STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, July 9, 2013

Spika Makinda avionya vyombo vya habari

Spika Anna Makinda
 Na Suleiman Msuya
SPIKA wa Bunge la Jamhuri ya Muungano Anna Makinda ametoa rai kwa wanahabari na vyombo vya habari nchini kuacha kutumika kwani watakuwa wakwanza kulaumiwa iwapo nchi itaingia katika machafuko.
Makinda aliyasema hayo wakati akizungumza na wanahabari katika makaribisho ya Spika wa Korea Kusini Kang Chang Hee na ujumbe wake ambao wapo hapa nchini kwa mwaliko wa Bunge la Tanzania.
Alisema wapo wanahabari ambao wanakubali kutumiwa vibaya na wanasiasa wakiamini uandishi ndivyo unataka jambo ambalo amelikemea kwa nguvu zote.
Spika alisema ni vema vyombo vya habari na wanahabari kutumia nafasi yao kukosa Bunge na Serikali pale vinapoenda kinyume na maadili na kushindwa kutumikia wananchi ambao ndio waajiri wao wakubwa.
“Napenda kutumia nafasi hii kuwaomba wanahabari na vyombo vyenu kukataa kutumiwa na wanasiasa pamoja na ukweli kuwa wapo ambao wanauhusiano  na vyama mbalimbali ,” alisema.
Aliwataka kwa wale wanahabari wenye kuhitaji kushiriki siasa ni vyema wajiweke wazi kwani haipo sababu ya kuwa vibaraka wakati fursa ya wao kushiriki ipo wazi.
Aidha alivitaka vyama vya siasa kufanya siasa za haki na kuacha kutumbukiza chuki kwa wananchi kwa kile wanachoamini kuwa ndio njia ya kufikia malengo yao ya kisiasa.
Makinda alisema iwapo vyama vya siasa nchini vitadumisha siasa za ukweli ni dhahiri kuwa wananchi watakuwa na maamuzi sahihi bila kusukumwa na mtu yoyote.
Pia aliwataka wanasiasa kuacha kumchafua kwa kile ambacho wanasema kuwa amekuwa akipendelea hasa kwa wabunge wa chama chake jambo ambalo halina ukweli wowote.

