STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, December 21, 2014

Rais JK kukataje kiu ya watanzania kesho?

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhLcBTaUn2K5EFfb-YZJkKO2h55foHxnikx-untCz65m2xFREdv72IRXmAU_a7FExuI-7Hw5MHx9rhneKpTihkeuDO10muvGq9ZF-2fuNkIHaiu6ZqaXXNF8BKaaQdnVef9igzFvd2t6Hs/s640/Rais+JK+2.jpgRAIS Jakaya Kikwete anasubiriwa kwa hamu na watanzania kukata kiu juu ya baadhi ya mambo yaliyojiri nchini ambayo yameliacha taifa kwenye sintifashamu.
Sakata la uchotwaji wa fedha katika Akaunti ya Tegeta Escrow zipatazo bil. 306, na mvurugano uliojitokeza kwenye uchaguzi wa Serikali za mitaa, vijiji na vitongoji ni kati ya vinavyosubiriwa kusikia Rais atasema nini.
Juzi watanzania walidokezwa kuwa kungekuwa na fursa kwa Rais kuzungumza na wananchi kabla ya kurugenzi ya mawasiliano ya Ikulu kukanusha taarifa hizo na kudai Rais atazungumza na Watanzania kesho kupitia Wazee wa mkoa wa Dar es Salaam.
Je mawaziri waliotajwa kuhusika kwa namna moja juu ya sakata ya Escrow na uchaguzi wa serikali za mitaa waenda na maji au watapeta kulingana na duru za kisiasa na kauli ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Prof Anna Tibaigana kwamba hatajiuzulu na pia yeye na Rais wametoka mbali?
Ngoja tusubiri tuone Rais atakata kiu ya watanzania kivipi hiyo kesho katika hotuba yake!

Liverpool, Arsenal hakuna mbabe

Borini akilimwa kadi kizembe
Olivier Giroud akiifungia Arsenal bao la pili
PAMBANO la kukata na shoka baina ya Liverpool na Arsenal limemalizika hivi punde kwa timu hizo kutoka sare ya mabao 2-2, huku wenyeji wakimaliza pungufu baada ya Fabio Borini kuonyesha kadi ya pili ya njano iliyoambatana na nyekundu na kutolewa nje ya uwanja wakati timu yake ikiwa nyuma ya ba02-1.
Borini aliyeingia toka benchi alipewa kadi hiyo, dakika ya 90 lakini vijana na Branden Rodgers walicharuka na kurejesha bao dakika za majeruhi kupitia Martin Skrtel.
Kabla ya hapo wageni walipata bao la pili dakika ya 64 kupitia kwa Olivier Giroud na kuonekana kama Arsenal wataibuka na ushindi kabla ya beki Skrtel akiwa amefungwa kichwani kutokana na kuumia kuryka juu kuunganisha mpira wa kona uliopigwa na Adam Lallana na kuipa afueni Liverpool iliyoiengua Everton na kukaa nafasi ya 10 kutoka ile ya 11 waliokuwa wakishikilia.
Arsenal kwa sare hiyo imeishusha Tottenham hotspur na kukalia nafasi ya sita licha ya zote kulingana pointi 27 kila moja baada ya timu zote kucheza mechi 17, ila zinatenganishwa kwa tofauti ya mabao ya kufunga na kufungwa.

Zaidi ya Uuaji! Mwenye VVU amnyonyesha mtoto wa jirani

MWANAMKE mmoja raia wa Zimbabwe aliyenyonyesha mtoto wa jirani bila ruhusa anakabiliwa na kifungo cha karibu miaka miwili kwa kumwambukiza mtu HIV kwa kukusudia kwa kuwa yeye ni mwathirika.
Annie Mpariwa, 39, alifikishwa mbele ya mahakama ya Gaborone wiki iliyopita na kesi hiyo iliahirishwa hadi january 24 kuruhusu kipimo cha pili cha HIV kufanyiwa mtoto huyo.
Matokeo ya kwanza ya mtoto huyo yalionyesha hana virusi ilhali ya mama huyo yalikuwa na virusi. Mpariwa alikamatwa wiki jana kwa mashtaka ya usumbufu na iwapo mtoto huyo atapatikana na virusi, mashtaka hayo yatazidishwa hadi 'kumwambukiza mtu mwingine HIV kimakusudi.
Mama wa mtoto huyo wa miezi14, Nyasha Mironga,alisema kumwona mwanawe akinyonyeshwa na jirani wake lilikuwa ni jambo lililomshtua sana.
Kisa hicho kimetokea baada ya kupitishwa kwa sheria mpya ya HIV/Aids inayotoa adhabu kali zaidi kwa wale wanaowaambukiza.Je kama wewe ndio mwanao utachukua hatua gani?
ALWAYS POSITIVE ATTITUDE.

