STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, January 2, 2015

Chelsea, Arsenal zagongwa, Man City yaikamata Chelsea

Danny Rose akifunga bao la Spurs
Harry Kane hunts down Chelsea's Cahill as the central defender knocks the ball back towards his goalkeeper
Vita ya Chelsea na Spurs
Alexis Sanchez, played up front in the absence of Danny Welbeck and Olivier Giroud, tries to escape the attentions of Steven Davis 
Arsenal ilipokufa kwa watakatifu wa Southampton
Fabricio Coloccini rises above Danny Ings during the 3-3 draw at St James' Park on New Year's Day
Newcastle United walipolazimishwa sare ya 3-3 na Burnley
LIGI Kuu ya England (EPL) iliendelea usiku wa jana kwa kushuhudiwa vigogo vya ligi hiyo vikishindwa kutamba kwa vinara Chelsea ikinyukwa mabao 5-3 na Tottenham Hotspur.
Ukiachana pambano la mapema liliikutanisha Stoke City iliyoikaribisha Manchester United na kumalizika kwa sare ya 1-1, Arsenal walikumbana na kipigo toka kwa Southampton.
Chelsea wakiwa wageni wa Spurs uwanja wa White Hart Lane walipoteza mchezo huo kwa kunyukwa kwa mabao 5-3.
Mshambuliaji Diego Costa alitangulia kufunga bao la mapema katika dakika 18 baada ya kumalizia mpira wa shuti uliopigwa na Oscar na kugonga mwamba.
Spurs walisawazisha bao hilo kwenye dakika ya 30 mfungaji akiwa mshambuliaji kijana Harry Kane aliyefunga kwa shuti la umbali wa karibu mita 25 baada ya kumpita Oscar .
Spurs walipata bao la pili kupitia kwa beki wa kushoto Danny Rose ambaye alimalizia mpira wa Nacer Chadli uliogonga mwamba .
Winga Andros Townsend alifunga bao la tatu kwa mkwaju wa penati baada ya beki Gary Cahill kumchezea vibaya Danny Rose kabla ya Spurs walipata bao la nne kupitia kwa Harry Kane kabla ya kumalizia karamu kwa bao safi la Nacer Chadli.
Mabao mengine ya Chelsea yalifungwa na Eden Hazard na John Terry .
Mara ya mwisho kwa Chelsea kufungwa idadi kubwa ya mabao kwenye ligi kuu ya England  ilikuwa mwaka 1991 ambapo walifungwa na Nottingham Forest 7-0.
Arsenal wakiwa kwenye uwanja wa St Mary’s walikubali kipigo cha 2-0 mbele ya Southampton huku mabao yote mawili yakifungwa kutokana na makosa ya kizembe ya kipa Wojciech Szczesny.
Wafungaji wa Saints kwenye mchezo huo walikuwa Sadio Mane na Dusan Tadic .
Katika michezo mingine Manchester City walishinda  mchezo wao dhidi ya Sunderland kwa 3-2 , Liverpool  na Leicester City wakitoka sare ya 2-2  wakati Newcastle  na Burnley nao walifunga 3-3.
West Ham United na West Brom wakiendeleza mfululizo wa sare baada ya kufungana 1-1.
Kwa matokeo hayo yameifanya Chelsea kubaki kileleni  mwa msimamo lakini ikilingana kila kitu na Manchester City.
Timu zote zina pointi 46 wakifunga mabao 44 na kufungwa mabao 19.
MATOKEO YA EPL MWAKA MPYA HAYA HAPA
Stoke 1-1 Man Utd
Aston Villa 0-0 Crystal Palace
Hull City 2-0 Everton
Liverpool 2-2 Leicester City
Man City 3-2 Sunderland
Newcastle Utd 3-3 Burnley
QPR 1-1 Swansea City
Southampton 2-0 Arsenal
West Ham 1-1 West Brom
Tottenham 5-3 Chelsea

No comments:

Post a Comment