STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, February 28, 2013

MIMBA YATAJWA CHANZO CHA MAUAJI YA MPENZI WA PISTORIUS

Pistorius akiwa katika moja ya mashindano ya mbio za walemavu alizoshiriki.
Johannesburg, Afrika Kusini
MWANARIADHA wa mbio za walemavu, Oscar Pistorius anayekabiliwa na shitaka la kumuua mpenzi wake kwa risasi, amedaiwa kuwa huenda alimuua mwanamitindo huyo wa zamani akiwa mjamzito.
Kama taarifa hizi zitathibitishwa, itakuwa mfululizo wa madai unaomuweka nyota huyo kwenye hatari ya kufungwa kifungo cha maisha – kwa kumuua mpenziwe Reeva Steenkamp katika nyumba yake katika usiku wa kuamkia Siku ya Wapendanao.
Katika utetezi wake wa awali, Pistorius alidai kumuua Steenkamp kwa bahati mbaya, baada ya kuhisi amevamiwa na jambazi aliyejificha bafuni na kwamba kwa kuwa hakuwa na miguu yake ya bandia, hakuona njia ya kujihami zaidi ya kufyatua risasi mfululizo.
Ni utetezi uliopingwa na waendesha mashtaka wa kesi hiyo – waliodai kuwa tukio limefanyika kwa makusudi baada ya mabishano.
Taarifa zilizochapishwa juzi Jumatatu na gazeti la National Enquirer la hapa zimedai kuwa, huenda mabishano baina ya wawili hao yalitokana na habari kuwa Pistorius alikuwa akikaribia kuitwa baba wa kichanga cha mrembo huyo.
Chanzo cha karibu na uchunguzi kililiambia gazeti la udaku kuwa: 'Polisi inaamini kuwa siri ya ujauzito aliyopewa ilimfanya Pistorius acharuke na kuingia katika mabishano yaliyosababisha kifo cha Reeva – kwa kupigwa risasi nne kichwani, kifuani, mkononi na nyongani.'
Chanzo hicho kiliongeza kuwa: 'Baadaye usiku, majirani walisikia mabishano yaliyofuatiwa na ufyatuaji risasi katika nyumba yao.
'Polisi waliitwa kwa uchunguzi, lakini walijiridhisha tu kuwa ulikuwa ubishani wa kimapenzi, hivyo hawakuwa na uchunguzi wa maana waliotarajiwa wangeulizwa kuhusiana na sakata hilo.'
Likiambatanisha na picha iliyopigwa siku chache kabla ya kifo cha Reeva, gazeti hilo limeripoti wasiwasi huo, sambamba na habari kuhusu ibada maalum ya kumuombea marehemu aliyoandaa Pistorius nyumbani kwa mjomba wake anakoishi kwa hivi sasa.

No comments:

Post a Comment