STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, May 11, 2013

Polisi wakanusha kulipuliwa kwa Kanisa Dar

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgmZailT3xrp_mk4Dl2u_YjPQh8mEPXYeZtf7E1E66J078Snu1TzABUaqlPeG2dze1Hb2Y_9wvsUOiVOLCV-VcAFOuJvfj2AX9O2UBubmDtdX5BbQdyH1LPgYLQqeDEJjamzISAmcb7TXeP/s1600/_MG_0506.jpg
Kamanda Kova (kati) na Kenyela (kulia) wakiwa na IGP Said Mwema katika moja ya shughuli za kitaifa

JESHI la Polisi Mkoa wa Kinondoni, umekanusha taarifa zilizosambazwa kwenye baadhi ya mitaandao ya kijamii na mtaani kwamba Kanisa la KKKT Kunduchi limelipuliwa mabomu kama ilivyotokea kwa Kanisa la Katoliki la Arusha.


Kamanda wa Polisi mkoa huo, Charles Kenyela alisema taarifa zilizoenea kwamba bomu limelipuka katika Kanisa la Kilutheri la Kiinjili Tanzania (KKKT), Kunduchi jijini Dar es Salaam zimeenea ndivyo sivyo ukweli ni kwamba askari walikuwa wanapambana na majambazi karibu na kanisa hilo.
 

Afande Kenyela alisema kwamba taarifa hizo sio za kweli na kwamba askari wa jeshi la polisi walikuwa wanapambana na majambazi karibu na eneo la kanisa hilo.

Alidai walipata taarifa za kundi la watu hao wanaosadikiwa kuwa majambazi ambao walijificha kwenye jengo ambalo ni la ghorofa na ndipo katika kuwalazimisha watokea askari wao waliamua kuwatupia bomu la machozi ambalo ndilo lililowatisha watu na kusambaza taarifa zisizo za kweli.


"Wakati askari wetu wanapambana na majambazi hayo- waumini wa kanisa hilo wamejitokeza kuwasaidia askari wetu. Naomba unisaidie kukanusha siyo kweli, nitazungumza na vyombo vingine vya habari kuweka sawa," amesema Kamanda Kenyela hivi punde alipokuwa akihojia na kituio cha redio cha Clouds FM.

Ufafanuzi kama huo pia umetolewa na Kamanda wa Polisi Kanda Maalum, Suleiman Kova, aliyesema hajui uvumi huo umetolewa kwa lengo gani, wakati taifa bado likiwa katika 'vuguvugu' la tukio lililoacha majonzi la Arusha ambapo watu wasiojulikana walilipua bomu lililosababisha vifo vya watu wanne mpaka sasa na wengine kujeruhiwa baadhi vibaya ambapo wanaendelea na matibabu.


Kamanda Kova alisema ni vyema wanaosambaza taarifa hizo wajiridhishe na ushahidi ili kutowatia hofu watu wengine walio, kama alivyosema Kenyela kwamba japo leo haikuwa siku ya ibada lakini katika kanisa hilo la KKKT lililopo salama wa salimu walikuwepo baadhi ya watumishi waliotoa msaada kwao na kufanikiwa kuwanasa watuhumiwa wanne wakiwemo wanafunzi wawili wenye umri kati ya miaka 13 na 16 waliokuwa kundi moja na wahalifu hao waliodaiwa walikuwa wakipanga mipango ya uhalifu.

Lampard aiweka pazuri Chelsea EPL

Frank Lampard: Chelsea's history man.
Frank Lampard akishangili moja ya mabao yake yanayomfanya azidi kuimarisha rekodi yake ya mabao 'Darajani'

MAGOLI mawili kupitia kwa kiungo mzoefu, Frank Lampard yameiweka pazuri Chelsea katika kujihakikishia kuwepo kwenye Top $ ya kushiriki  moja kwa moja Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya jioni hii kuitambia Aston Villa nyumbani kwa mabao 2-1.
Chelsea kwa ushindi huo uliotokana na mabao ya dakika ya 61 na 88 ya kiungo huyo mkongwe ambaye kadri siku zikizidi kuyoyoma anazidi kuonyesha umuhimu wake 'Darajani' yameifanya waliokuwa mabingwa hao wa Ulaya kufikisha pointi 72, akisaliwa na mechi moja.
Arsenal ambayo itashuka dimbani Jumanne kupepetana na 'vibonde' Wigan Athletic ndiyo pekee inayoweza kuzivuka pointi ilizonazo Chelsea na kuweza kuitoa kwenye tatu bora, lakini uhakika wa 4 Bora imeshaupata kwa ushindi huo wa leo.
Katika pambano la leo Chalsea walishtuliwa na bao la robo ya kwanza ya kipindi cha kwanza kupitia Christian Benteke bao lilodumu hadi mapumziko ambapo wageni walijikuta wakimaliza pungufu baada ya Ramires kupewa kadi ya pili ya njano na kusindikizwa na nyekundu na mwamuzi Lee Stephen Mason.Hata hivyo wenyeji nao walijikuta wakimpoteza mchezaji wao muhimu Benteke kwa kulimwa kadi ya pili ya njano kama ilivyokuwa kwa Ramires na kutolewa nje kwa kadi nyekundu na kutoa mwanya kwa wageni kufunga bao la kusawazisha kabla ya kuwazima dakika za lala salama na kuwaacha na pointi zao 40 wakiendelea kupumua katika janga na kushuka daraja kama haitashinda mechi ya mwisho na waliopo nyuma yake kushinda michezo yao kesho na siku ya Mei 19.
Mabao hayo mawili yamemfanya Lampard kufikisha jumla ya mabao 203 mpaka sasa katika michuano yote kati ya mechi 606.