Copy and WIN : http://bit.ly/copy_win

Kumekucha Anfield! sasa mapumziko 1-1

Mathieu Debuchy akiisawazishia Arsenal bao dakika za majeruhi kabla ya mapumziko
Coutinho (10) kulia akiifungia Liverpool bao la kuongoza uwanja wa Anfield.

PAMBANO la Liverpool na Arsenal limeenda mapumziko matokeo yakiwa bao 1-1 baada ya wababe hao kutumia sekunde chache kabla ya mapumziko kupata mabao yake, wenyeji Liverpool wakianza kupitia Phillipe Coutinho katika dakika ya 45.
Hata hivyo dakika mbili za nyongeza, Mathieu Debuchy aliisawazishia timu yake ya Arsenal na kufanya mambo yaendelee kuwa magumu tofauti na mechi kama hiyo msimu uliopita ambapo mpaka dakika ya 20 Liverpool walikuwa tayari wapo mbele kwa mabao 4-0.

Muhammad Ali akimbizwa hospitalini

http://media.washtimes.com/media/image/2012/09/13/people-muhammad-ali_lea.jpg
Bingwa wa zamani wa Dunia, Muhammad Ali
 BINGWA wa zamani wa Dunia wa Ngumi za Kulipwa Uzito wa Juu, Muhammad Ali, amekimbizwa hopitalini baada ya kubanwa na 'Vichomi' (Pneumonia)
Mwanamasumbwi hiuyo aliyenyakua ubingwa huo wa dunia mara tatu kwa mujibu wa msemaji wake Bob Gunnell, hali yake inaendelea vema.
Gunnell amesema kwamba familia ya bingwa huyo mwenye miaka 72 inahitaji faragha wakati akiendelea kupata matibabu dhidi ya maambukizi hayo ya mapafu.
Kwa muda mrefu bondia huyo wa zamani amekuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa 'Kutetemeka' (Parkinson) tangu alipostaafu ngumi mwaka 1984.

Sunderland yaizamisha Newcastle Utd nyumbani kwao

Sunderland's Adam Johnson
Adam Johnson akiwaliza wapinzani wao
http://news.bbcimg.co.uk/media/images/79876000/jpg/_79876229_newcastlevsunderland.jpgSunderland's Steven Fletcher and Newcastle's Steven TaylorBAO la dakika ya 90 lililofungwa na Adam Johnson limeiwezesha Sunderland kuwatambia wapinzani wao wa jadi Newcastle United wakiwa nyumbani kwao katika mfululizo wa Ligi Kuu ya England.
Sunderland ambayo imekuwa ikipigana kuondoka maeneo ya mkiani, imeweza kufikisha jumla ya pointi 19 ns kuchupa hadi nafasi ya 14 ya msimamo wa ligi hiyo inayoongozwa na Chelsea.
Kipigo hicho cha Newcastle ni cha pili mfululizo katika ligi hiyo baada ya awali kupata ushindi mfululizo na kusaliwa na pointi zake 23 ikiwa nafasi ya 9.
Ligi hiyo inaendelea usiku huu kwa pambano la kukata na shoka kati ya Arsenal waliowafuata Liverpool nyumbani kwao kwenye uwanja wa Anfield na mpaka sasa matokeo ni 0-0.

