STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, September 19, 2014

Kivumbi England, Arsenal kesho, Man City, Chelse J'pili

http://img.eplmatches.com/2014/06/premier-league.jpg
KIVUMBI cha Ligi Kuu ya England kinatarajiwa kuendelea tena kesho wakati Arsenal watakapokuwa ugenini kuvaana na wenyeji wao Aston Villa, huku kazi nzima ikiwa Jumapili.
Arsenal iliyotoka kukong'otwa mabao 2-0 na Borussia Dortmund katika Ligi ya Mabingwa Ulaya watawafuata Villa ambayo haijapoteza mchezo wowote mpaka sasa ikiwa nafasi ya pili katika msimamo nyuma ya Chelsea wanaoongoza wakiwa na pointi 12, Villa ikiwa na 10.
Arsenal inayokamata nafasi ya saba itahitaji ushindi ili kurejea kwenye mbio zao za kutaka kutwaa ubingwa licha ya kukabiliwa na majeruhi katika kikosi chao.
Mechi nyingine za kesho Jumamosi zitakuwa ni kati ya vibonde QPR waliozabuliwa mabao 4-0 wiki iliyopita na Manchester United itakapokuwa nyumbani kuialika Stoke City, huku Liverpool itaifuata West Ham ikiwa inaugua kipigo ilichopewa wiki iliyopita na Aston Villa.
Ratiba kamili ya kesho ni;
14:45 QPR v Stoke  
17:00 Aston Villa v Arsenal
17:00 Burnley v Sunderland
17:00 Newcastle v Hull
17:00 Swansea v Southampton
19:30 West Ham v Liverpool
Jumapili  
15:30 Leicester v Man United  
15:30 Tottenham v West Brom
18:00 Everton v Crystal Palace
18:00 Man City v Chelsea
Ratiba nyingine ya ligi hiyo;
Jumamosi Septemba 27  
14:45 Liverpool v Everton
17:00 Chelsea v Aston Villa
17:00 Crystal Palace v Leicester
17:00 Hull v Man City
17:00 Man United v West Ham
17:00 Southampton v QPR
17:00 Sunderland v Swansea
19:30 Arsenal v Tottenham
Jumapili Septemba 28
18:00 West Brom v Burnley
Jumatatu Septemba 29  
22:00 Stoke v Newcastle

No comments:

Post a Comment