STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, December 19, 2014

Neymar amwagiwa sifa lukuki na Carlos

http://img.crunchsports.com/crunchsports/NewsImages/160422581.jpg
Neymar
http://img01.mundodeportivo.com/2013/03/08/Roberto-Carlos-Neymar-tiene-un_54368194317_54115221213_490_300.jpg
Roberto Carlos (kushoto) akifurahia jambo na Neymar (kati) na Ronaldo de Lima
MSHAMBULIAJI nyota wa Brazil anayekipiga Barcelona, Neymar amemwagiwa sifa akidai kuwa kiwango chake kinachuana na nyota wengine wa dunia, Lionel Messi na Cristiano Ronaldo.
Beki wa zamani wa kimataifa wa Brazil, Roberto Carlos ndiye aliyemmwagia misifa nahodha huyo wa sasa wa Brazil akisisitiza kuwa sasa anashindana na Lionel Messi na Ronaldo akiwa kama mchezaji bora duniani. Neymar,22 alipewa unahodha wa timu ya taifa ya Brazil na kocha mpya Dunga ambapo tayari ameshaingoza timu hiyo kushinda mechi sita mfululizo toka baada ya Kombe la Dunia huku akifunga mabao saba. 
Neymar alikuwa mchezaji pekee wa Brazil kuwepo katika orodha ya wachezaji 23 waliotajwa kugombea tuzo ya Ballon d’Or na Carlos anaamini mshambuliaji huyo wa Barcelona ni mchezaji bora wa tatu kumuona msimu huu. 
Carlos amesema Neymar ni mchezaji wa aina yake kwani amezoea soka la Ulaya haraka tatizo kubwa ni kwamba Messi na Ronaldo wanaimarika kila siku hivyo kila Neymar akijaribu kuwakaribia wanamuacha tena.

No comments:

Post a Comment