TIC yafichua muarobaini wa tatizo la ajira nchini

Meneja Uhusiano wa TIC, Pendo Gongwe (Kati) akisisitiza jambo
Na Suleiman Msuya
ZAIDI ya ajira 174,412 zinatarajiwa kuzalishwa iwapo miradi 869 iliyosajiliwa Kituo cha Taifa cha Uwekezaji (TIC) itakamilika kwa wakati ulipangwa.
Hayo yamebainishwa na Meneja Mahusiano wa TIC Pendo Gondwe wakati akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam.
Alisema katika kipindi cha Januari hadi Desemba 2012 TIC ilifanikiwa kusajili miradi 869 ambayo imegawanyika katika sekta mbalimbali ambayo inathamani ya dola za kimarekani shilingi milioni 11,420.
Gondwe alisema katika miradi hiyo 869 miradi 469 ni ya wazawa ambayo ni asilimi 54 na iliyobakia ni wawekezaji kutoka nje miradi 205 sawa na asilimia 23.5 na miradi ya ubia kati ya wageni na watanzania ni 195 sawa na asilimia 22.5  jambo ambalo ni la kujisifia kwa nchi.
Meneja huyo alisema sekta tano zimeongoza katika kuwekezwa ambazo ni sekta ya utalii miradi 144, usafirishaji 92, uzalishaji viwandani 86, majengo ya biashara 78 na kilimo miradi 28.
“ Ndugu zangu wanahabari napenda kutumia nafasi hii kuwataarifu kuwa miradi ya uwekezaji imeongezeka kwa ksi kubwa jambo ambalo tunaona na mwendelezo mzuri katika kukuza uchumi na ishara tosha ya kuonyesha kuwa nchi yetu ina usalama kwani hadi kufikia mwezi desemba mwaka jana miradi 869 imesajiliwa,” alisema.
Gondwe alisema jitihada za TIC ni kuhakikisha kuwa faida za uwekezaji katika uchumi wa Tanzania ikiwa ni kuweka mazingira rahisi kwa wawekezaji kuwa wanapata vibali vyote vinavyohitajika chini ya mfumo wa One Stop Shop.
Aidha alibainisha kuwa nchi kumi ambazo zinaongoza kwa uwekezaji hapo nchini kuwa ni Uingereza, China, India, Kenya Marekani, Uholanzi, Afrika Kusini, Canada, Ujerumani na Italia.
Naye Meneja Huduma kwa Wawekezaji Revocatus Arbogats alisema pamoja na ukweli kuwa miradi hiyo imesajiliwa lakini bado haijaanza kutoa matunda ya ajira kwani bado wawekezaji wako kwenye mchakato wa utekelezaji.
Alisema miradi hiyo itaanza kuonyesha matunda baada ya miaka mitatu ambapo watanzania wa kada mbalimbali wataanza kufaidika na ajira ambazo zitahusu uwekezaji husika.
Kuhusu wawekezaji kupendelea kuwekeza maeneo ambayo tayari wananchi wanaishi alisema kuwa hali hiyo inatokea mara chache baada ya mwekezaji kuonyesha kuwa eneo hilo linahusika na mradi.
Arbogats alisema pamoja na changamoto hizo TIC imekuwa ikijitahidi kutatua kwa kuhakikisha kuwa kila pande inaridhika na hatua ambazo zinachukuliwa.
Akizungumzia kuhusu sekta ya kilimo kuwa na wawekezaji wachache katika takwimu ambazo zimeanishwa Kaimu Meneja Utafiti wa TIC Nyoki Tibenda alisema sekta hiyo ni sekta muhimu ambayo inahitaji mitaji mikubwa bila kutarajia faida ya haraka.
Tibenda alisema TIC inaendelea kuwavutia wawekezaji ambao wapo tayari kuwekeza katika sekta hiyo ambapo alimtolea mfano mwekezaji aliyewekeza mkoani Morogoro Kilombero katika kilimo cha mpungu kuwa ameonyesha mafanikio makubwa.

