STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, January 2, 2015

Bosi wa Wigan afungiwa kwa ubaguzi

http://cdn.images.express.co.uk/img/dynamic/67/590x/Dave-Whelan-538904.jpgMMILIKI wa klabu ya Wigan Athletic Dave Whelan amefungiwa kwa wiki sita kujishughulisha na masuala yeyote ya michezo na kutozwa faini ya paundi 50,000 kwa kutoa kauli ya kibaguzi kuwalenga watu wenye asili ya Uyahudi na Wachina. 
Tajiri huyo mwenye umri wa miaka 78 ambaye amepewa wiki moja kukata rufani kuhusiana na adhabu hiyo pia ametakiwa kuhudhuria darasa la ushauri litakalokuwa likiendeshwa na Chama cha Soka cha Uingereza. 
Mwezi uliopita Whelan alikubali tuhuma hizo lakini alikataa kauli alizotoa wakati akihojiwa na gazeti moja kuwa za kibaguzi. 
Novemba mwaka huu Whelan alidai kuwa atajiuzulu kama akikutwa na hatia ya kuwa mbaguzi.

No comments:

Post a Comment