STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, January 23, 2013

Kinyambe aufungua mwaka na mpya

KInyambe akiwa katika pozi zake
MCHEKESHAJI anayezidi kutamba nchini kwa sasa, Mohammed Abdallah 'Kinyambe' ameufungua mwaka 2013 kwa kuachia filamu yake mpya iitwayo 'Urithi wa Kinyambe'.
Akizungunza na gazeti hili, Kinyambe anayefahamika pia kama James, alisema filamu hiyo tayari imeshaingia sokoni akiwa ameigiza na wasanii kadhaa maarufu nchini.
Kinyambe mwenyeji wa Mbeya, alisema baadhi ya wasanii alioigiza nao filamu hiyo ya vichekesho ni pamoja na Chrispin Masele 'Masele Chapombe' na Erick Ivyoivyo.
"Nimeuanza mwaka mpya kwa kuachia sokoni filamu yangu mpya ya komedi iitwayo 'Urithi wa Kinyambe' ambayo nimeigiza na wakali kadhaa akiwemo Masele na Erick Ivyo ivyo ninaotamba nao kwenye 'Vituko Show'," alisema Kinyambe.
Kinyambe alisema kazi hiyo mpya ni mwanzo wa raha alizojiandaa kuwapa mashabiki wake, kwani pia anajipanga kuwapa burudani katika muziki.
"Mashabiki wangu wakae tayari kupata vitu vizuri, kwani baada ya Urithi wa Kinyambe pia nakamilisha nyimbo zangu kadhaa ili niikamilishe albamu yangu," alisema.
Msanii huyo, alisema nyimbo mpya hizo zinakuja baada ya kuachia vibao vitatu tofauti kama 'Maumivu' alioimba na Baguje, 'Maimuna' alioimba na Leila Tot na Erick Ivyo ivyo na kile cha 'Kiduku Mpapaso' aliomshirikisha Kesse.

Baby J ataka ubunifu zaidi Bongofleva

Msanii Baby J
MSANII anayezidi kuja juu katika muziki wa kizazi kipya nchini, Jamila Abdullah 'Baby J', anayejiandaa kuachia hadharani wimbo wake mpya uitwao 'Nimempenda Mwenyewe' alioimba na Diamond, amewataka wasanii wenzake kuwa wabunifu na kulinda asili yao.
Baby J, alisema ubinifu na kulinda mila na asili ya kitanzania inaweza kuwa njia rahisi ya kujitambulisha kimataifa kuliko tabia ya kuiga kazi za watu na tamaduni za kigeni.
Akizungumza na MICHARAZO katika mahojiano maalum, msanii huyo anayetoka visiwani Zanzibar, Baby J alisema tabia ya kuiga kazi za wasanii wa nje au kuuiga utamaduni wa wa kigeni unawafanya wasanii wa Tanzania kushindwa kujitangaza kimataifa.
Baby J, alisema ni vema wasanii wakaumiza vichwa vyao kubuni vitu vyao wenyewe pamoja na kuhakikisha katika kazi zao zinaegemea katika mila na tamaduni za kitanzania ili hata zikishindanishwa nje ya nchi iwe rahisi kutambulika kuliko ilivyo sasa.
"Kwa kuwa muziki wetu umepiga hatua kubwa kwa sasa kulinganisha na siku za nyuma ni vema sasa wasanii wakabadilika na kubuni kazi zao wenyewe wakizingatia mila na asili ya Tanzania ili kujitambulisha kwa urahisi kimataifa," alisema.
Kuhusu mipango yake, Baby J, alisema kwa sasa yu mbioni kuachia hadharani wimbo wake wa nane uitwao 'Nimempenda Mwenyewe' aliomshirikisha Diamond.
"Wimbo umeshakamilika na utakuwa wimbo wangu wa nane baada ya awali kutoa nyimbo saba nilizoshirikisha wasanii kadhaa nyota kama Chid Benz, Pasha, Ally Kiba na Banana Zorro na wengine," alisema Baby J.
Msanii huyo ambaye ni mke wa mtu alianza kufahamika kwenye ulimwengu wa muziki mwaka 2006 alipotoka na wimbo uitwao 'Mpenzi wa Moyo' alioimba na Taqwa.