Maaskofu wawacharukia wanasiasa wanaotumia vibaya makanisa, msikiti

Askofu Mwamalanga
Na Suleiman Msuya
IKIWA ni siku chache baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Jakaya Kikwete kuwataka viongozi na wanachama wa kisiasa kuacha kutumia nyumba za ibada kusakamana na kukashfiana viongozi wa dini wamemtaka kutumia nafasi yake kwa kuwataja wahusika kwani wanachochea uvunjifu wa amani.
Hayo yamebainishwa na Askofu  William Mwamalanga wa Kanisa la Kiinjili la Kipentakosti Tanzania pamoja na Mchungaji wa Kanisa la AGAPE Tanzania Onesmo Mwakyambo wakati wakizungumza na mwandishi wa habari hii.
Alisema ujumbe wa Rais ni muhimu hasa ukizingatia katika kipindi hiki ambacho kumejitokeza watu ambao wanaonekana kutumia nyumba za ibada kutoa misaada ambayo kwa upande mwingine kunatia shaka jamii ya Wanzania.
Mwamalanga alisema haipo sababu ya Rais kumumunya maneno kwani ni ukweli kuwa wahusika wakubwa wa mtindo huo wanatoka katika Chama Cha Mapinduzi (CCM) hivyo ni vema wakakutana ili kukemea kichama zaidi.
“Mimi na baadhi ya viongozi wa dini na wananchi tunaamini kuwa Rais Kikwete amefanya jambo muhimu zaid katika kutatua hali ilivyo sasa kisiasa ila ni vema akaenda mbali zaidi kwa kuwaita hao wahusika na kuwakemea kichama kwani ni wanachama wa chama chake,” alisema
Askofu huyo alisema suala la baadhi ya viongozi wa kisiasa kutumia nyumba za ibada kwa kutoa misaada sio baya iwapo misaada hiyo ni safi ila akawataka kutambua kuwa ni vyema wakatubu iwapo wanatumia nafasi hiyo kujisafisha.
Mwamalanga alisema ni wazi kuwa Taifa linaweza kuingia katika hali sio sahihi iwapo haki za wananchi zitavunjwa kwani ni vigumu amani kuwepo katika eneo haki zinavunjwa.
Alisema watu baadhi wamefanikiwa kupoka haki za wananchi nje ya kanisa hali ambayo inaonyesha kuwa wanajipanga kuingia kuichukia haki iliyopo kanisani jambo ambalo amewataka viongozi wa kidini kupinga kwa nguvu zote.
Pia Askofu Mwamalanga alitoa wito kwa baadhi ya watu ambao wamekuwa wakiibuka na kujiita manabii kuwa waache kwani kufanya hivyo ni kinyume cha dini ya Kikristo.
Alisema kumekuwepo na uibukaji wa manabii wa uongo hasa katika mkoa wa Dar es Salaam jambo ambalo halipo katika maandiko na kuwataka viongozi wa dini kukemea hali hiyo kwani ni uzalilishaji wa dini.
Kwa upande wake Mchngaji Onesmo Mwakyambo ni vyema Serikali ikahakikisha kuwa amani inadumu kwani jamii ya Tanzania inatambua umuhimu wa kuwepo kwa amani ila kitendo cha viongozi kuwa sababu serikali itawajibika.
Alisema iwapo serikali itaangalia amani ikitoweka itambua kuwa athari zake ni kubwa kwani kwa muda mrefu jamii ya kitanzania imekuwa katika amani na upendo kama msingi wa maisha yao ya kila siku.
Mwakyambo alisema serikali inawajibika kuweka wazi mamabo yote ambayo yanalalamikiwa na wananchi kama moja ya njia ya kutatua matatizo hayo.
Aliwataka viongozi wa kidini kuacha kutumiwa kwani kufanya hivyo ni kukosea mungu jambo ambalo ni kinyume na mafundisho ya dini zao.

TUNAWATAKIA RAMADHANI KAREEM




http://thumbp4-ne1.thumb.mail.yahoo.com/tn?sid=2126005954&mid=AGjkimIAAAkoUdw7wQAAACwWcqw&midoffset=2_0_0_1_1024953&partid=2&f=1215&fid=Inbox&w=480&h=331
WASOMAJI WETU WAPENDWA AMBAO MMEINGIA KWENYE MFUNGO WA MWEZI MTUKUFU WA RAMADHANI, TUNAWATAKIA KILA LA HERI NA MFUNGO MWEMA TUKIWAOMBEA KWA ALLAH SUBHANNA WATAALA AWASAIDIE MTEKELEZE KWA SHUFAA NA UTIIFU IBADA HIYO SAMBAMBA NA KUWAKUMBUKA WOTE WENYE MATATIZO NA INSHALLAH TUWE NI WENYE KUFUZU MWISHOWE.
RAMADHANI KAREEM

MASOGANGE ANASWA NA DAWA ZA KULEVYA SAUZI?!

