STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, January 2, 2015

Podolski awindwa Inter Milan

http://1nildown2oneup.net/wp-content/uploads/2013/12/LukasPodolskiMontpelliervArsenalpa_2830453.jpg
Lucas Podolski
OFA kutoka klabu ya Inter Milan imetua mezani mwa uongozi wa klabu ya Arsenal kwa ajili ya kumwinda, Lucas Podolski na klabu hiyo itafikiria ofa hiyo iliyoimarishwa.
Podolski, 29 ameshindwa kupata namba katika kikosi cha kwanza cha Arsenal msimu huu huku akiukosa mchezo dhidi ya Southampton jana kutokana na kusumbuliwa na maumivu ya nyonga.
Kocha wa Arsenal, Arsene Wenger amesema ofa ya kwanza waliyotoa Inter ilikuwa ndogo hivyo kama wakirudi tena na fungu la kueleweka wataangalia uwezekano wa kufanya biashara.
Podolski alinunuliwa na Arsenal kwa kitita cha paundi milioni 11 akitokea klabu ya Cologne mwaka 2012 lakini amefanikiwa kuanza kucheza mechi 39 pekee katika akiwa chini ya Wenger.
Mshambuliaji huyo amefunga jumla ya mabao 31 katika mechi 82 alizoichezea Arsenal katika mashindano yote.
Pazia la dirisha dogo la usajili nchini England linatarajiwa kufunguliwa kesho Jumamosi na tayari tetesi zimeshaanza juu ya nani na nani anawindwa wapi. 

No comments:

Post a Comment