STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, August 27, 2011

Kaseba, Oswald kuzipiga Okt Mosi




BINGWA wa zamani wa ngumi za kulipwa nchini, Ernest Bujiku na Chaurembo Palasa ni kati ya mabondia watakaopanda ulingoni kusindikiza pambano la mkongwe Maneno Oswald na Japhet Kaseba litakalofanyika Oktoba Mosi.
Pambano hilo la raundi 10 lisilo la ubingwa la uzani wa kilo 72 la Kaseba na Oswald maarufu kama Mtambo wa Gombo litafanyikia kwenye ukumbi wa hoteli ya Travertine Magomeni likisimamiwa na Shirikisho la Ngumi za Kulipwa nchini, PST, chini ya uratibu wa promota, Gervas Muganda wa kampuni ya Babyface ya jijini Dar.
Akizungumza na Micharazo jana, Kaseba, alisema kabla ya yeye kupigana na Oswald watasindikizwa na michezo kadhaa akiyataja baadhi likiwakutanisha Chaurembo Palasa dhidi ya Sweet Kalulu, Ernest Bujiku atakayepigana na Mbukile Chuwa.
Kaseba alisema pia siku hiyo Venance Mponji atapanda ulingoni kuzipiga na Jafar Majiha 'Mr Nice' na kutakuwa na michezo miwili ya kick boxing ambapo Ramadhani Mshana atapigana na Hamed Said na jingine la wapiganaji chipukizi.
Mkali huyo alisema amekuwa akiendelea kujifua vema ili kuweza kukkabili Oswald aliyekiri ni mmoja wa mabondia bora na wenye uwezo mkubwa katika mchezo huo.
"Naendelea kujifua kwa lengo la kutaka kumshinda Oswald ambaye namheshimu kwa umahiri wake katika mchezo wa ngumi, naamini nikizembea anaweza kunitoa nishai," alisema Kaseba.
Katika hatua nyingine, bondia Stan Kessy anatarajiwa kupanda ulingoni Septemba 25 kupigana katika pambano lisilo la ubingwa dhidi ya Seleman Habib, ambalo litasindikizwa na michezo mitano tofauti ya utangulizi.
Mratibu wa pambano hilo litakalofanyikia kwenye ukumbi wa Friend's Rangers jijini Dar es Salaam, Dk John Magambo, alisema Kessy na Habib watapigana kwenye uzani wa middle raundi 10 na kusindikizwa na mabondia wengine.
Dk Magambo aliwataja watakaowasindikiza wawili hao ni Salehe Mkalekwa atayaepigana na Jafari Majiha, Doto KIpacha dhidi ya Jones Godfrey, Yohana Thobias atayepigana na Huseni Mashaka na Omar Rajab dhidi ya Husseni Mandula.

Mwisho

No comments:

Post a Comment