Agnes Gerard 'MASOGANGE'
Mellisa Edward
WALE wanawake wawili walionaswa majuzi nchini Afrika Kusini na shehena kubwa ya dawa za kulevya wamebainika ni watanzania na mmojawao jina lake linafanana kwa video queen anayetamba nchini, Agness Gerard 'Masogange'.
Wawili hao walinaswa Ijumaa iliyopita kwenye uwanja wa Ndege wa Oliver Tambo wakiwa wamebeba dawa hizo zente thamani ya Sh. Bilioni 6.8.
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Kitengo cha Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya, Geofrey Nzoa, alisema haijafahamika wanawake hao wanatoka mikoa gani.
Hata hivyo aliwataja wanawake hao kuwa ni Agnes Gerard, 25, na Melisa Edward, 24 ambao  bado wanaendelea kuhojiwa na polisi wa Afrika Kusini.
Ingawa Kamnada hakubainisha wazi, lakini jina la kwanza linafanana na la msanii mwenye mvuto wa kipekee aliyeshiriki kazi mbalimbali za wasanii wa muziki wa kizazi kipya akiwamo Belle 9, Prof Jay na wengine maarufu kama MASOGANGE.
Alisema Jeshi la Polisi Nchini kwa upande wake linaendelea kufanya uchunguzi kubaini kama dawa hizo walitoka nazo wapi na pia linawasaka watu ambao watakuwa ndiyo wamiliki wa dawa hizo.
Dawa walizokamatwa nazo kwa mujibu wa taarifa kutoka Afrika Kusini ni  Crystal Methamphetamine zenye thamani hiyo nchini Afrika Kusini wakati zikisafirishwa kutoka Tanzania.
Taarifa hizo zilionyesha kuwa wanawake wawili walikamatwa katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Oliver Tambo uliopo eneo la Kempton Park siku ya Ijumaa wiki iliyopita wakitokea Tanzania.
Wanawake hao walikamatwa na maofisa wa Mamlaka ya Mapato ya Afrika Kusini wakiwa na masanduku sita ambayo yalipokaguliwa yalikutwa na takribani kilo 150 za dawa hizo ambazo pia zinajulikana kama ‘Tik’ zikiwa na thamani ya bei ya mtaani ya Randi milioni 42 sawa na Sh. bilioni 6.8.
Baada ya kukamatwa na dawa hizo wanawake hao walikabidhiwa polisi.
Tukio hilo linatoka takribani wiki moja baada ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, Juni 28, mwaka huu kutangaza kuwa tatizo la dawa za kulenya hivi sasa ni janga la kitaifa nchini.
Alisema kumekuwa na wimbi kubwa la Watanzania wanaojiingiza katika biashara haramu ya dawa za kulevya ndani na nje ya nchi na kwamba, katika kipindi cha miaka mitano iliyopita, watuhumiwa 10,799 walikamatwa kwa kujihusisha na dawa hizo.
Pia alisema katika kipindi hicho, Watanzania 240 walikamatwa katika nchi za Brazil, Pakistan na Afrika Kusini, na hivyo kuharibu taswira ya nchi na kusababisha Watanzania wasio na hatia kupata usumbufu na masharti magumu wanapotaka kusafiri kwenda nchi mbalimbali duniani.
Pinda alisema mwaka huu pekee kumekuwa na ukamataji mkubwa wa dawa za kulevya katika eneo la kimataifa la Bahari ya Hindi karibu na Tanzania.
Alisema hivi sasa mikate, maandazi na askrimu zinazouzwa kwenye shule za msingi, zinawekwa dawa za kulevya.
Alisema vitendo hivyo vinafanya vijana wengi wa shule za msingi na hata sekondari kuwa na tabia za ajabu, ikiwamo kuingia darasani wakiwa na kiatu kimoja mguuni, mkufu wenye nyembe na kidani chenye nyembe kifuani.

Watu 40 wahofiwa kufa baada ya treni ya mafutaa kulipuka

Taswira ya treni iliyoripuka moto nchini Canada
MAAFISA wa usalama nchini Canada wamesema shughuli za kuwatafuta watu 40 ambao hawajulikani waliko, baada ya ajali treni ya mafuta kushika moto mwishoni mwa wiki iliyopita, imetatizika kutokana na mazingira magumu. 
 
Mkuu wa polisi wa eneo hilo la Quebec, Benoit Richard, amesema hakukuwa na shughuli ya uokozi jana usiku kwa sababu hali bado ni ya hatari mno, huku wazima moto wakijaribu kwanza kuhakikisha kuwa moto huo umezimwa kabisa. 
 