Friends Rangers yapeta RCL, kivumbi kuanza ligi hiyo kuanza kesho

 
Mmoja wa wachezaji wa Friends Rangers (mwenye mpira) akichakarika uwanjani kabla timu yao haijafuzu ligi ya mabingwa wa mkoa (RCL) ambapo pia imepeta hadiu raundi ya pili
Na Boniface Wambura
Wakati Ligi ya Mabingwa wa Mikoa (RCL) inaanza kutimua vumbi keshokutwa (Mei 12 mwaka huu), timu mbili zinakwenda moja kwa moja raundi inayofuata baada ya mabingwa wa Pwani, Kiluvya United kuondolewa na mkoa wa Manyara kutowasilisha bingwa wake.

Kamati ya Mashindano ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) iliyokutana leo (Mei 10 mwaka huu) imeiondoa Kiluvya United baada ya kubaini kuwa timu hiyo haikushiriki ligi ya mkoa wala wilaya msimu uliopita, hivyo kutokuwa na sifa ya kucheza Ligi ya Mkoa msimu huu.

Hivyo Friends Rangers ya Dar es Salaam iliyokuwa icheze na Kiluvya United na Mpwapwa Stars ya Dodoma iliyokuwa iwakabili mabingwa wa Manyara zinakwenda moja kwa moja raundi ya pili.

Timu nyingine iliyokwenda moja kwa moja raundi ya pili itakayochezwa kati ya Mei 25 na 25 mwaka huu na mechi za marudiano ni kati ya Juni 1 na 2 mwaka huu baada ya kupita kwenye upangaji ratiba ni mabingwa wa Shinyanga, Stand United FC.

Kamati hiyo iliyokutana chini ya uenyekiti wa Blassy Kiondo pia imeagiza viongozi wa mikoa ya Manyara na Pwani waandikiwe barua za onyo kwa kushindwa kuwasilisha majina ya mabingwa wao.

Vilevile imesisitiza viwanja vitakavyotumika kwa mechi za RCL ni vya makao makuu ya mikoa tu, isipokuwa kwa Uwanja wa CCM Mkamba ulioko Ifakara, Morogoro ambao ulishakaguliwa na TFF, hivyo kutumika kwa michuano ya Ligi Daraja la Kwanza (FDL) msimu huu. Pia usajili unaotumika katika RCL ni ule ule wa ligi ya mkoa.

Mechi za Mei 12 mwaka huu zitakuwa kati ya Kariakoo ya Lindi dhidi ya Coast United ya Mtwara (Uwanja wa Ilulu), Techfort ya Morogoro vs African Sports ya Tanga (Uwanja wa CCM Mkamba), Machava FC ya Moshi vs Flamingo SC ya Arusha (Uwanja wa Ushirika), Simiyu United ya Simiyu vs Magic Pressure ya Singida (Uwanja wa Simiyu) na Polisi Jamii Bunda ya Mara vs UDC ya Mwanza (Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume).

Polisi SC ya Geita vs Biharamulo FC ya Kagera (Uwanja wa Geita), Saigon FC ya Kigoma vs Milambo FC ya Tabora (Uwanja wa Lake Tanganyika), Katavi Warriors ya Katavi vs Rukwa United ya Rukwa (Uwanja wa Katavi), Njombe Mji ya Njombe vs Mbinga United ya Ruvuma (Uwanja wa Sabasaba) na Kimondo SC ya Mbeya dhidi ya 841 KJ FC ya Iringa (Uwanja wa Sokoine, Mbeya).

Mechi kati ya Red Coast na Abajalo itachezwa Mei 13 mwaka huu Uwanja wa Azam ulioko Chamazi, Dar es Salaam. Mei 12 mwaka huu uwanja huo utatumika kwa mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kati ya Azam na Mgambo Shooting.
ZA LEO LEO