Southampton yazinduka, Spurs kanyaga twende England

Southampton
Southampton wakiangika moja ya mabao yao
Graziano Pelle
Pelle akimtungua Tim Howard
Erik Lamela, Tottenham
Spurs wakiangilia moja ya mabao yao mawili walipoizamisha Burnley
BAADA ya kufungwa mechi tano mfululizo zikiwamo nne za Ligi Kuu na moja ya Kombe la Ligi, hatimaye Southampton wikiendi hii imezinduka baada ya kuinyoa Everton mabao 3-0 na kuendelea kusalia kwenye nafasi ya tano katika msimamo wa ligi hiyo inayoongozwa na Chelsea.
Bao la penati la Romeo Lukaku katika dakika ya 38 na mengine mawili ya kipindi cha pili kupitia kwaGraziano Pelle katika dakika ya 65 na lile la Maya Yoshida dakika nane kabla ya kumalizika kwa pambano kuliwafanya Southampton kuonja ushindi ikiwa nyumbani na kufikisha pointi 29.
Katika mechi nyingine za ligi hiyo Mashetani Wekundu wakiwa ugenini walishindwa kuitambia Aston Villa waliokuwa pungufu kw akutoka sare ya 1-1, Mabingwa watetezi, Manchester City wakipata ushindi wa nyumbani wa mabao 3-0 dhidi ya Crystal Palace na Tottenham Hotspur ikiwa nyumbani White Hartlane waliishinda timu ya Burnley mabao 2-2 na kuwaengua Arsenal waliokuwa juu yao.
Pia timu ya QPR ikiwa nyumbani iliwaduwaza wageni wao West Bromwich kwa kuwalaza mabao 3-2, Hull City ikakubali kipigo cha nyumbani cha bao 1-0 dhidi ya Swansea City na West Ham United ikatamba nyumbani dhidi ya Leicester City kwa kuilaza mabaio 2-0.
Ligi hiyo itaendelea leo kwa michezo miwili, Liverpool itaialika Arsenal uwanja wa Anfield na wapinzani wajadi Newcastle United itaonyeshana kazi na Sunderland katika mchezo mwingine kabla ya kesho kushuhudiwa vinara Chelsea wakikwaruzana na Stoke City ugenini.

Mkutano Mkuu wa TFF kufanyika mkoani Singida


Kamati ya Utendaji imejadili rasimu ya Kanuni za Leseni za Klabu (Club Licensing Regulations), na kuagiza Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ifanye marekebisho ya mwisho, kabla ya kanuni hizo kusainiwa na kuanza kutumika.
UANZISHAJI MFUKO WA MAENDELEO YA MPIRA WA MIGUU (FDF)Kamati ya Utendaji imepokea taarifa ya maendeleo ya mchakato wa uanzishwaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (Football Development Fund- FDF).
Imeipongeza Kamati ya Mfuko huo inayoongozwa na Rais wa zamani wa TFF, Leodegar Tenga, na kuitaka fanye jitihada za kukamilisha rasimu ya kanuni za uendeshaji mfuko huo.
Mbali ya Tenga, wajumbe wengine wa mfuko huo ni Ayoub Chamshama, Ephraim Mafuru, Frederick Mwakalebela, Tarimba Abbas na Zarina Madabida. Sekretarieti ya mfuko huo inaundwa na Henry Tandau ambaye ni Katibu, Wakili Emmanuel Muga na Boniface Wambura.
FDF ambao ni mfuko utakaokuwa unajitegemea utakuwa unashughulika na maendeleo ya mpira wa miguu kwa vijana, na nyanja nyingine za maendeleo kwa mchezo huo.
MKUTANO MKUU KUFANYIKA SINGIDA MACHI 14
Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imepanga Mkutano Mkuu wa Kawaida wa mwaka ufanyike Machi 14 na 15 mwakani mjini Singida.
MGOGORO NDANI YA ZFA
Kamati ya Utendaji imepokea kwa masikitiko taarifa za masuala ya mpira wa miguu Zanzibar kupelekwa mahakamani.
Kwa mujibu wa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) kitendo hicho ni kinyume cha taratibu za uendeshaji mpira wa miguu ambazo zinakataza masuala ya mchezo huo kupelekwa katika mahakama za kawaida.
Kamati ya Utendaji inatoa rai kwa pande zote mbili zinazohusika na mgogoro huo kukaa kwenye meza ya mazungumzo ili kumaliza tofauti zao.
Kamati ya Utendaji imejitolea kutuma ujumbe wake Zanzibar ili ukutane na pande zinazohusika katika mgogoro huo.
Ni muhimu usuluhisho upatikane haraka ili tuweze kujua hatma ya washiriki wetu kwenye michuano ya Kombe la Mapinduzi.