Richard amesema wengi wa wanaoshukiwa kutojulikana waliko walikuwa wanakunywa katika mkahawa mmoja karibu na ajali hiyo ilipotokea na mpaka sasa bado maafisa hao hawajaweza kufikia baa hiyo. 
 
Kiasi ya thuluthi moja ya idayi ya wakaazi 6,000 wa eneo hilo walilazimika kuhama makwao kutokana na moto huo uliosababishwa na ajali hiyo.

Du hii kali! Timu yafungwa mabao 146-0 hata hivyo zafungiwa


Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya NFF, Muke Umeh

KLABU nne za soka nchini Nigeria zimepigwa marufuku kujihusisha na mchezo huo kutokana na kutuhumiwa kupanga njama za upangaji wa matokeo ya michezo yao nchini humo.
Katika mechi moja klabu moja iliilaza nyingine magoli 79-0 na magoli 67-0 katika mechi ya pili. Jumla ya magoli 146 zilifungwa katika mechi hizo mbili, idadi ambayo inaingia katika vutabu vya kumbukumbu kama mechi iliyokuwa na idadi kubwa zaidi ya magoli duniani.
Klabu ya Plateau United Feeders iliilaza timu ya Akurba ili hali timu ya Polisi ya Machine FC kwa upande wake ikailaza Bubayaro magoli 67-0.
Mwenyekiti wa kamati andalizi ya shirikisho la mchezo wa soka nchini Nigeria, Muke Umeh amesema ufisadi na ulaghahi wa kiwango hicho hakiwezi kukubalika katika soka ya sasa.
Umeh ametangaza kuwa baada ya mkutano wa kamati hiyo, ilibainika wazi kuwa vilabu hivyo vina kesi ya kujibu na hivyo vyote vinne vimepigwa marafuku ya kushiriki katika mecho yoyote, hadi uchunguzi utakapokamilika.
Kabla ya mechi hiyo vilabu vya Plateau United Feeders na Police Machine vilikuwa na alama sawa na vilikuwa vikipania kupandishwa daraja hadi ligi daraja ya pili. Feeders ilipata magoli 72, katika kipindi cha pili ili hali Machine nao wameripotiwa kufunga magoli 61 katika kipindi cha mechi yao.
Kufuatia matokeo hayo Plateau ilimaliza ya kwanza kwenye msimamo wa ligi na idadi kubwa ya magoli ikifuatwa na timu hiyo ya polisi.
''Tutachunguza sakata hii na kuwachukulia hatua kali wote waliohusika'' Alisema Ummeh.
Mkurugenzi wa michezo na mashindano wa Shirikisho la mchezo wa soka nchini Nigeria, Dkt. Mohamed Sanusi, amekariri tangazo lililotolewa na mwenyekiti wa kamati andalizi kuwa waliohusika wataadhibiwa vikali.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na NFF, vilabu vilivyohusika, wachezaji,, maafisa wa kiufundi wa timu na wasimamizi wa mechi hiyo watakaopatikana kuhusika kwa njia moja au nyingine, katika kashfa hiyo ambayo imetajwa kuwa mbaya zaidi katika historia ya soka nchini Nigeria watachukulia hatua kali za kisheria.

BBC

Mashujaa wanogesha shamrashamra za Bonnah Kaluwa Cup

DC wa Ilala, Raymond Mushi akikabidhi mfano wa hundi kwa washindi

Wanenguaji wa bendi ya Mashujaa wakionyesha manjonjo yao

Chaz Baba akiimba sambamba na Diwani Bonnah Kaluwa

DC Mushi, akikabidhi washindi mfano wa hundi

Weweeeeee!  Diwani Bonnah Kaluwa akishangiliwa wakati akiserebuka Kibega cha Mashujaa

Chaz Baba akiwaongoza wanamashujaa
Aah Kibega....aah Kibega...Diwani akifanya vitu vyake mbele ya muimbaji Chaz Baba

