STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, September 19, 2014

Hujuma mechi ya Stars, Mambas kuchunguzwa

http://shaffihdauda.com/wp-content/uploads/2014/07/10s.jpgSHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko makubwa taarifa zilizoandikwa kwenye baadhi ya Vyombo vya Habari zikielezea tuhuma za hujuma kwa timu ya Taifa (Taifa Stars) katika mechi za kufuzu mashindano ya AFCON. TFF pamoja na kutokuwa na uthibitisho wa tuhuma hizi nzito haliwezi kuzikalia kimya. TFF itateua jopo la kuchunguza tuhuma hizi. Wanafamilia wa mpira wa miguu Tanzania (Members of TFF Family) watakaohitajika kuhojiwa na jopo hilo kwa mujibu wa Ibara ya 37 ya Kanuni za Maadili za TFF watalazimika kutoa ushirikiano. 
Atakayeshindwa kutoa ushirikiano atachukuliwa hatua za kimaadili. 
Pia wadau wa mpira wa miguu ambao sio wanafamilia wa TFF, watakaoitwa na jopo hili wanaombwa watoe ushirikiano kwa nia ya kujenga mpira wetu.

No comments:

Post a Comment