YANGA-MBIWA ASAINI MIAKA 5 NEWCASTLE

Mapou Yanga-Mbiwa

NEWCASTLE United wamemsajili beki Mapou Yanga-Mbiwa kutoka katika klabu ya Ufaransa ya Montpellier kwa ada isiyotajwa, inayoaminika kuwa ni paundi milioni 6.7.

Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ufaransa mwenye umri wa miaka 23 amesaini mkataba wa miaka mitano na nusu klabuni St James' Park.

Na mshambuliaji wa Bordeaux, Yoan Gouffran amebainisha kwamba pia anajiandaa kutua Newcastle leo.

Aliandika kwenye ukurasa wake wa Twitter:  "Kesho (leo) nitakuwa mchezaji mpya wa Newcastle na najivunia. Shukrani kwa kila mmoja."

Newcastle, ambao tayari wamemsajili beki wa kulia wa Ufaransa, Mathieu Debuchy katika kipindi hiki cha usajili cha Januari, pia wanakaribia kumsajili beki Massadio Haidara kutoka klabu ya Nancy ya Ufaransa pia.

Yanga-Mbiwa alikuwa nahodha wa Montpellier wakati wakitwaa taji lao la kwanza la Ligi Kuu ya Ufaransa, Ligue 1, msimu uliopita aliichezea klabu hiyo zaidi ya mechi 200.

"Ni heshima kutua katika klabu ya Newcastle United na kuwa na nafasi ya kucheza katika Ligi Kuu ya England," alisema. 


CHANZO:STRIKAMKALI

Arsene Wenger amvulia kofia Diame


LONDON, England
KOCHA wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger amemwagia sifa kiungo wa West Ham na ambaye wanamfukuzia kumnasa katika kipindi hikicha usajili wa dirisha dogo la Januari, Mohamed Diame.
Arsenal wamekuwa wakihusishwa mara kwa mara na usajili wa kiungo huyo mwenye miaka 25, anayeaminiwa kuwa na kipengele katika mkataba wake kinachomruhusu kuondoka ikiwa zitalipwa paundi za England milioni 3.5 (Sh. bilioni 9)
Diame ameonyesha kiwango cha juu na kuibuka kuwa mmoja wa wachezaji nyota wa klabu hiyo msimu huu, akifunga mabao mawili, yakiwamo dhidi ya Arsenal  katika mechi yake ya 18 tangu aanze kuichezea timu hiyo inayoongozwa na kocha Sam Allardyce.
Wenger ameongeza uvumi kuhusiana na kiungo huyo mwenye mwili 'jumba' wa timu ya taifa ya Senegal, akiwaambia waandishi wa habari: "Anafanya vitu vikubwa katika mechi, nimemuona akionyesha kiwango cha juu."
Arsenal ilifungwa 2-1 katika mechi yao dhidi ya Chelsea Jumapili, hivyo kuambulia pointi moja tu katika mechi tatu zilizopita za Ligi Kuu ya England ambazo zinawafanya waachwe kwa pointi saba na mahasimu wao katika kuwania nafasi ya nne kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya England, Tottenham na pia kulingana na Liverpool na West Brom ambao wote wana pointi 34.
Hata hivyo, kuna habari njema kwa Arsenal kufuatia taarifa za kupona kwa kiungo wao Mikel Arteta aliyekuwa nje kutokana na majeraha.