Misri inatisha, inasikitisha kwa mauaji yanayoendelea



       

Refa achinjwa Brazili ni baada ya kumchoma kisu mchezaji

Mwamuzi aliyeuwawa
MWAMUZI wa soka nchini Brazili, Otavio Jordao da silver (20) ameuwawa kikatili na kunyofolewa kichwa baada ya kumchoma kisu na kumuua mchezaji Josenir Dos Santos Abreu (30) uwanjani katika mechi ya kienyeji iliyofanyika June 30. Moranhao, Brazil.
Taarifa zinasema kuwa, refa huyo aliingia katika mzozo na mchezaji huyo baada ya kupuliza kipenga. baada ya kushindwana katika ubishi huo, refa alichukua kisu cha mfukoni na kumchoma mara nyingi na kusababisha kifo cha mchezaji huyo ambae alifia njiani akikimbizwa hospitali.
Baada ya tukio hilo watu walio na hasira na wanao aminika kuwa ndugu na marafiki wa mchezaji huyo, walimshambulia refa huyo, wakaanza kumpiga, wakamfunga na kumpiga na mawe kabla ya kumkata kichwa na kukitundika kwenye mti na baadae kukisimika katikati ya uwanja.
Mpaka sasa polisi wanamshikilia Luiz Moraes de souza (27) kwa tuhuma za mauaji hayo, ambae amekubali kumtukana refa huyo lakini amekanusha kumuua.

SIMBA, YANGA WAKABIDHIWA VIFAA NA TBL




Ikiwa ni sehemu ya udhamini wake, bia ya Kilimanjaro Premium Lager imekabidhi vifaa vya michezo kwa klabu maarufu za Simba SC na Young Africans SC kwa ajili ya msimu wa 2013/14 wa Ligi Kuu inayotarajiwa kuanza mwezi ujao.

Meneja wa bia ya Kilimanjaro Premium Lager, George Kavishe alisema “Tunawapatia vifaa mapema kabla ya ligi kuanza ili wapate muda wa kutosha kujiandaa kwa ajili ya msimu wa 2013/14 ambayo bila shaka itakuwa na changamoto kubwa kwa timu hizi mbili na pia tunaamini kuwa siri ya mafanikio katika michezo ni maandalizi mazuri. Ni matumaini yetu kuwa wachezaji wapya waliosajiliwa Simba na Yanga wataiwakilisha Kili vizuri na kufurahia kuzichezea klabu hizi kongwe.”

Kavishe aliongeza kuwa Vifaa ambavyo leo tunatoa ni pamoja na mipira, viatu, soksi, shin guards, nguo za mazoezi, nguo za kawaida, gloves na vitu vingine vingi ambavyo vitawezesha timu hizi za Simba na Yanga kucheza wakifurahia kuvaa vifaa vyenye ubora wa hali ya juu.

Kilimanjaro Premium Lager kama mdhamini mkuu wa Simba na Yanga, na kinywaji kinachoongoza katika udhamini wa soka hapa nchini tunadhani kwamba uhusiano wetu na klabu hizi ni kiungo muhimu sana katika kuendeleza mpira wa miguu hapa Tanzania. Tutaendelea kutimiza wajibu wetu kwa klabu hizi na kama ilvyo kawaida yetu, tutahakikisha tunalifikisha soka la Tanzania kwenye kilele cha mafanikio. 

Kavishe alisema kuwa udhamini wa Kilimanjaro Premium Lager kwa Simba na Yanga umelenga kukuza soka la Tanzania, kuleta msisimko, na kuvutia mashabiki wengi wa mpira wakati na vilevile kuwaweka wachezaji wa Tanzania katika nafasi nzuri ya kimataifa.

Tunawashukuru viongozi wa Simba na Yanga, mashabiki wote, vyombo vya habari na wadau wote wa mpira kwa ushirikiano mzuri tunaoendelea kupata kwenye udhamini wetu na hiyo ndio siri ya mafanikio ya uhusiano wetu na klabu hizi mbili maarufu.

