STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, December 19, 2014

FIFA yakubali kuchapisha taarifa ya rushwa hadharani

http://www.playlouisianasoccer.org/assets/946/15/FIFA%20Logo.jpg 
MAOFISA wakuu wa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA wamekubaliana kutoa ripoti yote kuhusu uchunguzi wa madai ya ufisadi uliotokea wakati wa kutolewa kwa uenyeji wa michuano ya Kombe la Dunia Urusi mwaka 2018 na Qatar mwaka 2022.
Maofisa hao wamekubali kutoa kurasa 430 za uchunguzi wa Michael Garcia baada ya kufanya mkutano kufuatia pendekezo la rais wa FIFA Sepp Blatter.
Hatua hiyo ya kuichapisha ripoti hiyo inaonyesha mabadiliko ya sera baada ya FIFA kukataa shinikizo kutoka kwa Garcia mwenyewe na wengine kutoa ripoti hiyo. 
Garcia alijiuzulu siku ya Jumatano baada ya ombi lake la kupinga ripoti fupi ya uchunguzi wake iliotolewa na mwenyekiti wa kamati ya maadili katika shirikisho hilo Hans-Joachim Eckert kukataliwa.

No comments:

Post a Comment