Raheem Sterling atwaa tuzo akiisubiri kwa hamu Arsenal leo

http://assets.lfcimages.com/uploads/9559__1458__sterling560_512X287.jpg
Raheem Sterling akiwa na tuzo yake
http://i1.liverpoolecho.co.uk/incoming/article8287825.ece/alternates/s1023/JS52985656.jpg
Sterling akiwajibika uwanjani

WAKATI leo akitarajiwa kuiongoza klabu yake ya Liverpool watakapoikaribisha Arsenal, Raheem Sterling amefanikiwa kushinda tuzo ya Golden Boy kwa mwaka huu na kuwa Mwingereza wa kwanza kushinda tuzo hiyo toka Wayne Rooney aliposhinda mwaka 2004. Msghambuliaji huyo nyota wa Liverpool ametwaa tuzo hiyo kwa umahiri wake uliomfanya kuwa mchezaji muhimu katika kikosi cha Liverpool huku akiwa amejihakikishia namba katika kikosi cha timu ya taifa. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 20, amewashinda chipukizi wenzake akiwemo Adnan Januzaj wa Manchester United na Hakan Calhanoglu wa Bayer Leverkusen pamoja an wachezaji wenzake wa Liverpool Lazar Markovic na Divock Origi. 
Akihojiwa Sterling aliuambia mtandao wa Liverpool kuwa ni mafanikio makubwa kushinda tuzo kama hiyo na ni jambo la furaha kwake na familia yake. Wachezaji wengine wlaiowahi kushinda tuzo hiyo ni pamoja na Lionel Messi, Cesc Fabregas na Sergio Aguero.
Mshambuliaji huyo leo anatarajiwa kuingoza timu yake kuikaribisha Arsenal kwenye uwanja wa Anfield katika mechi ya Ligi Kuu ya England linalosubiriwa kwa hamu.
Katika mechi kama hiyo katika msimu uliopita, Raheem akisaidiana na nyota wenzake Martin Skrtel na Daniel Sturridge waliiangamiza Arsenal kwa mabao 5-1.
Raheem katika mchezo huo alifunga mabao mawili sawa na Skrtel na jingine liliwekwa kimiani na Sturridge ambaye bahati mbaya leo hatakuwepo dimbani kutokana na kuwa majeruhi.
Pia mchezaji aliyechangia ushindi huo Luis Suarez hayupo kikosini kwa vile amehamia Barcelona hali na kwa mwenendo iliyonayo timu hiyo msimu huu inaleta mashaka kama wanaweza kurudia ilichofanya msimu uliopita.

M

Real Madrid bingwa wa Dunia, Aucland City waitoa nishai Cruz Azul

Bale akilibuzu kombe la Klabu Bingwa la Dunia baada ya jana kuiwezesha Real Madird kulitwaa kwa kuinyuka San Lorenzo
Wachezaji wa Real madrir wakiwa na taji la Klabu Bingwa la Dunia
Wachezaji wa Real Madrid wakishangilia taji lao
Real Madrid star Cristiano Ronaldo kisses the Club World Cup trophy after their triumph
Ronaldo akilibusu taji
MABINGWA wa Ulaya, Real madrid wameliwekwa kibindoni taji la kwanza la Klabu Bingwa ya Dunia na kuwa taji la nne katika mwaka 2014 baada ya kuinyuka San Lorenzo ya Amerika Kusini kwa mabao 2-0.
Madrid iliinyoa Mabingwa hao wa Amerika Kusini katika panbano la fainali ya michuano hiyo ya Klabu Bingwa Duniani lililochezwa usiku wa jana mjini Marrakech, Morocco ikiwa ni baada ya miaka 12 tangu klabu hiyo iliposhiriki michuano hiyo.
Mabao ya beki Sergio Ramos katika dakika ya 37 na jingine na winga na mchezaji ghali duniani, Gareth Bale katika dakika ya 51 yalitosha kuwapa Real Madrid taji hilo la kwanza kwao na kuendeleza reklodi ya kucheza mechi 22 bila kupoteza msimu huu.
Katika mechi nyingine ya kusaka mshindi wa tatu wa michuano hiyo timu ya Aucland City ya New Zealand ilifanikiwa kutwaa ushindi wa tatu baada ya kuinyuka Cruz Azul ya Mexico kwa mikwaju ya penati 4-2.
Awali timu hizo zilizomaliza muda wa kawaida wa dakika 90 na ule wa nyongeza wa 120 kwa kufungana bao 1-1, Wamexico wakilazimika kusawazisha baada ya kutanguliwa na wapinzani wao ambao waliong'olewa hatua ya Nusu fainali za San LOrenzo.