STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, January 2, 2015

Breaking News! Panya Road waleta taharuki jijini Dar

http://freemedia.co.tz/daima/wp-content/uploads/2014/05/mwitu_2.jpg
Picha ya Maktaba mmoja wa vijana wa kundi la Panya Road akiwa amepewa kipigo mapema mwaka jana walipofanya uvamizi kama huu
TAARIFA zilizotufikia hivi punde zinasema kuwa mitaa kadhaa jijini Dar es Salaam 'kimenuka' baada ya kundi la vijana wahuni lifahamikalo kama 'Panya Road' limesambaa mitaani likipora na kufanya uhuni mwingine.
Mitaa ambayo inadaiwa kuvamiwa na kundi hilo linaloundwa na vijana zaidi ya 20 wakipora kwenye nyumba maduka na magari wakiwa na silaha ni Sinza, Magomeni, Tandale , Kinondoni na Mwananyamala.
Pia Tabata, Ubungo na Yombo inadaiwa vijana hao wameshika hatamu na kufanya vurugu, na kuleta taharuki kwa wakazi wa jijini, ingawa mpaka sasa jeshi la Polisi halijatoa taarifa zozote kuhusu matukio hayo.
Hata hivyo watu wlaioidokeza MICHARAZO wanasema kundi hiloi limeamua kuingia mitaani baada ya mmoja wao kuuwawa usiku wa kuamkia jana na ni kama wanalipa kisasi wakivamia na kujeruhi watu kwa silaha za jadi.
MICHARAZO inaendelea na juhudi za kusaka taarifa toka jeshi la polisi na juhudi wanazofanya kulizima kundi hilo ambalo linadaiwa ni kama limeteka jiji kwa sasa.

No comments:

Post a Comment