STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, August 27, 2011

Mnanda wamtoa Ferouz wa Daz Nundaz


MSANII nyota wa muziki wa kizazi kipya nchini, Feruzi Mrisho 'Ferouz' aliye mbioni kuachia kazi yake mpya iitwayo 'Ndege Mtini', amedai kibao hicho alichokiimba katika miondoko ya Mchiriku utamrejesha kwenye chati yake ya zamani.
Ferouz aliyekuwa kimya karibu miaka mitatu iliyopita, alisema aliamua kuimba kibao hicho kipya alichomshirikisha chipukizi wa THT, Shoz Dia, miondoko ya 'mnanda' ili kurudi upya.
"Nimeamua kutoa upya na mnanda kwa nia ya kurejesha makali yangu, pia kuonyesha utoauti wa Ferouz wa Das Nundaz au wa 'Starehe' na huyu wa sasa," alisema.
Mkali huyo aliyetamba na vibao kadhaa kikiwemo hicho cha Starehe alichoimba na Profesa Jay, alisema kibao hicho cha Niwqe Nawe anachojiandaa kukifyatulia video yake, ni utangulizi wa ujio wa albamu yake mpya itakayofahamika kwa jina la 'Reserve'.
Aliongeza ndani ya albamu hiyo atakayowashirikisha wasanii kadhaa nyota akiwemo mshindi wa Tuzo Tano za Kili Music Awards-2011, 20 Percent itakuwa na nyimbo nane.
Feropuz alizitaja nyimbo hizo kuwa ni pamoja na Ndege Mtini, Nimemfukuza, 'Reserve' na Tusifuatane.
Hiyo itakuwa ni albamu ya tatu kwa mkali huyo kwani baada ya kutoa albamu ya 'Safari' mwaka 2004 iliyokuwa na wimbo wa Starehe, alifyatua nyingine ya pili iitwayo Sauti Nyimbo na Vyombo iliyokuwa na wimbo wa 'Mr Policeman, kabla ya kutoweka hadi alipobuka juzi.

Mwisho.

Kaseba, Oswald kuzipiga Okt Mosi




BINGWA wa zamani wa ngumi za kulipwa nchini, Ernest Bujiku na Chaurembo Palasa ni kati ya mabondia watakaopanda ulingoni kusindikiza pambano la mkongwe Maneno Oswald na Japhet Kaseba litakalofanyika Oktoba Mosi.
Pambano hilo la raundi 10 lisilo la ubingwa la uzani wa kilo 72 la Kaseba na Oswald maarufu kama Mtambo wa Gombo litafanyikia kwenye ukumbi wa hoteli ya Travertine Magomeni likisimamiwa na Shirikisho la Ngumi za Kulipwa nchini, PST, chini ya uratibu wa promota, Gervas Muganda wa kampuni ya Babyface ya jijini Dar.
Akizungumza na Micharazo jana, Kaseba, alisema kabla ya yeye kupigana na Oswald watasindikizwa na michezo kadhaa akiyataja baadhi likiwakutanisha Chaurembo Palasa dhidi ya Sweet Kalulu, Ernest Bujiku atakayepigana na Mbukile Chuwa.
Kaseba alisema pia siku hiyo Venance Mponji atapanda ulingoni kuzipiga na Jafar Majiha 'Mr Nice' na kutakuwa na michezo miwili ya kick boxing ambapo Ramadhani Mshana atapigana na Hamed Said na jingine la wapiganaji chipukizi.
Mkali huyo alisema amekuwa akiendelea kujifua vema ili kuweza kukkabili Oswald aliyekiri ni mmoja wa mabondia bora na wenye uwezo mkubwa katika mchezo huo.
"Naendelea kujifua kwa lengo la kutaka kumshinda Oswald ambaye namheshimu kwa umahiri wake katika mchezo wa ngumi, naamini nikizembea anaweza kunitoa nishai," alisema Kaseba.
Katika hatua nyingine, bondia Stan Kessy anatarajiwa kupanda ulingoni Septemba 25 kupigana katika pambano lisilo la ubingwa dhidi ya Seleman Habib, ambalo litasindikizwa na michezo mitano tofauti ya utangulizi.
Mratibu wa pambano hilo litakalofanyikia kwenye ukumbi wa Friend's Rangers jijini Dar es Salaam, Dk John Magambo, alisema Kessy na Habib watapigana kwenye uzani wa middle raundi 10 na kusindikizwa na mabondia wengine.
Dk Magambo aliwataja watakaowasindikiza wawili hao ni Salehe Mkalekwa atayaepigana na Jafari Majiha, Doto KIpacha dhidi ya Jones Godfrey, Yohana Thobias atayepigana na Huseni Mashaka na Omar Rajab dhidi ya Husseni Mandula.

