STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, February 28, 2013

NI FAINALI YA WANA MADRID WATUPU KOMBE LA MFALME HISPANIA

Ramidel Falcao akiwajibika uwanjani kuipeleka Atletico Madrid fainali ya Kombe la Mfalme kuvaana na mahasimu wao Real Madrid
MAHASIMU wa jiji la Madrid, nchini Hispania, Real Madrid na Atletico Madrid zitatarajiwa kuumana kwenye pambano la fainali za michuano ya Kombe la Mfalme litakalochezwa Mei 18 mwaka huu.
Atletico Madrid iliifuata Real Madrid kwenye fainali baada ya usiku wa kuamkia leo kulazimisha sare ya mabao 2-2 dhidi ya Sevilla katika mechi ya marudiano ya hatua ya nusu fainali iliyochezwa ugenini.
Mabao ya haraka ya kipindi cha kwanza kutoka kwa nyota wake, Diego Costa na Falcao yalitosha kuivusha Atletico hadi fainali kuwakabili Real iliyoitoa nishai Barcelona juzi usiku kwa kuisasambua mabao 3-1.
WEnyeji walipata bao la kwanza dakika ya 39 lililofungwa na Jesus Navas na kufanya matokeo ya mchezo huo wa jana kusomeka 2-1 wakati wa mapumziko.
Kipindi cha pili wenyeji kilianza kwa kasi na wenyeji walijikuta wakipoteza wachezaji wake wawili kabla ya kusawazisha bao dakika za lala salama na kuepuka aibu ya kulala nyumbani.
Sevilla ilimpoteza Medel dakika ya 76 kabla ya kufuatiwa na Kondogbia aliyeonyeshwa kadi ya pili ya njano dakika moja baada ya kusaidia kupatikana kwa bao la kusawazishwa lililofungwa na Rakitic dakika za nyongeza za pambano hilo.
Mashabiki wa soka wanasubiri kwa hamu pambano hilo la fainali, licha ya Real Madrid inayonolewa na kocha Jose Madrid ikipewa nafasi kubwa ya kujifariji kwa kutwaa taji hilo baada ya kuonekana wazi ni vigumu kutetea taji la Ligi Kuu ya nchi hiyo.

MIMBA YATAJWA CHANZO CHA MAUAJI YA MPENZI WA PISTORIUS

Pistorius akiwa katika moja ya mashindano ya mbio za walemavu alizoshiriki.
Johannesburg, Afrika Kusini
MWANARIADHA wa mbio za walemavu, Oscar Pistorius anayekabiliwa na shitaka la kumuua mpenzi wake kwa risasi, amedaiwa kuwa huenda alimuua mwanamitindo huyo wa zamani akiwa mjamzito.
Kama taarifa hizi zitathibitishwa, itakuwa mfululizo wa madai unaomuweka nyota huyo kwenye hatari ya kufungwa kifungo cha maisha – kwa kumuua mpenziwe Reeva Steenkamp katika nyumba yake katika usiku wa kuamkia Siku ya Wapendanao.
Katika utetezi wake wa awali, Pistorius alidai kumuua Steenkamp kwa bahati mbaya, baada ya kuhisi amevamiwa na jambazi aliyejificha bafuni na kwamba kwa kuwa hakuwa na miguu yake ya bandia, hakuona njia ya kujihami zaidi ya kufyatua risasi mfululizo.
Ni utetezi uliopingwa na waendesha mashtaka wa kesi hiyo – waliodai kuwa tukio limefanyika kwa makusudi baada ya mabishano.
Taarifa zilizochapishwa juzi Jumatatu na gazeti la National Enquirer la hapa zimedai kuwa, huenda mabishano baina ya wawili hao yalitokana na habari kuwa Pistorius alikuwa akikaribia kuitwa baba wa kichanga cha mrembo huyo.
Chanzo cha karibu na uchunguzi kililiambia gazeti la udaku kuwa: 'Polisi inaamini kuwa siri ya ujauzito aliyopewa ilimfanya Pistorius acharuke na kuingia katika mabishano yaliyosababisha kifo cha Reeva – kwa kupigwa risasi nne kichwani, kifuani, mkononi na nyongani.'
Chanzo hicho kiliongeza kuwa: 'Baadaye usiku, majirani walisikia mabishano yaliyofuatiwa na ufyatuaji risasi katika nyumba yao.
'Polisi waliitwa kwa uchunguzi, lakini walijiridhisha tu kuwa ulikuwa ubishani wa kimapenzi, hivyo hawakuwa na uchunguzi wa maana waliotarajiwa wangeulizwa kuhusiana na sakata hilo.'
Likiambatanisha na picha iliyopigwa siku chache kabla ya kifo cha Reeva, gazeti hilo limeripoti wasiwasi huo, sambamba na habari kuhusu ibada maalum ya kumuombea marehemu aliyoandaa Pistorius nyumbani kwa mjomba wake anakoishi kwa hivi sasa.