Azam yarejea nchini kamili gado

Kikosi cha Azam

MABINGWA wa Kombe la Mapinduzi, Azam Fc wanatarajiwa kurejea leo usiku Dar es Salaam, wakitokea Nairobi, Kenya walipokwenda kwa ziara ya wiki moja hya michezo ya kujipima nguvu kujiandaa na mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.
AZAM FC yenye maskani yake Chamazi, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam, ilihitimisha vema ziara yake hiyo jana, baada ya kuifunga timu ya Benki ya Biashara Kenya, KCB bao 1-0 kwenye Uwanja wa City, Nairobi jioni hii.
Bao pekee la ushindi la Azam jioni ya jana lilifungwa na kiungo Ibrahim Mwaipopo kwa shuti la mpira wa adhabu katika dakika ya pili ya muda wa nyongeza, baada ya kutimu kwa dakika 45 za kawaida za kipindi cha kwanza.
Hata hivyo, Azam ingeweza kuondoka na ushindi mnene zaidi jana, kama si kiungo wake mwingine Abdulhalim Humud ‘Gaucho’ kukosa penalti dakika ya 83 baada ya shuti lake la kudakwa na kipa wa KCB.
Huo unakuwa ushindi wa pili katika mechi zake tatu za kujipima nguvu nchini humo, kwani awali bao pekee la Gaudence Exavery Mwaikimba kwa penalti dakika ya 58 liliipa Azam FC ushindi wa 1-0 dhidi ya Sofapaka ya Kenya kwenye Uwanja wa Nyayo, Nairobi, Kenya.
Katika mchezo wake wa kwanza, mabingwa hao wa Kombe la Mapinduzi walifungwa mabao 2-1 na AFC Leopard kwenye Uwanja huo huo wa Nyayo.
Pamoja na kufungwa na Leopard, Azam watajilaumu wenyewe, kwani walipoteza penalti mbili kupitia kwa Joackins Atudo na Khamis Mcha ‘Vialli’.
Mabao ya Leopard katika mchezo huo, yalifungwa na Paul Were na Mike Barasa, wakati la Azam lilifungwa na Sammih Hajji Nuhu kwa penalti.
Azam ilimaliza mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ikiwa katika nafasi ya pili kwa pointi zake 24, nyuma ya vinara Yanga waliomaliza na pointi 29, wakati Simba walimaliza nafasi ya tatu kwa pointi zao 23.
Pamoja na Ligi Kuu, Azam pia itacheza Kombe la Shirikisho la Soka Afrika na itaanza na Al Nasir Juba ya Sudan Kusini mjini Dar es Salaam kati ya Februari 15 na 17 mwaka huu.
Mechi hiyo itachezeshwa na marefa wa Kenya, katikati Davies Omweno na atakayesaidiwa na mwamuzi msaidizi namba moja Peter Keireini, mwamuzi msaidizi namba mbili Gilbert Cheruiyot wakati mwamuzi wa mezani Anthony Ogwayo.
Kamisaa wa mechi hiyo atakuwa Hassan Mohamed Mohamud kutoka Somalia, wakati marefa wa mechi ya marudiano itakayochezwa mjini Juba wiki mbili baada ya mechi ya kwanza watatoka Rwanda, wakiongozwa na Gervais Munyanziza.


CHANZO:BIN ZUBEIRY

Simba yamalizana na akina Ochieng

Kamati ya Sheria, Maadili na Hadhi za Wachezaji iliyokutana Januari 19 mwaka huu chini ya Mwenyekiti wake Alex Mgongolwa, imeliondoa shauri lililokuwa mbele yake dhidi ya klabu ya Simba lililowasilishwa na wachezaji Pascal Ochieng na Daniel Akuffor baada ya pande hizo kufikia makubaliano.
Wachezaji hao kutoka Kenya na Uganda waliwasilisha malalamiko mbele ya kamati wakipinga kukatizwa mikataba yao bila kulipwa stahili zao. Hata hivyo, pande zimefikia makubaliano ya kuvunja mikataba nje ya kamati, na wachezaji hao kulipwa stahili zao.
Simba imekiri vilevile kudaiwa na wachezaji Shija Mkina, Swalehe Kabali, Victor Costa na Rajab Isiaka na kuahidi kuwalipa wachezaji hao wakati Coastal Union na mchezaji wake Mohamed Issa wamefikia makubaliano ya malipo, hivyo kuvunja mkataba kati ya pande hizo mbili.