"Tunawaomba mashabiki wa Simba na Yanga waendelee kuiunga mkono bia yao ya Kilimanjaro Premium Lager kwani tunafanya kila jitihada kuwapa burudani na kufikisha soka la Tanzania kwenye kilele cha mafanikio."

Tenga asisitiza hakuna hila marekebisho ya Katiba

Rais wa TFF, Leodger Tenga akiwa na Katibu Mkuu, Angetile Osiah
Na Boniface Wambura
RAIS wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Leodegar Tenga amesema hakuna hila yoyote katika marekebisho ya Katiba kwa vile yametokana na maagizo ya Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA).

Akizungumza na Wahariri wa Michezo kwenye ofisi za TFF, Dar es Salaam leo (Julai 9 mwaka huu), Rais Tenga amewahakikishia wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Dharura kuwa dhamira ya marekebisho hayo ni nzuri, kwani lengo ni kila mtu apate haki yake.

Amesema Mkutano huo utakaofanyika Jumamosi (Julai 13 mwaka huu) utakuwa na ajenda moja tu ya kuingiza Kamati ya Maadili, na Kamati ya Rufani ya Maadili katika Katiba ya TFF kama ilivyoelekezwa na FIFA ili baadaye uanze mchakato wa uchaguzi.

“Katika kuunda Kamati ya Maadili tumeangalia ile ile ya FIFA, tusitengeneze kitu kipya, yaondolewe yale yanayotakiwa kuondolewa, na yaongezwe yale yanayotakiwa kuongozwa. Kwa sababu tumeangalia mazingira kwa Tanzania ni tofauti na Ujerumani au nchi za sehemu zingine,” amesema.

Rais Tenga amewataka wajumbe wafike kwenye Mkutano wakiwa na mtazamo wa kujenga, kwani kuna maagizo ya FIFA ambayo wanatakiwa kuyatekeleza ili wasonge mbele.

“Tutawaeleza kwanini hili limewekwa na lile limeondolewa. Mpira unataka unit (kitu kimoja), ni mchezo wa kila mtu. Baada ya hapa tunaanzisha mchakato wa uchaguzi. Watu wanaingia wakiwa wamoja, wanatoa hoja wanasikilizwa. Wanahukumiwa kwa hoja,” amesema na kuongeza utatolewa muda wa kutosha wajumbe ili wayaone na kuelewa marekebisho hayo.

Rais Tenga pia alizungumzia kipindi hiki cha usajili na kutaka klabu ziwaachie wataalamu wa mpira wa miguu kwani ndiyo wanaojua upungufu wa timu, hivyo wanaweza kusajili wachezaji sahihi.

Amesema tatizo kubwa la klabu za Tanzania ni kuwa timu zao hazina uwezo wa kuhimili dakika 90, hivyo watu wanapaswa pia kuzungumzia aina ya mazoezi ambayo timu zao zinafanya badala ya kubakia kutaja tu majina ya wachezaji wanaotaka kusajiliwa.

Kuziona Stars, The Cranes Buku 5 tu

Kikosi cha Stars
Na Boniface Wambura
KIINGILIO cha chini katika mechi ya mchujo ya Kombe la Afrika kwa Wachezaji wa Ligi za Ndani (CHAN) kati ya Tanzania (Taifa Stars) na Uganda (The Cranes) itakayochezwa Jumamosi (Julai 13 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ni sh. 5,000 kwa viti vya rangi ya kijani.

Viti vya kijani katika uwanja huo wenye uwezo wa kuchukua watazamaji 60,000 viko 19,648. Kwa upande wa viti vya rangi ya bluu ambavyo viko 17,045 kiingilio ni sh. 7,000. Kiingilio kwa viti vya rangi ya chungwa ambavyo viko 11,897 ni sh. 10,000.

