STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, August 27, 2011

Sekretarieti ya CCM yashtukiwa, ila Nape mmmh!



WASOMI wa Vyuo vya Elimu ya Juu wanaokiunga mkono chama tawala, CCM, wamemtaka Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye asitishwe na kauli za watu wachache katika kuendeleza moto aliouanza dhidi ya vigogo wanaoatakiwa kujivua gamba wakiapa kumuunga mkono kwa hali yoyote.
Kadhalika wanachama wa CCM hasa vijana wajipange na kujitokeza kwa wingi kuwania nafasi za uongozi ndani ya Jumuiya ya chama hicho, ili kuleta mabadiliko yatakairejeshea heshima chama hicho mbele ya wananchi.
Katibu wa Shirikisho la Wana-CCM Vyuo vya Elimu ya Juu mkoa wa Dar es salaam, Asenga Abubakar, alitoa kauli hizo juzi kupitia taarifa aliyoitoa kwa vyombo vya habari akizungumzia kufifia kwa moto ulioanzishwa na Sekratarieti ya chama chao.
Abubakar, alisema moto ulioanzishwa na sekretarieti ya chama hicho chini ya Katibu Mkuu, Wilson Mukama, ni kama imefifia na hasa zile kelele zilizokuwa zikitolewa na Nape Nnauye, wakidai huenda zimetokana na vitisho vinavyotolewa dhidi yao.
Hata hivyo shirikisho hilo lilimtaka Nnauye, kutohofia vitisho hivyo na badala yake aendeleze moto zaidi ili kuhakikisha chama cgao kinasimama imara dhidi ya wachache wanaoutolea macho nafasi ya Urais kwa Uchaguzi Mkuu ujao wa mwaka 2015.
"Tunamuomba asitishwe na wanaoutolea macho uraisi wa 2015 na wafuasi wao, sisi tunamuonga mkono na tupo pamoja nae dhidi ya wachache hao wenye njaa," taarifa hiyo ya Abubakar inasomeka hivyo.
Taarifa hiyo ya Abubakar, licha ya kuihimiza sekretarieti hiyo kusimama imara, pia imewaomba na kuwataka wanachama wa CCM waliopo vyuoni na vijana kwa ujumla kujitokeza kwa wingi kuwania nafsi katika uchaguzi mkuu wa chama hjicho utakaofanyika mwakani, ili kuleta mabadiliko mbele ya umma wa Watanzania.
Kadhalika shirikisho hilo limesisitiza kwa kuwataka vijana wasiamini kwamba ndani ya CCM kuna ufisadi, bali wafuasi wachache wa chama hicho ndio wenye vitendo hivyo na hivyo wakijitokeza kushiriki uchaguzi watasaidia kurahisisha dhana ya kujivua gamba na kukifanya CCM kiwe makini nchini.
Kwa muda mrefu ndani ya CCM kumekuwa na msigano wa shinikizo la kuwataka baadhi ya wanachama wao wanaotuhumiwa kwa vitendo vya ufisadi kujivua gamba, kitu kilichomlazimisha aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Igunga, Rostam Aziz kung'atuka.
Wengine wanaotuhumiwa kwa vitendo hivyo walipewa muda hadi mwezi ujao kuamua mwenyewe kufuata mkumbo wa Rostam au wang'olewe kwa nguvu.

No comments:

Post a Comment