STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, December 11, 2012

Linah: 'Napenda kubambiwa na mashabiki'







Linah Sanga katika mwonekano wa picha tofauti.
 
Na Kambi Mbwana, Handeni
MWIMBAJI wa  muziki wa kizazi kipya hapa nchini, Linah Sanga, maarufu kama Lina, amesema huwa haogopi kubambiwa na mashabiki wake, ndio maana amekuwa mwepesi kuwahitaji kila anavyofanya shoo zake.

Linah aliyeibukia katika taasisi ya kukuza na kulea vipaji ya Tanzania House of Talents (THT), ni miongoni mwa  wasanii wanaofanya vyema mno katika tasnia ya muziki wa kizazi kipya nchini.
 

Akizungumza na Handeni Kwetu, Linah alisema kwamba anapenda kucheza na mashabiki wake kila anavyoona inafaa, hivyo anaamini aina hiyo itaendelea kwa ajili ya kujipa amani na kuwapa fursa mashabiki wake kucheza nae jukwaani.

Alisema katika maeneo mengi, hasa kwa kuangalia amani, amekuwa akihitaji mmoja wao kwa ajili ya kuacha amani na heshima kwa mashabiki wake, hivyo lengo lake haliwezi kusitishwa na woga wa kucheza, au kubambiwa na mashabiki wake.

"Huwa napenda sana kucheza na shabiki wangu katika shoo ninazofanya, hivyo siogopi kubambiwa, ingawa najua watu ukiwapa nafasi hiyo wanakuja jukwaani na kucheza kwa fujo hasa wale wanaowakamia wasanii.

"Nafanya hivyo kwakuwa sina woga na ndio maana mashabiki wangu nawaacha katika furaha kwa kushangilia, hivyo kwakweli hili ni lengo langu zaidi, ili mradi tu kuwe na amani kwa kuimarishwa ulinzi, hasa katika shoo kubwa.

Linah amewahi kutamba na nyimbo mbalimbali, ukiwamo ule wa ‘Atatamani’, uliomuweka juu na kumpatia mashabiki lukuki.

NMB YAKABIDHI MADAWATI SHULE YA MSINGI VICTORIA


Meneja wa benki ya NMB tawi la NMB House Bi. Benedictor Byabyato (kulia) akikabidhi madawati 25 yenye thamani ya shilingi milioni 5 kwa Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Victoria Bw. Sufini Mbwambo iliyopo Dar es Salaam wiki iliyopita.Aanayeshuhudia tukio hilo ni Afisa wa tawi la NMB House Jane Mubezina pamoja na mmoja wa maafisa wa Elimu.
 
Meneja wa tawi la NMB House  Bi. Benedictor Byabyato (kulia) akiwa pamoja na baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Msingi Victoria pamoja na Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Bw. Sufini Mbwambo (kulia) wakati wa makabidhiano ya madati yenye thamani ya shilingi milioni 5, jijini Dar es Salaam.
Wanafunzi wa Shule ya Msingi Victoria wakiimba nyimbo kushukuru benki ya NMB kwa msaada wa madawati waliyotoa shuleni hapo

NMB YAKABIDHI MADAWATI SHULE YA MSINGI VICTORIA


Meneja wa benki ya NMB tawi la NMB House Bi. Benedictor Byabyato (kulia) akikabidhi madawati 25 yenye thamani ya shilingi milioni 5 kwa Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Victoria Bw. Sufini Mbwambo iliyopo Dar es Salaam wiki iliyopita.Aanayeshuhudia tukio hilo ni Afisa wa tawi la NMB House Jane Mubezina pamoja na mmoja wa maafisa wa Elimu.
 
Meneja wa tawi la NMB House  Bi. Benedictor Byabyato (kulia) akiwa pamoja na baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Msingi Victoria pamoja na Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Bw. Sufini Mbwambo (kulia) wakati wa makabidhiano ya madati yenye thamani ya shilingi milioni 5, jijini Dar es Salaam.
Wanafunzi wa Shule ya Msingi Victoria wakiimba nyimbo kushukuru benki ya NMB kwa msaada wa madawati waliyotoa shuleni hapo

JOKHA KASSIM Mwimbaji wa taarabu anayetamba na T-Moto


Jokha Kassim
 
Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
UKIPATA bahati ya kuusikia wimbo wa Riziki Mafungu Saba, hakika utaanza kuupenda muziki wa taarabu, hata kama awali hujaupenda.
 
Ni wimbo mzuri. Wenye mashairi mazito na yenye ujumbe murua, unaoelezea jinsi riziki zinavyopangwa na Mungu na wala sio binadamu, wakiwamo wenye roho mbaya.
 
Wimbo huo umeimbwa na mwanamama Jokha Kassim, alipokuwa na kundi zima la Zanzibar Stars Modern Taarab.
 
Kwa sasa Jokha anafanya kazi katika kundi zima la Tanzania Moto Modern Taarab, maarufu kama T-Moto, lenye wakali wengine kibao.
 
