STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, January 2, 2015

Yanga yamtosa Kaseja Kombe la Shirikisho Afrika

Kipa Juma Kaseja
Yanga
Azam
KLABU ya Yanga imemtosa rasmi kipa wao waliye kwenye mgogoro naye, Juma Kaseja baada ya kutolituma jina lake kwenye kikosi cha timu hiyo kwa ushiriki wa michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.
Jina la Kaseja si miongoni mwa wachezaji 24 waliopo kwenye orodha iliyotumwa ofisi za CAF kwa usajili wa michuano hiyo ambayo itakayoanza katikati ya mwaka huu kwa Yanga kuumana na BDF IX ya Botswana.
Kaseja amekuwa na mgogoro na klabu hiyo ya Jangwani kutokana na kutochezewa kwenye mechi za Ligi Kuu hivyo kuomba kupitia wakili wake kuachwa na timu hiyo, huku Yanga wakitangaza kuendelea kumkomalia kwa kuwa wana mkataba naye.
Wakati Yanga ikituma majina 24, nao mabingwa wa Tanzania Azam watakaoshiriki Ligi ya Mabingwa Afrika wakianza kibarua chao kwa kuumana na El Merreikh imetuma pia idadi ya wachezaji kama hiyo kwa ajili ya ushiriki wa michuano hiyo watakayoicheza kwa mara ya kwanza mwaka huu.
Kikosi cha Yanga kilichowasilishwa CAF kwa mujibu wa taarifa ambazo MICHARAZO inayo ni Makipa: Ally Mustafa 'Barthez' na Deogratius Munishi 'Dida', Mbuyu Twite, Juma Abdul, Nadir Haroub 'Cannavaro', Edward Charles, Kelvin Yondani, Salum Telela, Rajab Zahir, Andrey Coutinho na Haruna Niyonzima.
Wengine ni Said Juma, Hassan Dilunga,  Sherman Kpah, Jerson Tegete, Pato Ngonyani, Nizar Khalfan, Mrisho Ngassa, Alphonce Matogo, Amissi Tambwe, Hussein Javu, Said Juma,  Danny Mrwanda na Simon Msuva.
Kikosi cha Azam kilichopelekwa CAF ni; Mwadini Ali, Gadiel Michael, Shomari Kapombe, Serge Wawa, Erasto Nyoni, Kelvin Friday, Salum Abubakar 'Sure Boy', Khalid Haji, Kipre Tchetche, Didier Kavumbagu, David Mwantika, Aggrey Morris na Amri Kiemba.
Wengine ni Said Morad, Frank Domayo, John Bocco, Yahya Mudathir, Brian Majwega, Khamis Mcha, Himid Mao, Gaudence Mwaikimba, Waziri Salum, Aishi Manula na Wilfred Michael Bolou.

No comments:

Post a Comment