STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, December 21, 2014

Sunderland yaizamisha Newcastle Utd nyumbani kwao

Sunderland's Adam Johnson
Adam Johnson akiwaliza wapinzani wao
http://news.bbcimg.co.uk/media/images/79876000/jpg/_79876229_newcastlevsunderland.jpgSunderland's Steven Fletcher and Newcastle's Steven TaylorBAO la dakika ya 90 lililofungwa na Adam Johnson limeiwezesha Sunderland kuwatambia wapinzani wao wa jadi Newcastle United wakiwa nyumbani kwao katika mfululizo wa Ligi Kuu ya England.
Sunderland ambayo imekuwa ikipigana kuondoka maeneo ya mkiani, imeweza kufikisha jumla ya pointi 19 ns kuchupa hadi nafasi ya 14 ya msimamo wa ligi hiyo inayoongozwa na Chelsea.
Kipigo hicho cha Newcastle ni cha pili mfululizo katika ligi hiyo baada ya awali kupata ushindi mfululizo na kusaliwa na pointi zake 23 ikiwa nafasi ya 9.
Ligi hiyo inaendelea usiku huu kwa pambano la kukata na shoka kati ya Arsenal waliowafuata Liverpool nyumbani kwao kwenye uwanja wa Anfield na mpaka sasa matokeo ni 0-0.

No comments:

Post a Comment