STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, December 19, 2014

Breaking News! Ikulu yakana Rais Kikwete kulihutubia taifa leo

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiPAd2mufOSWsRJT4w_lKEdDQCc1IMqTtswgJ123OH67pmpaEbvH90ACdbz_jNqCAh11YC_eof9AM6zPZoZgsExCqU_ZVKJgruZgtjgQH4OmVApzg_PkjzbOI4bNY_a3RfrKVq4BwgdyKE/s1600/RAIS+KIKWETE+1.JPG
Rais Jakaya Kikwete atakayelihutubia taifa siku ya Jumatatu na siyo leo kama ilivyodokezwa awali na vyombo vya habari
WAKATI masikio ya watanzania yakiwa yamejiandaa kumsikiliza Rais Jakaya Kikwete baada ya kuwepo kwa taarifa kwamba huenda angelihutubia taifa leo na kufichua mambo mbalimbali yaliyolighubika taifa, Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu imekanusha taarifa hizo.
Kwa mujibu wa taarifa ambazo MICHARAZO imezipata muda mfupi uliopita zinasema kuwa kilichokuwa kimeandikwa kwenye  mitandao ya kijamii na katika gazetini kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dk. Jakaya Mrisho Kikwete siyo kweli.
Kurugenzi hiyo ya Mawasiliano imesema kuwa ukweli wa taarifa ni kwamba Rais atalihutubia taifa siku ya Jumatatu, Desemba 22 mwaka huu muda utakaopangwa.
Watanzania wana hamu kubwa ya kusikia kauli ya Rais kutokana na Sakata la Akaunti ya Tegeta Escrow pamoja na vurugu zilizofanywa katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Vijiji na Vitongoji uliofanyika Jumapili na kushuhudia madudu yaliyosababisha wakurugenzi 17 wa Halmashauri na miji kukubwa na 'rungu' toka kwa Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Hawa Ghasia.

No comments:

Post a Comment