Toto Afrika, JKT Ruvu zikishuka dimbani, Ligi yazidi kunoga

Kikosi cha JKT Ruvu

WAKATI vijana wa Toto African leo wakijaribu bahati yao mbele ya wenyeji wa JKT Ruvu katika mechi ya kiporo ya Ligi Kuu Tanzania Bara, matokeo ya mechi za jana za ligi hiyo zimevuruga msimamo kwa baadhi ya timu nyingine zikinufaika na nyingine zikiporomoka katika nafasi walizokuwa wakizishikilia.
Kipigo cha bao 1-0 ilichopewa Kagera Sugar kimeishusha timu hiyo kutokana nafasi ya tano iliyokuwa ikishikilia hadi nafasi ya sita ikiwapisha ndugu zao Mtibwa Sugar walioambulia suluhu nyumbani kwao Manungu dhidi ya Prisons-Mbeya.
Timu hizo mbili zote zinalingana pointi 28, lakini Mtibwa imeiengua Kagera kwa vile ina uwiano mzuri wa mabao ya kufunga na kufungwa, ambapo hazina yake inaonyesha imefunga mabao 21 na kiufungwa 18 wakati ndugu zao wamefunga mabao 19 na kufungwa 17.
Pia ushindi wa Polisi Moro umeifanya timu hiyo kuchupa toka mkiani hadi kwenye nafasi ya 12 ikifikisha pointi 15 na kuirejesha African Lyon kuburuza mkia na pointi zake 13, wakifuatiwa na Toto African ambao jioni ya leo watacheza wakiwa na pointi 15 na iwapo iutashinda itachupa hadi nafasi ya 11 inayoshikiliwa na  wapinzani wa JKT Ruvu.
Kwa mujibu wa ratiba ni kwamba ligi hiyo itaendelea tena Jumatano ijayo kwa mechi tatu, 'vibonde' African Lyon kuikaribisha Ruvu Shooting kwenye uwanja wa Chamazi, Mgambo JKT kuialika Mtibwa Sugga kwenye dimba la Mkwakwani Tanga na JKT Oljoro wakaikaribisha Prisons ya Mbeya.
Siku inayofuata kutakuwa na pambano moja tu kati ya JKT Ruvu dhidi ya Kagera Sugar katika uwanja wa Chamazi na mwishoni mwa wiki kushuhudiwa mechi tatu zitakazozihusisha timu zilizopo nafasi nne za juu.
Jumamosi Machi 9, vinara Yanga itawakaribisha ndugu zao Toto African kwenye uwanja wa Taifa, wakati Azam itakayokuwa imerejea toka Sudan Kusini kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho itaialika Polisi Moro kabla ya siku inayoifuata yaani Jumapili 'ndugu' wengine, Simba na Coastal Union kuumana Taifa.

MSIMAMO WA LIGI KUU BARA
                        P W  D  L  GF GA GD Pts
1. Yanga 18 13 3 2 35   12 23 42

2. Azam 18  11 3 4  31   15  16   36

3. Simba SC 18 8 7 3  26   15   11 31

4. Coastal Union 19  8  4  21 16 5 31

5.
Mtibwa Sugar 19  7  5  21  18    3    28
6. Kagera Sugar 19 7  7 5  19  17      28
7. Ruvu Shooting 17  7 5 5  20 17     3 25
8. Mgambo JKT 19 7 3 9 14  18 -4   24

9. JKT Oljoro 18  5   6  7  19  22   -3 21

10.Tanzania 19  4   8 7  11  16   -5    20

11.JKT Ruvu  17  4 4 9 14  27 -13 16

12. Polisi Moro 18  3 6   9   9   18  -9   15

13.Toto African 18 2 8  8   14 25 -11  14
14.African Lyon 19 3 4 12 13  31 -18 13