STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, December 11, 2012

Linah: 'Napenda kubambiwa na mashabiki'







Linah Sanga katika mwonekano wa picha tofauti.
 
Na Kambi Mbwana, Handeni
MWIMBAJI wa  muziki wa kizazi kipya hapa nchini, Linah Sanga, maarufu kama Lina, amesema huwa haogopi kubambiwa na mashabiki wake, ndio maana amekuwa mwepesi kuwahitaji kila anavyofanya shoo zake.

Linah aliyeibukia katika taasisi ya kukuza na kulea vipaji ya Tanzania House of Talents (THT), ni miongoni mwa  wasanii wanaofanya vyema mno katika tasnia ya muziki wa kizazi kipya nchini.
 

Akizungumza na Handeni Kwetu, Linah alisema kwamba anapenda kucheza na mashabiki wake kila anavyoona inafaa, hivyo anaamini aina hiyo itaendelea kwa ajili ya kujipa amani na kuwapa fursa mashabiki wake kucheza nae jukwaani.

Alisema katika maeneo mengi, hasa kwa kuangalia amani, amekuwa akihitaji mmoja wao kwa ajili ya kuacha amani na heshima kwa mashabiki wake, hivyo lengo lake haliwezi kusitishwa na woga wa kucheza, au kubambiwa na mashabiki wake.

"Huwa napenda sana kucheza na shabiki wangu katika shoo ninazofanya, hivyo siogopi kubambiwa, ingawa najua watu ukiwapa nafasi hiyo wanakuja jukwaani na kucheza kwa fujo hasa wale wanaowakamia wasanii.

"Nafanya hivyo kwakuwa sina woga na ndio maana mashabiki wangu nawaacha katika furaha kwa kushangilia, hivyo kwakweli hili ni lengo langu zaidi, ili mradi tu kuwe na amani kwa kuimarishwa ulinzi, hasa katika shoo kubwa.

Linah amewahi kutamba na nyimbo mbalimbali, ukiwamo ule wa ‘Atatamani’, uliomuweka juu na kumpatia mashabiki lukuki.

No comments:

Post a Comment