STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, August 27, 2011

Ubalozi watumia Dola 80,000 kufuturisha waislam Tz




UBALOZI wa Nchi ya Falme za Kiarabu, UAE nchini kupitia taasisi ya kutoa huduma za kijamii ya Khalifa Bin Zaayid Al Nahyaan, umekuwa ukitumia Dola za Kimarekani 80,000 kila mwaka kufutisha waumini wa kiislam waliopo jijini Dar na mikoa mingine.
Taarifa hiyo ilitolewa juzi na Mhasibu wa Ubalozi huo, Abdallah Ahmedna, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kwa niaba ya Balozi wa UAE, Sheikh Mallalla Mubarak Al Ameri wakati wa kuwaturusiha waumini wa msikiti wa Anwar, Msasani.
Ahmedna, alisema fedha hizo zimekuwa zikitolewa karibu mwaka wa nne sasa na ubalozi wao kwa ajili ya kuwafuturisha na kuwasaidia waumini wa misikiti 10 iliyopo mikoa ya Dar es Salaam, Morogoro, Lindi, Mwanza, Tanga, Pwani na Mtwara.
Alisema, msaada huo wa futari, daku na fedha kwa wasiojiweza hutolewa kwa muda wa mwezi mzima wa mfungo wa mwezi wa Ramadhani kila mwaka, ambapo kwa Dar mbali na msikiti wa Anwar mwingine unaonufaika ni Al Rahman, uliopo Kinondoni.
"Kama waislam tumekuwa tukithamini waumini wa Tanzania kwa kuwafuturisha pamoja na kuwapa misaada, ambapo ubalozi umekuwa ukifadhili misaada hiyo kwa kiasi cha Dola za Kimarekani 80,000 kwa kila mwaka," alisema.
Baadhi ya waumini waliofuturishwa msikiti hapo waliushukuru ubalozi huo na kuomba watu wengine wenye uwezo kuiga mfano huo wakidai mwezi huu ndio wa waumini wa kweli kuonyesha upendo, ukarimu na kuhurumiana katika kutekeleza nguzo ya nne kati ya tano za Imani za Kiislam.

Mwisho

No comments:

Post a Comment