Viingilio vya daraja la juu ni kama ifuatavyo; VIP C yenye watazamaji 4,060 ni sh. 15,000 wakati sh. 20,000 ni kwa VIP B yenye watazamaji 4,160. VIP A yenye watazamaji 748 kiingilio chake ni sh. 30,000.

Mechi hiyo ya kwanza ya raundi ya mwisho kuwania tiketi ya kucheza fainali hizo zitakazofanyika mwakani nchini Afrika itachezeshwa na mwamuzi Thierry Nkurunziza kutoka Burundi. Mechi ya marudiano itachezwa jijini Kampala kati ya Julai 26 na 28 mwaka huu.

Tiketi kwa ajili ya mechi hiyo itakayoanza saa 9 kamili alasiri zitaanza kuuzwa siku moja kabla ya mchezo (Ijumaa) katika vituo vifuatavyo; Shule ya Sekondari Benjamin Mkapa, Sokoni Kariakoo, mgahawa wa Steers ulioko mtaa wa Ohio/Samora, Oilcom Ubungo, Kituo cha Mafuta Buguruni, Dar Live Mbagala na BMM Barbershop iliyoko Sinza Madukani.

Katika vituo hivyo tiketi zitauzwa katika magari maalumu. Magari hayo pia yatafanya mauzo ya tiketi uwanjani siku ya mechi.

Tunapenda kuwakumbusha watazamaji kutonunua tiketi mikononi mwa watu au katika maeneo yasiyohusika ili kuepuka kununua tiketi bandia, hivyo kukosa fursa ya kushuhudia mechi hiyo.

Mikoa yahimizwa ratiba Copa Coca Cola 2013

Na Boniface WamburaSHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), linavitaka vyama vya mpira wa miguu vya mikoa kuwasilisha ratiba zao za michuano ya U15 Copa Coca-Cola kabla ya Julai 15 mwaka huu.

Ni vyama vya mpira wa miguu vya mikoa 16 pekee ambavyo ndivyo vimewasilisha TFF ratiba hizo mpaka sasa. Jumla ya mikoa 32 ya Tanzania Bara na Zanzibar inashiriki katika michuano hiyo ya umri chini ya miaka 15 kuanzia ngazi ya wilaya ambapo ngazi ya mikoa inatakiwa kuanza Julai 15 mwaka huu.

Mikoa ambayo tayari imewasilisha ratiba zao ni Arusha, Ilala, Kagera, Kaskazini Pemba, Kaskazini Unguja, Kigoma, Kinondoni, Kusini Pemba, Kusini Unguja, Manyara, Mara, Mjini Magharibi, Morogoro, Singida, Tanga na Temeke.

Wash United yakabidhi fulana kliniki ya TFF

Na Boniface Wambura
Taasisi ya Wash United inayojishughulisha na usaji na utunzaji mazingira imeikabidhi fulana 200 na dola 1,000 za Marekani kwa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa makubaliano kati yake na TFF yaliyosainiwa Novemba mwaka jana.

Fulana hizo kwa ajili ya kliniki za kila wikiendi (Jumamosi na Jumapili) zinazoendeshwa na TFF katika vituo 20 nchini kikiwemo cha Karume ikiwa ni sehemu ya mpango wa grassroots unaoshirikisha watoto wa umri kati ya 6 na 17 zimekabidhiwa na Mratibu wa Wash United, Femin Mabachi.

Hafla ya kukabidhi msaada huo imefanyika leo (Julai 9 mwaka huu) kwenye ofisi za TFF ambapo kwa upande wake ulipokelewa na Ofisa Maendeleo wake Salum Madadi.

Wash United inafadhiliwa na Serikali ya Ujerumani kupitia shirika lake la maendeleo la GIZ, na hapa nchini moja ya eneo wanalotumia katika kampeni hiyo ili kupambana na magonjwa kama kuhara yanayosababishwa na uchafu ikiwemo kutonawa mikono vizuri, hivyo kusababisha vifo kwa Watanzania ni mpira wa miguu.