STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, September 19, 2014

Gareth Bale bado aiwaza Spurs, ahidi kurejea

Gareth Bale alihama Spurs masimu uliopita
http://www.guinnessworldrecords.com/media/6352324/Gareth-Bale-main.jpgWINGA machachari wa Real Madrid, Gareth Bale amezungumzia dokezo la kurejea Tottenham hapo baadaye.
Nyota huyo aliondoka White Hart Lane msimu uliopita kwa rekodi ya dunia ya uhamisho na ameendelea kuimarisha kiwango chake nchini Hispania.
Lakini licha ya kuonekana ametulia ndani ya kikosi akiwa sambamba na Cristiano Ronaldo ndani ya Bernabeu, Bale amesema bado anaipenda Tottenham.
"Tottenham siku zote itaendelea kuwepo ndani ya moyo wangu. Natumaini mashabiki bado wananipenda inagawa nimeondoka," alisema wakati akiongea na BT Sport.
"Nawapenda mashabiki wa Spurs. Huwezi jua ninaweza kurejea siku moja".

No comments:

Post a Comment