Mwisho

UAE embassy used US$ 80,000 for Tanzania Moslems



The United Arab Emirate (UAE) embassy in the country through its charity organization Khalifa Bin Zaayid Al Nahyaan has set aside $80.000 to provide food and other necessities to Muslims in the country during this holly months of Ramadhan.
Disclosing this, Abdallah Ahmedna, who represented UAE ambassador to the country, Mallalla Mubarak Al –Ameri he said the money has been set aside to help people during this month of ramadhan, he said it’s the traditional of his embassy to help people especially this holly months.
He was speaking this at a futari provided by his embassy at Anwar mosque in Msasani.
“This is the fourth year for our embassy through Khalifa Bin Zaayid Al Nahyaan to provide food and money to people during this month of ramadhan” he said
Ahmedna also disclosed that from tomorrow his embassy will start giving out money to the elderly, the disabled and other less privileged people, he said the money will help them to buy food and other necessities at Eid El Fitry .
He disclosed that the exercise will begin at Al Rahman mosque in Kinondoni

Ubalozi watumia Dola 80,000 kufuturisha waislam Tz




UBALOZI wa Nchi ya Falme za Kiarabu, UAE nchini kupitia taasisi ya kutoa huduma za kijamii ya Khalifa Bin Zaayid Al Nahyaan, umekuwa ukitumia Dola za Kimarekani 80,000 kila mwaka kufutisha waumini wa kiislam waliopo jijini Dar na mikoa mingine.
Taarifa hiyo ilitolewa juzi na Mhasibu wa Ubalozi huo, Abdallah Ahmedna, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kwa niaba ya Balozi wa UAE, Sheikh Mallalla Mubarak Al Ameri wakati wa kuwaturusiha waumini wa msikiti wa Anwar, Msasani.
Ahmedna, alisema fedha hizo zimekuwa zikitolewa karibu mwaka wa nne sasa na ubalozi wao kwa ajili ya kuwafuturisha na kuwasaidia waumini wa misikiti 10 iliyopo mikoa ya Dar es Salaam, Morogoro, Lindi, Mwanza, Tanga, Pwani na Mtwara.
Alisema, msaada huo wa futari, daku na fedha kwa wasiojiweza hutolewa kwa muda wa mwezi mzima wa mfungo wa mwezi wa Ramadhani kila mwaka, ambapo kwa Dar mbali na msikiti wa Anwar mwingine unaonufaika ni Al Rahman, uliopo Kinondoni.
"Kama waislam tumekuwa tukithamini waumini wa Tanzania kwa kuwafuturisha pamoja na kuwapa misaada, ambapo ubalozi umekuwa ukifadhili misaada hiyo kwa kiasi cha Dola za Kimarekani 80,000 kwa kila mwaka," alisema.
Baadhi ya waumini waliofuturishwa msikiti hapo waliushukuru ubalozi huo na kuomba watu wengine wenye uwezo kuiga mfano huo wakidai mwezi huu ndio wa waumini wa kweli kuonyesha upendo, ukarimu na kuhurumiana katika kutekeleza nguzo ya nne kati ya tano za Imani za Kiislam.

Mwisho

Sekretarieti ya CCM yashtukiwa, ila Nape mmmh!