Wakati huo huo kikosi cha timu hiyo ya Simba kilichokuwa Umangani kinatarajiwa kutua leo na kesho kikitarajiwa kushuka dimba la Taifa, Dar es Salaam kuvaana na Black Leopards ya Afrika Kusini.
Simba na Loepards watapambana katika mechi ya kirafiki ya kimataifa, ikitarajiwa kutambulisha mbinu walizojifunza wakiwa Oman.
Black Leopards leo wanatarajiwa kuvaana na Yanga katika pambano la marudiano litakalofanyika jijini Mwanza.
Pascal Ochieng
Katika mechi yao ya awali Yanga iliwalaza Waafrika Kusini haoa mabao 3-2, jijini Dar na pambano hilo la leo linatarajiwa kuwa na upinzani kila upande ukitamba kufanya kweli.

Masilahi yampeleka Kambi Msondo Ngoma

Muimbaji Athuman Kambi (wa pili toka kulia) akiwa na waimbaji wenzake wa Msondo Ngoma. Kutoka Kushoto ni Hassan Moshi , Eddo Sanga na Juma Katundu

MWANAMUZIKI mpya wa bendi ya Msondo Ngoma 'Baba ya Muziki', Athuman Kambi amesema kusaka masilahi na kujifunza zaidi muziki ndiko kulikomhamisha kutoka Mlimani Park 'Sikinde'.
Aidha muimbaji huyo anayeshabihiana sauti na mkongwe wa muziki wa dansi nchini, Hassani Rehani Bitchuka, amewaomba mashabiki wa Msondo kuwa na subira kabla ya kupata vitu adimu kutoka kwake.
Akizungumza na MICHARAZO, Kambi alisema hakuna kitu chochote kilichomtoa Sikinde na kutua Msondo zaidi ya kutafuta masilahi zaidi na pia kujifunza kwa wakongwe waliopo ndani ya bendi hiyo mpya aliyonayo.
Kambi alisema ameondoka Sikinde kwa amani na urafiki bila kugombana na mtu yeyote na kwamba hata kama mambo yatamshinda Msondo iwe rahisi kwake kurejea katika bendi hiyo iliyomtangaza hasa kwa kuweza kuimba kwa ufasaha sauti ya Bitchuka.
"Sijaondoka kwa ugomvi Sikinde, kilichonipeleka Msondo mbali na kusaka masilahi zaidi, lakini naamini nitaongeza ujuzi kwa kujifunza kutokwa wanamuziki waliopo ndani ya bendi hiyo," alisema.
Kambi aliongeza hana cha kuwaahidi kwa sasa Msondo zaidi ya kuomba wampe muda aweze kujipanga ili kuwapa vitu adimu ambavyo hawajawahi kuvipata.
"Wanipe muda nizoee mazingira kisha waone nitawapa kitu gani, ila nimejipanga kuwapa fadhila kwa namna walivyonipokea," alisema.
Muimbaji huyo alijiunga na Msondo wiki mbili zilizopita na tayari ameshaanza mazoezi na kushiriki maonyesho ya bendi hiyo.
-------

RATIBA MZUNGUKO WA PILI LIGI KUU TANZANIA BARA 





























































SECOND ROUND TANZANIA PREMIER LEAGUE






VODACOM PREMIER LEAGUE (VPL) FIXTURE 2012/2013






26TH JAN. 2013 - 18th MAY, 2013.






