![]() |
| Gareth Bale alihama Spurs masimu uliopita |
WINGA machachari wa Real Madrid, Gareth Bale amezungumzia dokezo la kurejea Tottenham hapo baadaye.
Nyota
huyo aliondoka White Hart Lane msimu uliopita kwa rekodi
ya dunia ya uhamisho na ameendelea kuimarisha kiwango chake nchini
Hispania.
Lakini
licha ya kuonekana ametulia ndani ya kikosi akiwa sambamba na Cristiano
Ronaldo ndani ya Bernabeu, Bale amesema bado anaipenda Tottenham.
"Tottenham
siku zote itaendelea kuwepo ndani ya moyo wangu. Natumaini mashabiki
bado wananipenda inagawa nimeondoka," alisema wakati akiongea na BT Sport.
"Nawapenda mashabiki wa Spurs. Huwezi jua ninaweza kurejea siku moja".

SHIRIKISHO
la Soka Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko makubwa taarifa
zilizoandikwa kwenye baadhi ya Vyombo vya Habari zikielezea tuhuma za
hujuma kwa timu ya Taifa (Taifa Stars) katika mechi za kufuzu mashindano
ya AFCON.



SHIRIKISHO
la Soka Ulaya, UEFA limethibitisha kuwa Uwanja wa Wembley uliopo
jijini London Uingereza ndiyo utakaotumika kwa mchezo wa nusu
fainali na fainali ya michuano ya Ulaya 2020.
IMETHIBITIKA kuwa, beki wa kulia wa Arsenal, Mathieu Debuchy atakuwa nje ya dimba kwa muda wa wiki sita hali inayozidi kuiweka pabaya klabu hiyo.