STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, August 27, 2011

Mnanda wamtoa Ferouz wa Daz Nundaz


MSANII nyota wa muziki wa kizazi kipya nchini, Feruzi Mrisho 'Ferouz' aliye mbioni kuachia kazi yake mpya iitwayo 'Ndege Mtini', amedai kibao hicho alichokiimba katika miondoko ya Mchiriku utamrejesha kwenye chati yake ya zamani.
Ferouz aliyekuwa kimya karibu miaka mitatu iliyopita, alisema aliamua kuimba kibao hicho kipya alichomshirikisha chipukizi wa THT, Shoz Dia, miondoko ya 'mnanda' ili kurudi upya.
"Nimeamua kutoa upya na mnanda kwa nia ya kurejesha makali yangu, pia kuonyesha utoauti wa Ferouz wa Das Nundaz au wa 'Starehe' na huyu wa sasa," alisema.
Mkali huyo aliyetamba na vibao kadhaa kikiwemo hicho cha Starehe alichoimba na Profesa Jay, alisema kibao hicho cha Niwqe Nawe anachojiandaa kukifyatulia video yake, ni utangulizi wa ujio wa albamu yake mpya itakayofahamika kwa jina la 'Reserve'.
Aliongeza ndani ya albamu hiyo atakayowashirikisha wasanii kadhaa nyota akiwemo mshindi wa Tuzo Tano za Kili Music Awards-2011, 20 Percent itakuwa na nyimbo nane.
Feropuz alizitaja nyimbo hizo kuwa ni pamoja na Ndege Mtini, Nimemfukuza, 'Reserve' na Tusifuatane.
Hiyo itakuwa ni albamu ya tatu kwa mkali huyo kwani baada ya kutoa albamu ya 'Safari' mwaka 2004 iliyokuwa na wimbo wa Starehe, alifyatua nyingine ya pili iitwayo Sauti Nyimbo na Vyombo iliyokuwa na wimbo wa 'Mr Policeman, kabla ya kutoweka hadi alipobuka juzi.

Mwisho.

No comments:

Post a Comment