WASOMI wa Vyuo vya Elimu ya Juu wanaokiunga mkono chama tawala, CCM, wamemtaka Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye asitishwe na kauli za watu wachache katika kuendeleza moto aliouanza dhidi ya vigogo wanaoatakiwa kujivua gamba wakiapa kumuunga mkono kwa hali yoyote.
Kadhalika wanachama wa CCM hasa vijana wajipange na kujitokeza kwa wingi kuwania nafasi za uongozi ndani ya Jumuiya ya chama hicho, ili kuleta mabadiliko yatakairejeshea heshima chama hicho mbele ya wananchi.
Katibu wa Shirikisho la Wana-CCM Vyuo vya Elimu ya Juu mkoa wa Dar es salaam, Asenga Abubakar, alitoa kauli hizo juzi kupitia taarifa aliyoitoa kwa vyombo vya habari akizungumzia kufifia kwa moto ulioanzishwa na Sekratarieti ya chama chao.
Abubakar, alisema moto ulioanzishwa na sekretarieti ya chama hicho chini ya Katibu Mkuu, Wilson Mukama, ni kama imefifia na hasa zile kelele zilizokuwa zikitolewa na Nape Nnauye, wakidai huenda zimetokana na vitisho vinavyotolewa dhidi yao.
Hata hivyo shirikisho hilo lilimtaka Nnauye, kutohofia vitisho hivyo na badala yake aendeleze moto zaidi ili kuhakikisha chama cgao kinasimama imara dhidi ya wachache wanaoutolea macho nafasi ya Urais kwa Uchaguzi Mkuu ujao wa mwaka 2015.
"Tunamuomba asitishwe na wanaoutolea macho uraisi wa 2015 na wafuasi wao, sisi tunamuonga mkono na tupo pamoja nae dhidi ya wachache hao wenye njaa," taarifa hiyo ya Abubakar inasomeka hivyo.
Taarifa hiyo ya Abubakar, licha ya kuihimiza sekretarieti hiyo kusimama imara, pia imewaomba na kuwataka wanachama wa CCM waliopo vyuoni na vijana kwa ujumla kujitokeza kwa wingi kuwania nafsi katika uchaguzi mkuu wa chama hjicho utakaofanyika mwakani, ili kuleta mabadiliko mbele ya umma wa Watanzania.
Kadhalika shirikisho hilo limesisitiza kwa kuwataka vijana wasiamini kwamba ndani ya CCM kuna ufisadi, bali wafuasi wachache wa chama hicho ndio wenye vitendo hivyo na hivyo wakijitokeza kushiriki uchaguzi watasaidia kurahisisha dhana ya kujivua gamba na kukifanya CCM kiwe makini nchini.
Kwa muda mrefu ndani ya CCM kumekuwa na msigano wa shinikizo la kuwataka baadhi ya wanachama wao wanaotuhumiwa kwa vitendo vya ufisadi kujivua gamba, kitu kilichomlazimisha aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Igunga, Rostam Aziz kung'atuka.
Wengine wanaotuhumiwa kwa vitendo hivyo walipewa muda hadi mwezi ujao kuamua mwenyewe kufuata mkumbo wa Rostam au wang'olewe kwa nguvu.