Tayari Jokha amerekodi wimbo unaokwenda kwa jina la ‘Domo la Udaku’, ukiwa ni ujio mpya wa kundi hilo la taarabu nchini.
 
Mwimbaji huyo juzi alifanya mazungumzo na Fiesta Magazine na kusema kuwa muziki ni kipaji chake, alichobarikiwa na Mungu.
 
Cheche zake zilianza kuonekana tangu zamani, alipokuwa hodari sana wa kuimba nyimbo mbalimbali za taarabu.
 
“Muziki huu ni kipaji changu, tangu zamani niliweza kuimba kwa ufanisi na kushangaza wengi waliokuwa wakiona mahala popote.
 
“Nashukuru, leo hii nimeweza kufanya juhudi na kufika T-Moto, ikiwa ni baada ya kujulikana nilipofanya kazi na Zanzibar Stars kwa mafanikio makubwa,” alisema.
 
Licha ya kuanza zamani kuimba, lakini alianza kuingia kwenye kundi la muziki mwaka 2002, alipohitajiwa na uongozi wa Zanzibar Stars na kumtambulisha kimuziki.
 
Kilichomkwamisha kuingia mapema kwenye sanaa ni kukatazwa na wazazi wake, hivyo kusubiri hadi mwaka huo alipoanza kushika kipaza sauti na kurindimisha sauti yake.
 
Jokha alikuwa mke wa kwanza wa Mfalme, Mzee Yusuph, ila kwa sasa wameachana na kila mmoja anaishi kivyake.
 
Siku chache baada ya kuachana na mzee Yusuph, hamu ya kuimba ilimtesa, hivyo kuamua kufanya harakati za kuibua kipaji chake.
 
Jokha na Mzee Yusuph wamezaa mtoto mmoja, ambaye pia ni mwimbaji na Mkurugenzi wa kundi la Jahazi Modern Taarab.
 
“Nilifanya kazi ya ziada kuingia kwenye muziki, maana baba yangu hakupenda suala hilo, hivyo kunipa wakati mgumu.
 
“Hata hivyo Mungu akipanga lake hakuna wa kuweza kutengua, ndio maana nimeweza kufika hatua hii na kujulikana sehemu kubwa kupitia soko la muziki wa taarabu,” alisema.
 
Mwimbaji huyo mwenye mvuto wa aina yake, anashindwa kubainisha chanzo cha kuvunjika kwa ndoa yake na mume wake Mzee Yusuph.
 
Anasema riziki imekwisha kwa ndoa yao, huku akisema bado wanaheshimiana kwasababu wameachana bila kuwa na ugomvi, huku wakifanikiwa kupata mtoto mmoja, aliyepewa jina la Yusuph Mzee Yusuph.
 
Muziki wa taarabu unazidi kufanya vizuri kutokana na waimbaji wake wengi kuwa wabunifu.
 
Katika hilo anaamini kuwa mambo yatazidi kuwa mazuri, huku mashabiki wakipata vitu adimu kutoka kwao.
 
Mwimbaji huyo anavutiwa na mkali wa muziki huo nchini, Zuhura Shaaban.
 
Katika kundi lake la T-Moto, Jokha ameimba nyimbo zaidi ya tatu, ukiwamo wa ‘Unavyojidhani Haufanani’ ‘Mimi ni Star’ na ‘Aliyeniumba Hajanikosea’, ambao ulibeba jina la albamu ya kwanza.
 
Kwa albamu hii mpya inayoandaliwa, Jokha amesharekodi wimbo mmoja unaokwenda kwa jina la Domo la Udaku.
 
Katika hilo, ni wazi kuwa wao watakuwa juu zaidi, maana bendi nyingi zimekosa ubunifu na mikakati ya kimuziki.
 
“Kwenye muziki kumekuwa na ushindani, hivyo nadhani kinachotakiwa ni mipango, mikakati pamoja na nyimbo nzuri.
 
“Sisi tunavyo vitu hivyo, nadhani ni wakati wetu kuwa kileleni maana mashabiki wana kiu ya kuona mambo yetu yanakuwa mazuri,” alisema.
 
Jokha alizaliwa miaka kadhaa iliyopita, Zanzibar, katika Hospitali ya Mnazi Mmoja.
 
Elimu ya Msingi aliipata katika shule ya Darajani na kuhitimu mwaka 1995 ile ya Sekondari aliipata kwenye shule ya Haile Selasi.
 
