STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, January 2, 2015

Vumbi la Ligi Kuu Tanzania Bara kuendelea bila vigogo

Kagera Sugar watakaoifuata Ruvu Shooting
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiyEobPE20ZtNi1R-UopKnA1am4dMWYZsa7756AEyfSHcvOosRNMAP-efMmHJrvyF7Ow87HahcM35Mc0PHS1WKnJYrQVgpIPDUG7wM0AXLdLATZWM_FgJbvsrDo8w3YZiZ3RL3zmCrX9Dff/s640/DSC_0125.JPG
JKT Ruvu ambao watavaana na Coastal Union jijini Tanga

Ruvu Shooting

Prisons Mbeya watakaoikaribisha Ndabnda Fc Jumapili
Ndanda watakaojiuliza tena mjini Mbeya
KIPUTE cha Ligi Kuu Tanzania Bara kinatarajiwa kuendelea wikiendi hii, bila kushuhudiwa vigogo, Simba, Yanga, Azam na Mtibwa Sugar ambazo zipo visiwani Zanzibar kushiriki michuano ya Kombe la Mapinduzi.
Kwa mujibu wa ratiba ya ligi hiyo kesho kutakuwa na michezo mitatu tu itakayozikutanisha timu za Coastal Union itaikaribisha JKT Ruvu kwenye uwanja wa Mkwakwani, Tanga.
Pambano jingine la kesho litazikutanisha timu za Ruvu Shooting watakaovaana na Kagera Sugar kwenye dimba la Mabatini, Mlandizi Pwani.
Mchezo wa mwingine utakaopigwa kesho Jumamosi ni Stand United itakayokuwa nyumbani mjini Shinyanga kuikaribisha Polisi Morogoro waliotoka kupata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Mgambo JKT ambao wapo likizo kwa vile mpinzani wake, Simba yupo Zanzibar kwenye michuano ya Kombe la Mapinduzi 2015.
Ratiba hiyo hiyo ya ligi inaonyesha kuwa siku ya Jumapili kutakuwa na mchezo mmoja tu utakaozikutanisha maafande wa  Prisons-Mbeya dhidi ya Ndanda ya Mtwara kwenye uwanja wa Sokoine jijini Mbeya.
Msimamo wa ligi hiyo upo hivi;
                                           P   W    D    L    F   A   GD  Pts
 01. Mtibwa Sugar              08  04   04   00  11  04   07   16
02. Yanga                           08  04   02   02  11  07   04   14
03.  Azam                           08  04   02   02  10  06   04   14
04.  Kagera Sugar               08  03   04   01  07  04   03   13
05.  Coastal Union              08  03   03   02  09  07   02   12
06.  Polisi Moro                  08  03   03   02  08  07   01   12
06. JKT Ruvu                     08  03   01   04  07  08    -1   10
07. Ruvu Shooting              08  03   01   04  05  07    -2   10
08.Stand Utd                       08  02   04   02  06  10    -4   10
09.Simba                             08  01   06   01  07  07    00  09
09. Mgambo JKT                08  03   00   05  04  09    -5   09
12. Mbeya City                   08  02   02   04  03  06    -3   08
13. Prisons                          08   01   04  03   06  07    -1  07
14. Ndanda Fc                     08  02   00  06   08  13    -5  06
Wafungaji Bora:
5-
Didier Kavumbagu (Azam)
4-
Rama Salim (Coastal), Danny Mrwanda, Simon Msuva (Yanga) Ame Ally (Mtibwa), Rashid Mandawa (Kagera Sugar)
3-
Ally Shomari, Emmanuel Okwi (Simba)

2- Shaaban Kisiga, (Simba), Nassor Kapama (Ndanda), Salum Kanoni (Kagera), Aggrey Morris (Azam),  Najim Magulu, Samuel Kamuntu, Jabir Aziz (JKT Ruvu), Amissi Tambwe, Jerry Tegete (Yanga), Ibrahim Kihaka (Prisons), Mussa Mgosi (Mtibwa), Heri Mohammed (Stand Utd), Ally Nassor (Mgambo),  Malimi Busungu (Mgambo), Nicolaus Kabipe (Polisi) 
Mechi za Ligi Kuu; Jan 03, 2014
Coastal Union vs  JKT Ruvu
Ruvu Shooting vs Kagera Sugar
Azam vs Mtibwa Sugar (Imeahirishwa)
Stand United vs Polisi Moro
Mbeya City  vs  Yanga (Imeahirishwa)

Jan 4, 2015 
Mgambo JKT vs  Simba (Imeahirishwa) 
Prisons vs  Ndanda

No comments:

Post a Comment