STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, April 13, 2013

Prisons yazidi kukimbia janga la kushuka daraja


MAAFANDE wa Prisons Mbeya wamezidi kupigana kuepa janga la kushuka daraja baada ya kuinyoa Ruvu Shooting kwa mabao 2-0 katika pambano lililochezwa jioni ya leo mjini Mbeya.

Ushindi huo ni wa pili mfululizo baada ya Jumatano iliyopita kuicharaza Mgambo JKT, ulipatikana kwenye uwanja wa Sokoine na kuifanya Prisons kuchupa kwa nafasi moja toka nafasi ya 10 haid ya 9.
Hata hivyo bado Prisons ina kibarua cha kuhakikisha wanashinda mechi zao mbili zilizosalia dhidi ya JKT Ruvu na Kagera Sugar kujihakikishia kusalia Ligi Kuu msimu ujao.
Habari kutoka Mbeya zinasema kuwa Mabingwa hao wa zamani wa Tanzania walipata ushindi huo kwa magoli ya kipindi cha pili yaliyowekwa yote kimiani na mchezaji wake aliyekuw shujaa leo, Elias Maguli.Maguli alifunga bao la kwanza kwa shuti akiunganisha pasi murua ya mchezaji mwenzake katika dakika ya 53 kabla ya kuongeza jingine dakika tano baadaye kwa mkwaju wa penati baada ya beki mmoja wa Ruvu kuunawa mpira langoni mwake.
Kwa matokleo hayop Prisons imefikisha pointi 26 na kuishuka Mgambo katika nafasi ya tisa na kukalia wao nafasi hiyo.

Ligi hiyo inatarajiwa kuendelea tena kesho kwa pambano kati ya Azam na Simba litakalochezwa kwenye uwanja wa Taifa.

 Msimamo wa Ligi hiyo baada ya mechi za leo jioni;

                                        P     W     D    L     F     A     D     PTS
    1.  Young Africans     22     16    4     2    40   12    +28     52
    2.  Azam                     22     14    4     4    39   17    +22     46    
    3.  Kagera Sugar         22     10    7     5    25   18    +7       37     
    4.  Simba                     21     9     8     4     30   19   +11      35
    5.  Mtibwa Sugar        23      8     9     6     26   24    +2      33   
    6. Coastal Union         22     8     8     6     23    20    +3      32    
    7.  Ruvu Shooting       23     8     6     9     21     22     -1     30     
    8.  JKT Oljoro FC       23     7     7     9     22     27     -5     28     
    9. Tanzania Prisons     24     6     8    10    14     21     -7     26    
   10.JKT Mgambo          22     7     3    12    14     22     -8     24
   11.Ruvu Stars              21     6     4     11    19     34     -15   22
   12. Toto Africans        24     4     10    10    22    32     -10    22
   13.  African Lyon       23     5      4     14    16     35     -19   19
   14. Polisi Morogoro    23     3     10    10    11     21     -10   19    
             

Yanga yaitemesha Simba ubingwa, yaikwangua JKT Oljoro 3-0

Vinara wa ligi kuu Yanga walioivua Simba taji jioni ya leo
VINARA wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga imeendelea kudhihirisha wamepania kutwaa taji la msimu huu baada ya jioni hii kuikwangua JKT Oljoro ya Arusha mabao 3-0 katika pambano lililochezwa kwenye uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam.
Ushindi huo uliopatikana kwa mabao ya kipindi cha kwanza yameifanya Yanga kuendelea kujikita kileleni mwa msimamo wa ligi hiyo ikiwa na pointi 52 na kuivua rasmi Simba ubingwa kutokana na kufikisha pointi 52 ambazo haziwezi kufikiwa na Wana Msimbazi.
Simba ambayo itashula kesho dimbani kuumana na Azam yenyewe ina pointi 35 na kama itashinda mechi zake zote itafikisha pointi 50 tu.
Mabao yalioifanya Yanga kulishika taji la ubingwa kwa mkono mmoja na kusubiri mwingine iwapo Azam wanaowafukuzia watateleza katika mechi zake yaliwekwa kimiani na beki Nadir Haroub 'Cannavaro' katika dakika ya 5 tu ya mchezo kabla ya Simon Msuva kufunga la pili dakika ya 19 na Hamis Kiiza 'Diego' kuongeza la tatu dakika mbili kabla ya mapumziko.
Pambano hilo lililochezeshwa na mwamuzi Amon Paul wa Mara lilihuhudia kadi kadhaa za njano zikitolewa kwenye mchezo huo na mpaka dakika 90 zinamalizika Yanga walikuwa wababe mbele ya maafande hao kwa ushindi huo wa mabao 3-0.

Supersport yakwama kurusha live mechi za VPL

PRESS RELEASE



Na Boniface Wambura
MECHI tano kati ya sita za Super Week za Ligi Kuu ya Vodacom zilizokuwa zioneshwe moja kwa moja (live) na Kituo cha televisheni cha SuperSport cha Afrika Kusini sasa hazitaoneshwa kutokana na matatizo ya kiufundi.

Kwa mujibu wa Mtayarishaji Mtendaji (Executive Producer) wa SuperSport Kanda ya Afrika, Max Tshunungwa ambaye yuko nchini, wameshindwa kuonesha mechi hizo kutokana na matatizo ya kiufundi katika magari yao ya kurushia matangazo (OB van) yanayohudumia Afrika Mashariki- Kenya, Tanzania na Uganda.

Mechi hizo ni kati ya Azam na African Lyon, Yanga na Oljoro JKT, Azam na Simba, Coastal Union na JKT Ruvu na Mgambo Shooting na Yanga itakayochezwa Aprili 17 mwaka huu jijini Tanga.

Tatizo hilo pia limeathiri mechi za Ligi Kuu ya Kenya (KPL) ambazo hazitaonekana wikiendi hii. SuperSport ndiyo yenye haki za matangazo ya televisheni kwa ligi hiyo ya Kenya.

Tshunungwa amekutana na Sekretarieti ya TFF na Kamati ya Ligi kuelezea tatizo hilo. SuperSport kwa kushirikiana na Kamati ya Ligi na TFF watapanga mechi nyingine za Super Week kabla ya ligi kumalizika msimu huu.

Pia TFF, Kamati ya Ligi na SuperSport watakuwa na mkutano mfupi wa waandishi wa habari wakati wa mapumziko kwenye mechi ya leo kati ya Yanga na Oljoro JKT kwenye Uwanja wa Taifa.

ZA LEO LEO