Wasomi CCM, wamlilia Kikwete avunje ukimya kwa yanayoendelea nchini



RAIS wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzaania, Dk Jakaya Kikwete ametakiwa kutekeleza kwa vitendo dhana ya uwajibikaji kwa kuwatimua kazi mawaziri ambao wizara zao zimekumbwa na kashfa ikiwemo wa Nishari na Madini na ile ya Maliasili na Utalii.
Aidha serikali imeombwa kuchukua hatua ya haraka katika kutatua matatizo yaliyopo katika sekta ya elimu ikiwemo suala la kutimuliwa kwa wahadhiri na kusimamishwa kwa wanafunzi wa vyuo vikuu vya Dodoma, UDOM, taasisi ya IMTU na Chuo cha Ustawi wa Jamii.
Wito huo umetolewa na Shirikisho la Wana-CCM Vyuo vya Elimu ya Juu mkoa wa Dar es Salaam, katika mkutano wa viongozi wake na waandishi wa habari uliofanyika juzi jijini humo.
Mwenyekiti wa Shirikisho hilo, Lusekelo Mwandemange, alisema bila Rais Kikwete kufanya maamuzi magumu katika utekelezaji wa vitendo dhana ya uwajibikaji ni wazi serikali yake itaendelea kupoteza sifa mbele ya wananchi.
Mwandemange alisema kwa kuwa dhana ya uwajibikaji ipo ndani ya CCM tangu enzi za Hayati Baba wa Taifa, Mwl Nyerere, katika kulinda maadili ya viongozi ni vema Rais Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM Taifa akatekeleza kwa kuwawajibisha baadhi ya watendaji wake.
Mwenyekiti huyo alisema kwa kashfa zilizoikumba wizara za Nishati na Madini na ya Maliasili na Utalii za kusimamishwa baadhi ya watendaji wake haipaswi kuachwa kwa wahusika tu bila mawaziri wanaoziongoza wizara hizo kuwajibishwa kwa yaliyotokea.
Mwandemange alisema ni vigumu wananchi kuielewa serikali kama watu waliovurunda mambo serikalini wakapewa likizo za malipo na kurejeshwa kinyemela kwa bashasha kama mashujaa, wakati wanafunzi wanaosimama kutetea haki zao wakitimuliwa vyuoni bila huruma yoyote.
"Tunamuomba Mwenyekiti wetu wa CCM ambaye ndiye Rais wa Jamhuri, afumbe macho na kuwapiga chini (kuwaondoa) viongozi wote dhaifu serikalini, bila kufanya hivyo hatutaweza kurudisha taswira nzuri ya serikali na chama mbela ya wananchi," alisema Mwandemange.
Aliongeza pia kwa kulipongeza Bunge la Jamhuri kwa uamuzi wa kuunda Tume ya

kuchunguza upya sakata la katibu wa wizara ya Nishati na Madini, akiiomba Tume hiyo isiishie kwa David Jairo, bali iimulike wizara nzima pamoja na wizara nyingine za serikali zilivurunda.
"Tume hiyo ichunguze kashfa ya wizara ya Maliasili na Utalii ambayo waziri wake, Ezekiel Maige aliwasimamisha watendaji wake akiwemo Mkurugenzi wa Idara ya Wanyama Pori nchini, Obed Mbangwa bila mwenyewe kuwajibika kwa hilo," alisema.
"Kwa hili tunashangaa waziri anaendelea kukalia kiti kwa kuwasimamisha kazi watendaji wake kwa staili ile ile ya Jairo, alikuwa wapi siku zote hadi wabunge walipofichua, lazima naye awajibike, ndio maaana tunamkata Rais avunje ukimya kwa kuwajibisha wahusika," aliongeza.
Shirikisho hilo liligusia matatizo ya sekta ya elimu yaliyopo katika baadhi ya vyuo vikuu nchini kwa kuitaka serikali ichukue hatua za haraka kuyatatua, licha ya kuipongeza kwa uamuzi wa kuongeza posho za wanavyuo kutoka Sh 5,000 hadi kuwa Sh 7,000.
Uongozi wa shirikisho hilo kupiotia taarifa yao iliyosainiwa na Katibu Mkuu wao, Asenga Abubakar, umesema hawakubaliani na maamuzi ya fedha za mikopo kupelekwa moja kwa moja vyuoni badala ya Bodi ya Mikopo kama zamani wakidai itazidisha matatizo.
Pia waliiomba serikali kuwarejesha wanafunzi na wahadhiri walitimuliwa na kusimamishwa vyuo vya Chuo cha Ustawi wa Jamii, taasisi ya IMTU na UDOM, wakidai kinachofanywa dhidi yao ni uonevu aliodai kama shirikisho hawaridhiki nayo.