STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, July 9, 2013

Wash United yakabidhi fulana kliniki ya TFF

Na Boniface Wambura
Taasisi ya Wash United inayojishughulisha na usaji na utunzaji mazingira imeikabidhi fulana 200 na dola 1,000 za Marekani kwa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa makubaliano kati yake na TFF yaliyosainiwa Novemba mwaka jana.

Fulana hizo kwa ajili ya kliniki za kila wikiendi (Jumamosi na Jumapili) zinazoendeshwa na TFF katika vituo 20 nchini kikiwemo cha Karume ikiwa ni sehemu ya mpango wa grassroots unaoshirikisha watoto wa umri kati ya 6 na 17 zimekabidhiwa na Mratibu wa Wash United, Femin Mabachi.

Hafla ya kukabidhi msaada huo imefanyika leo (Julai 9 mwaka huu) kwenye ofisi za TFF ambapo kwa upande wake ulipokelewa na Ofisa Maendeleo wake Salum Madadi.

Wash United inafadhiliwa na Serikali ya Ujerumani kupitia shirika lake la maendeleo la GIZ, na hapa nchini moja ya eneo wanalotumia katika kampeni hiyo ili kupambana na magonjwa kama kuhara yanayosababishwa na uchafu ikiwemo kutonawa mikono vizuri, hivyo kusababisha vifo kwa Watanzania ni mpira wa miguu.

No comments:

Post a Comment