NO
DATE
No.
HOME TEAM
AWAY TEAM
STADIUM
VENUE






14
26. 01. 2013.
92
AFRICAN LYON FC
SIMBA SC
NATIOANAL STADIUM
DAR ES SALAAM






26. 01. 2013.
95
MTIBWA SUGAR FC
POLISI MOROGORO
Manungu
MOROGORO






27. 01. 2013.
94
YOUNG AFRICANS
TANZANIA PRISONS
NATIOANAL STADIUM
DAR ES SALAAM






26. 01. 2013.
95
COASTAL UNION
MGAMBO JKT
Mkwakwani
TANGA






26. 01. 2013.
96
RUVU SHOOTING
JKT RUVU
Mabatini
PWANI






26. 01. 2013.
97
AZAM FC
KAGERA SUGAR
AZAM COMPLEX
DAR ES SALAAM






26. 01. 2013.
98
JKT OLJORO
TOTO AFRICANS
Sh. Amri Abeid
ARUSHA












15
03.02.2013.
99
SIMBA SC
JKT RUVU
NATIOANAL STADIUM
DAR ES SALAAM






02.02.2013.
100
YOUNG AFRICANS
MTIBWA SUGAR FC FC
NATIOANAL STADIUM
DAR ES SALAAM






02.02.2013.
101
POLISI MOROGORO
AFRICAN LYON FC
Jamhuri
MOROGORO






02.02.2013.
102
MGAMBO JKT
RUVU SHOOTINGS
Mkwakwani
TANGA






03.02.2013.
103
COASTAL UNION
TANZANIA PRISONS
Mkwakwani
TANGA






30.01.2013.
104
JKT OLJORO
KAGERA SUGAR
Sh. Amri Abeid
ARUSHA






30.01.2013.
105
AZAM FC
TOTO AFRICANS
AZAM COMPLEX
DAR ES SALAAM






6/2 /2013 FIFA DATE FOR FRIEND MATCH






16
21.04.2013.
106
JKT RUVU
YOUNG AFRICANS
NATIOANAL STADIUM
DAR ES SALAAM






09.02.2013.
107
MTIBWA SUGAR FC
AZAM FC
AZAM COMPLEX
DAR ES SALAAM






02.03.2013.
108
POLISI MOROGORO
JKT OLJORO
JAMHURI
MOROGORO






09.02.2013.
109
TOTO AFRICANS
COASTAL UNION
CCM Kirumba
MWANZA






09.02.2013.
110
KAGERA SUGAR
MGAMBO JKT
Kaitaba
KAGERA






25.04.2013.
111
RUVU SHOOTINGS
SIMBA SC
NATIOANAL STADIUM
DAR ES SALAAM






09.02.2013.
112
TANZANIA PRISONS
AFRICAN LYON FC
SOKOINE
MBEYA






15 - 17. FEB. 2012 PRELIMINARY CL & CC FIRST LEG






17
13.02.2013.
113
KAGERA SUGAR
COASTAL UNION
Kaitaba
KAGERA






20.02.2013.
114
JKT RUVU
AZAM FC
AZAM COMPLEX
DAR ES SALAAM






13.02.2013.
115
TOTO AFRICANS
POLISI MOROGORO
CCM KIRUMBA
MWANZA






13.02.2013.
116
MGAMBO JKT
JKT OLJORO
MKWAKWANI
TANGA






13.02.2013.
117
MTIBWA SUGAR FC
RUVU SHOOTING
MANUNGU
MOROGORO






20.02.2013.
118
TANZANIA PRISONS
SIMBA SC
SOKOINE
MBEYA






13.02.2013.
119
AFRICAN LYON FC
YOUNG AFRICANS
NATIONAL STADIUM
DAR ES SALAAM












18
23.02.2013.
120
YOUNG AFRICANS
AZAM FC
NATIOANAL STADIUM
DAR ES SALAAM






24.02.2013.
121
SIMBA SC
MTIBWA SUGAR FC
NATIOANAL STADIUM
DAR ES SALAAM






20.02.2013.
122
COASTAL UNION
JKT OLJORO
Mkwakwani
TANGA






20.02.2013.
123
TOTO AFRICANS