Mbali na Jokha, wengine wanaopatikana kwenye kundi hilo ni pamoja na Nyawana Fundikira, Aisha Masanja, Shimuna Kassim, Amina Rashid, Hanifa Juma, Shaban Ramadhan, Mrisho Rajabu, Rahma Omari, Silver Mwandilee, Kasikile Msukule na wengineo.
You might also like:

Azam hatimaye yaiangukia Simba kuhusu Ngassa wakubali kugawa mgao wa usajili kwa wana Msimbazi


KLABU ya soka ya Azam imeuangukia uongozi wa klabu ya Simba wakiwaomba walimalize suala la nyota wao Mrisho Ngassa kwa njia ya amani mradi winga huyo awahi kwenda kufanyia vipimo kwa lengo la kutua rasmi katika klabu ya El Merreikh ya Sudan.
Kwa mujibu wa taarifa zilizopatikana jana jioni na kuthibitishwa na Katibu Msaidizi wa Azam, Twalim Suleiman 'Chuma' ni kwamba Azam imeuandikia barua uongozi wa Simba ukisema wapo tayari kuwapa sehemu ya fedha za usajili za Ngassa, mradi waondoe pingamizi lao lililopo TFF kabla ya saa 5 asubuhi ya leo.
Barua hiyo iliyosainiwa na Makamu Mwenyekiti wa Azam, Shani Cristom, imesema kuwa kwa vile muda wa usajili wa wachezaji kwa El Merreikh ni mfupi wangeomba Simba kutumia uungwana ili kumruhusu Ngassa aende Sudan kufanyiwa vipimo vya afya baada ya awali kusaini mkataba wa miaka miwili kuichezea timu hiyo.
Pia barua hiyo inasema Azam wapo tayari kuwapa Simba Dola za Kimarekani 25,000 na wapo (Azam) kusaliwa na Dola 50,000 katika Dola 75,000 za kumuuzia Ngassa, na kuutaka uongozi huo wa Simba kuhakikisha suala la mchezaji huyo ikiwemo kuondoa pingamizi lao TFF linafanyika kabla ya saa 5 asubuhi.
Katibu Msaidizi wa Azam, Twalib Chuma alikiri kuandikwa kwa barua hiyo na kutumwa kwa uongozi wa Simba na nakala kupelekwa TFF akisema lengo ni kuhakikisha Ngassa anapata fursa ya kujiunga na timu ya El Merreikh inayoshiriki Ligi ya Mabingwa wa Afrika mwakani.
"NI keli tumewaandikia barua Simba na kutuma nakala TFF kwa sababu ya kutaka kulimaliza suala la Ngassa kiungwana ili kumpa nafasi mchezaji huyo kwenda kucheza soka la kulipwa Sudan kwa manufaa ya taifa," alisema.
Twalib alisema anadhani jambo hilo la Ngassa litaisha kwa amani na kila upande kuridhia, japo walisema hawakuona sababu ya kulumbana na Simba ilihali klabu zote zipo kwa maendeleo ya soka la Tanzania.
Habari nyingine zilizotufikia asubuhi hii zinasema kuwa, pande mbili za klabu hizo wanatarajia kukutana kwa ajili ya kusaini makubaliano mapya juu ya uhamisho wa nyota huyo alioyeng'ara katika michuano ya Kombe la Chalenji iliyomalizika nchini Uganda hivi karibuni.





KIM POULSEN AWATAJA ASKARI WA KUWAVAA WAZAMBIA 

KOCHA wa Taifa Stars, Kim Poulsen ametangaza kikosi cha wachezaji 24 kitakachoingia kambini jioni ya Desemba 12 mwaka huu kuajianda kwa mechi ya kirafiki dhidi ya mabingwa wa Afrika, Zambia.

Katika kikosi hicho, wachezaji walioitwa kwa mara ya kwanza ni kipa Aishi Manula anachezea kikosi cha U20 cha Azam na timu ya Taifa kwa vijana wenye umri chini ya miaka 20 (Ngorongoro Heroes), beki wa kushoto wa Azam, Samih Nuhu, beki wa kushoto wa Mtibwa Sugar, Issa Rashid na mshambuliaji wa Azam, Mcha Khamis.

Pia kati ya wachezaji walioitwa, sita walikuwa kwenye kikosi cha Zanzibar (Zanzibar Heroes) kilichokamata nafasi ya tatu katika michuano ya Kombe la Chalenji iliyomalizika Jumamosi jijini Kamapala, Uganda. Wachezaji hao ni Mwadini Ally, Nassoro Masoud Cholo, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Samih Nuhu, Aggrey Morris na Mcha Khamis.

Kikosi kamili kilichoitwa ni makipa; Juma Kaseja (Simba), Mwadini Ally na Aishi Manula (Azam U20). Mabeki ni Shomari Kapombe (Simba), Erasto Nyoni (Azam), Nassoro Masoud Cholo (Simba), Aggrey Morris (Azam), Samih Nuhu (Azam), Nadir Haroub ‘Cannavaro’ (Yanga), Amir Maftah (Simba), Issa Rashid (Mtibwa Sugar) na Kevin Yondani (Simba).

Viungo ni Frank Domayo (Yanga), Athuman Idd Chuji (Yanga), Mrisho Ngasa (Simba), Shabani Nditi (Mtibwa Sugar), Mcha Khamis (Azam), Salum Abubakar (Azam), Amri Kiemba (Simba) na Mbwana Samata (TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo- DRC).

Washambuliaji ni John Bocco (Azam), Simon Msuva (Yanga), Thomas Ulimwengu (TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo- DRC) na Mwinyi Kazimoto (Simba).