STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, January 2, 2015

Simba bado gonjwa, yapigwa na Mtibwa Mapinduzi Cup

KIKOSI cha Simba kikiwa tayari na vita dhidi ya Mtibwa kwenye michuano ya Kombe la Mapinduzi, ambapo Mnyama alikubali kipigo cha bao 1-0 lililowekwa kimiani na Nahodha wao wa zamani, Henry Joseph katika dakika ya 44. Kipigo hicho ni cha pili mfululizo kwa Simba baada ya wiki iliyopita kupigwa baoa 1-0 na 'ndugu' wa Mtibwa, Kagera Sugar kartika pambano la Ligi Kuu Tanzania Bara. (Picha kwa hisani ya ZanziNews
Wachezaji wa timu ya Mtibwa Sugar wakipasha moto misuli kabla ya kukaguliwa na Mgeni Rasmi Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi, wakati wa ufunguzi wa michuano hiyo iliyoanza jana Uwanja wa Amaan Zanzibar.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi, akisalimiana na Kamisaa wa Mchezo huo Muhsin Kamara, wakati wa uzinduzi wa michuano ya Kombe la Mapinduzi yaliozinduliwa leo na Balozi Seif, katika uwanja wa Amaan.    
Makamu wa Pili wa Rais wac Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akisalimiana na Wachezaji wa timu ya Simba kabla ya kuanza kwa mchezo huo wa ufunguzi uliofanyika uwanja wa Amaan usiku jana.
Makamu wa Pili wa Rais wac Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akisalimiana na Wachezaji wa timu ya Mtibwa Sigar,kabla ya kuaza kwa mchezo huo wa ufunguzi uliofanyika uwanja wa Amaan usiku wa jana
Wachezaji wa timu ya Simba wakisalimiana na Wachezaji wa timu ya Mtibwa Sugar kabla ya kuaza kwa mchezo wao wa ufunguzi uliofanyika uwanja wa Amaam. Timu ya Mtibwa imeshinda bao 1--0
Kikosi cha Simba kilichokubali kipigo cha bao 1-0 kwa mara ya pili mchezo wa mwanzo dhidi ya Mtibwa Sugar baada ya msimu uliopita kunyukwa mabao 4-2.
Kikosi cha  timu ya Mtibwa Sugar kilichotoka kifua mbele dhidi ya ushindi wa bao 1-0 dhidi ya timu ya Simba wakati wa mchezo wa ufunguzi wa Kombe la Mapinduzi uliofanyika usiku wa jana uwanja wa Amaan Zanzibar.
Makamu wa Rais wa Simba, Nyange Kaburu alikuwa akishuhudia kipigo kando ya kocha wa Mbeya City, Juma Mwambusi.
KOcha mpya wa Simba, Goran Kapunovic akiwa na Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Simba wakifuatilia mchezo huo wa jana
Makocha wa Yanga, Hans van der Pluijm na Boniface Mkwasa walikuwapo uwanjani

No comments:

Post a Comment