AFRICAN LYON FC
CCM KIRUMBA
MWANZA






11.05.2013.
124
KAGERA SUGAR
RUVU SHOOTINGS
Kaitaba
KAGERA






23.02.2013.
125
MGAMBO JKT
JKT RUVU
Mkwakwani
TANGA






23.02.2013.
126
TANZANIA PRISONS
POLISI MOROGORO
SOKOINE
MBEYA












NO
DATE
No.
HOME TEAM
AWAY TEAM
STADIUM
VENUE






01 - 03. MARCH. 2013 PRELIMINARY CL & CC SECOND LEG






19
10.04.2013.
127
AZAM FC
AFRICAN LYON FC
AZAM COMPLEX
DAR ES SALAAM






27.02.2013.
128
COASTAL UNION
RUVU SHOOTING 
MKWAKWANI
TANGA






09.02.2013.
129
JKT OLJORO
SIMBA SC
Sh. Amri Abeid
ARUSHA






27.02.2013.
130
YOUNG AFRICANS
KAGERA SUGAR
NATIOANAL STADIUM
DAR ES SALAAM






27.02.2013.
131
POLISI MOROGORO
MGAMBO JKT
JAMHURI
MOROGORO






27.02.2013.
132
JKT RUVU
TOTO AFRICANS
AZAM COMPLEX
DAR ES SALAAM






27.02.2013.
133
MTIBWA SUGAR FC
TANZANIA PRISONS
MANUNGU
MOROGORO












20
07.03.2013.
134
JKT RUVU
KAGERA SUGAR
AZAM COMPLEX
DAR ES SALAAM






09.03.2013.
135
YOUNG AFRICANS
TOTO AFRICANS
NATIOANAL STADIUM
DAR ES SALAAM






09.03.2013.
136
AZAM FC
POLISI MOROGORO
AZAM COMPLEX
DAR ES SALAAM






06.03.2013.
137
JKT OLJORO
TANZANIA PRISONS
Sh. Amri Abeid
ARUSHA






10.03.2013.
138
SIMBA SC
COASTAL UNION
NATIOANAL STADIUM
DAR ES SALAAM






06.03.2013.
139
AFRICAN LYON FC
RUVU SHOOTINGS
AZAM COMPLEX
DAR ES SALAAM






06.03.2013.
140
MGAMBO JKT
MTIBWA SUGAR FC FC
MKWAKWANI
TANGA






15/3 - 17/3/2013 1/16 CL & CC FIRST LEAGUE






21
27.03.2013.
141
AZAM FC
TANZANIA PRISONS
AZAM COMPLEX
DAR ES SALAAM






17.03.2013.
142
JKT RUVU
POLISI MOROGORO
AZAM COMPLEX
DAR ES SALAAM






27.03.2013.
143
KAGERA SUGAR
SIMBA SC
Kaitaba
KAGERA






16.03.2013.
144
TOTO AFRICANS
MGAMBO JKT
CCM KIRUMBA
MWANZA






18.03.2013.
145
AFRICANS LYON
JKT OLJORO
AZAM COMPLEX
DAR ES SALAAM






16.03.2013.
146
RUVU SHOOTINGS
YOUNG AFRICANS
NATIOANAL STADIUM
DAR ES SALAAM






16.03.2013.
147
MTIBWA SUGAR FC
COASTAL UNION
MANUNGU
DAR ES SALAAM






22 - 24. MARCH. 2013. WC QUALIFIER BRAZIL - 2014






22
30.03.2013.
148
JKT OLJORO
JKT RUVU
SH. AMRI ABEID
ARUSHA






08.05.2013.
149
SIMBA SC
MGAMBO JKT
NATIOANAL STADIUM
DAR ES SALAAM






03.04.2013.
150
TOTO AFRICANS
TANZANIA PRISONS
CCM KIRUMBA
MWANZA






30.03.2013.
151
RUVU SHOOTINGS
AZAM FC
MABATINI
PWANI






30.03.2013.
152
AFRICAN LYON FC
COASTAL UNION
AZAM COMPLEX
KAGERA






30.03.2013.
153
POLISI MOROGORO
YOUNG AFRICANS
JAMHURI
MOROGORO






