na Al Ahly kwenye fainali za Kombe la Shirikisho
BAADA ya kutemeshwa taji la Ligi ya Mabingwa Afrika, Al Ahly ya Misri imejiweka katika nafasi nzuri ya kujifariji kwa taji la Kombe la Shirikisho baada ya kufanikiwa kutinga Fainali ya michuano hiyo.
Timu hiyo iliyoing'oa Yanga kwenye mechi ya raundi ya pili ya Ligi ya Mabingwa mapema mwaka huu, imetinga hatua hiyo baada ya kuifunga Coton Sports ya Cameroon kwa mabao 2-1 katika nusu fainali.
Katika mechi ya kwanza Al Ahly walishinda ugenini bao 1-0 na ushindi huo wa jana umewafanya kufuzu Fainali kwa jumla ya mabao 3-1.
Kwa maana hiyo wababe hao wa Afrika watavaana na Sewe Sports ya Ivory Coast iliyotangulia mapema kwa kuinyoa AC Leopards ya Congo.
Mechi za hatua hiyo zitachezwa mwishoni mwa Novemba na mwanzoni mwa Desemba na kujulikana bingwa mpya wa michuano hiyo baada ya taji kuwa wazi lililokuwa likishikiliwa na Sfaxien ya Tunisia walioshiriki Ligi ya Mabingwa na kutolewa na AS Vita.

No comments:

Post a Comment