STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, February 28, 2013

NI FAINALI YA WANA MADRID WATUPU KOMBE LA MFALME HISPANIA

Ramidel Falcao akiwajibika uwanjani kuipeleka Atletico Madrid fainali ya Kombe la Mfalme kuvaana na mahasimu wao Real Madrid
MAHASIMU wa jiji la Madrid, nchini Hispania, Real Madrid na Atletico Madrid zitatarajiwa kuumana kwenye pambano la fainali za michuano ya Kombe la Mfalme litakalochezwa Mei 18 mwaka huu.
Atletico Madrid iliifuata Real Madrid kwenye fainali baada ya usiku wa kuamkia leo kulazimisha sare ya mabao 2-2 dhidi ya Sevilla katika mechi ya marudiano ya hatua ya nusu fainali iliyochezwa ugenini.
Mabao ya haraka ya kipindi cha kwanza kutoka kwa nyota wake, Diego Costa na Falcao yalitosha kuivusha Atletico hadi fainali kuwakabili Real iliyoitoa nishai Barcelona juzi usiku kwa kuisasambua mabao 3-1.
WEnyeji walipata bao la kwanza dakika ya 39 lililofungwa na Jesus Navas na kufanya matokeo ya mchezo huo wa jana kusomeka 2-1 wakati wa mapumziko.
Kipindi cha pili wenyeji kilianza kwa kasi na wenyeji walijikuta wakipoteza wachezaji wake wawili kabla ya kusawazisha bao dakika za lala salama na kuepuka aibu ya kulala nyumbani.
Sevilla ilimpoteza Medel dakika ya 76 kabla ya kufuatiwa na Kondogbia aliyeonyeshwa kadi ya pili ya njano dakika moja baada ya kusaidia kupatikana kwa bao la kusawazishwa lililofungwa na Rakitic dakika za nyongeza za pambano hilo.
Mashabiki wa soka wanasubiri kwa hamu pambano hilo la fainali, licha ya Real Madrid inayonolewa na kocha Jose Madrid ikipewa nafasi kubwa ya kujifariji kwa kutwaa taji hilo baada ya kuonekana wazi ni vigumu kutetea taji la Ligi Kuu ya nchi hiyo.

No comments:

Post a Comment