30.03.2013.
154
KAGERA SUGAR
MTIBWA SUGAR FC FC
Kaitaba
KAGERA






05 - 06 APRIL. 2013. 1/16TH CL & CC SECOND LEG






23
13.04.2013.
155
AZAM FC
SIMBA SC
NATIOANAL STADIUM
DAR ES SALAAM






10.04.2013.
156
YOUNG AFRICANS
JKT OLJORO
NATIOANAL STADIUM
DAR ES SALAAM






23.03.2013.
157
KAGERA SUGAR
AFRICAN LYON FC
Kaitaba
KAGERA






10.04.2013.
158
TANZANIA PRISONS
MGAMBO JKT
SOKOINE
MBEYA






10.04.2013.
159
POLISI MOROGORO
RUVU SHOOTINGS
JAMHURI
MOROGORO






10.04.2013.
160
COASTAL UNION
JKT RUVU
MKWAKWANI
TANGA






10.04.2013.
161
MTIBWA SUGAR FC
TOTO AFRICANS
MANUNGU
MOROGORO






19 - 21 APRIL. 2013.  1/8TH FINAL CL & CC FIRST LEG






24
13.04.2013.
162
MGAMBO JKT
YOUNG AFRICANS
MKWAKWANI
TANGA






28.04.2013.
163
SIMBA SC
POLISI MOROGORO
NATIOANAL STADIUM
DAR ES SALAAM






17.04.2013.
164
KAGERA SUGAR
TOTO AFRICANS
Kaitaba
KAGERA






17.04.2013.
165
AFRICAN LYON FC
JKT RUVU
AZAM COMPLEX
DAR ES SALAAM






13.04.2013.
166
MTIBWA SUGAR FC
JKT OLJORO
MANUNGU
MOROGORO






13.04.2013.
167
TANZANIA PRISONS
RUVU SHOOTINGS
SOKOINE
MBEYA






27.04.2013.
168
COASTAL UNION
AZAM FC
MKWAKWANI
TANGA
























03 - 05. MAY. 2013.  1/8TH FINAL CL & CC SECOND LEG






NO
DATE
No.
HOME TEAM
AWAY TEAM
STADIUM
VENUE






25
11.05.2013.
169
AZAM FC
MGAMBO JKT
AZAM COMPLEX
DAR ES SALAAM






01.05.2013.
170
MTIBWA
AFRICAN LYON FC
MANUNGU
MOROGORO






30.03.2013.
171
TOTO AFRICANS
SIMBA SC
CCM KIRUMBA
MWANZA






01.05.2013.
172
YOUNG AFRICANS
COASTAL UNION
Mkwakwani
TANGA






01.05.2013.
173
JKT RUVU
TANZANIA PRISONS
AZAM COMPLEX
DAR ES SALAAM






01.05.2013.
174
POLISI MOROGORO
KAGERA SUGAR
JAMHURI
MOROGORO






01.05.2013.
175
RUVU SHOOTINGS
JKT OLJORO
MABATINI
PWANI












26
18.05.2013.
176
TOTO AFRICANS
RUVU SHOOTINGS
CCM KIRUMBA
MWANZA






18.05.2013.
177
MGAMBO JKT
AFRICAN LYON FC
Mkwakwani
TANGA






18.05.2013.
178
JKT RUVU
MTIBWA SUGAR FC FC
AZAM COMPLEX
DAR ES SALAAM






18.05.2013.
179
TANZANIA PRISONS
KAGERA SUGAR
SOKOINE
MBEYA






18.05.2013.
180
SIMBA SC
YOUNG AFRICANS
NATIONAL STADIUM
DAR ES SALAAM






18.05.2013.
181
JKT OLJORO
AZAM FC
SH. AMRI ABEID
ARUSHA






18.05.2013.
182
POLISI MOROGORO
COASTAL UNION
Jamhuri
MOROGORO

























* Endapo timu za Simba SC na Azam FC hazitafanikiwa kuvuka hatua mojawapo ya mashindano ya CL &






CC Orange 2013 ratiba itafanyiwa marekebi