STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, March 7, 2015

Real Madrid yazmishwa ugenini, Sevilla yaua

Karim Benzema (left) and Cristiano Ronaldo look on as the Bilbao team celebrate scoring in the first half
HAWAAMINI KAMA WAMETUNGULIWA!
Bilbao striker Inaki Williams (second left) tries to keep the ball away from the approaching Madrid player Asier Illaremendi 
Hata Bale alishindwa kuibeba Real Madrid leo kwa Athletic Bilbao
KLABU ya Real Madrid imechezea kichapo cha bao 1-0 ugenini mbele ya Athletic Bilbao katika mfululizo wa Ligi Kuu ya Hispania (La Liga) huku Sevilla wakishinda ugenini mabao 4-3 dhidi ya Deportivo la Coruna.
Bao pekee lililowazamisha Mabingwa wa Ulaya, liliwekwa kimiani kwa kichwa na Aduriz katika dakika ya 26 akimalizia kazi nzuri ya Mikel Rico.
Madrid ilikuwa na wakali wake wote akiwamo Cristiano Ronaldo, Gareth Bale, Karim Benzema, Isco, Ton Kroos na wengine ilishindwa kabisa kufuruka kwa wenyeji na kukubali kichapo hicho kilichowafanya wasaliwe na pointi zao 61 na kutoa nafasi kwa wapinzani wao wakuu Barcelona kuwapiku kama watashinda katika mechi yao ya kesho. Barcelona wana pointi 59,wakiwa wana mchezo mmoja pungufu zaidi ya Real Madrid.
Katika mchezo mwingine wa mapema, Deportivo la Coruna wakiwa nyumbani walizamishwa mabao 4-3 na Sevilla, huku kwa sasa pambano la ligi hiyo Elche ikiwa nyumbani inaongoza bao 1-0 dhidi ya Almeria na baadae Granada itaikaribisha Malaga.

Taifa Stars kuvaana na Malawi Machi 29

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEib4Geg2HzkrM8BDCTZpyd28JL_3avjxBBFaqs6CZXbhBFNXd34kYVHku38wroT3X297kNVt2VCkmx9rSLIMggDqH4wRuJ5ATjbIOGZ4lQ8txrgyljcmrIChSqjATeLt9tVQ0kvzxrFiQvm/s1600/Taifa+Stars+group+picture.JPG
Taifa Stars itakayovaana na Malawi katika pambano linalotambuliwa na FIFA
TIMU ya soka ya taifa, Taifa Stars inatarajiwa kushuka dimbani Jumapili ya Machi 29 mwaka huu, kucheza mchezo wa kirafiki na timu ya taifa ya Malawi, The Flames.
Pambano hilo litachezwa kwenye uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.
Mchezo huo wa kirafiki ambao upo katika kalenda ya FIFA kwa timu za Taifa (Machi 23-31) na utatarajiwa kuanza majira ya saa 10 na nusu jioni kwa saa za Afrika Mashariki.

Wawili waumia Twiga Stars ikijianda kuvaana na Zambia

WACHEZAJI wawili wa timu ya Taifa ya wanawake, Twiga Stars, wameshindwa kufanya mazoezi kutokana na kuwa majeruhi kwenye Uwanja wa Karume, Ilala jijini Dar es Salaam

Wachezaji ambao ni majeruhi ni Fatuma Khatib anayecheza beki ya kulia na Ziada Ramadhani beki wa kushoto na waliumia kwenye mchezo wa kirafiki wa timu hiyo dhidi ya timu ya makipa ikiwa ni maandalizi ya mchezo wa kufuzu Kombe la Mataifa Afrika dhidi ya Zambia Machi 22, mwaka huu.

Akizungumzia hali zao kocha wa Twiga Stars, Rogasian Kaijage alisema kuwa wachezaji hao wanaendelea na matibabu na anatarajia wiki ijayo watakuwa wamepona.

“Leo hawakufanya mazoezi kwa sababu wana maumivu, lakini natarajia mapema wiki ijayo watakuwa wamepona kwani wanaendelea vizuri na matibabu”, alisema Kaijage

Kaijage alisema kutokana na program ya mazoezi aliyoendesha tangu timu hiyo ianze kambi mwishoni mwa mwezi uliopita anatarajiwa kuwa na mchezo mmoja wa kujipima nguvu katikati ya mwezi huu.

Twiga Stars ambayo imeweka kambi katika Hosteli za Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) zilizopo ndani ya Uwanja wa Karume, Ilala, Dar es Salaam imeingia moja kwa moja katika hatua ya pili kucheza na Zambia kufuatia kuwa na matokeo mazuri katika msimamo wa viwango vya soka la wanawake barani Afrika.

Wachezaji waliopo kwenye kikosi cha Twiga ni Asha Rashid, Esther Chaburuma, Fatuma Bushiri, Fatuma Hassan, Fatuma Mustapha, Fatuma Omari, Eto Mlenzi, Mwajuma Abdallah, Sofia Mwasikili, Zena Khamis, Mwanahamisi Omar, Fadhila Hamad, Anastazia Anthony na Shelder Boniface.

Wengine ni Thereza Yonna, Happines Hezron, Amina Ally, Donizia Daniel, Fatuma Issa, Vumilia Maarifa, Maimuna Hamisi, Najiati Abbas, Stumai Abdallah, Zuwena Aziz, Irene Joseph, Dawa Haji Vuai, Belina Julius na Amina Ramadhani.

Spurs yailipua QPR kwao yaipumulia Liverpool

.
Muunganiko wa picha zilizochapishwa na Daily Mail zikionyesha mpambano wa Spurs na QPR ulivyokuwa leo
MSHAMBULIAJI Harry Kane amefunga mabao mawili jioni ya leo na kuiwezesha timu yake ya Tottenham Hotspur kupata ushindi muhimu ugenini dhidi ya QPR katika mechi ya kiporo cha Ligi Kuu ya England.
Kane ambaye amekuwa moto wa kuotea mbali alifunga mabao hayo katika kila kipindi na kuifanya Spurs kufikisha pointi 50 na kupaa hadi nafasi ya sita nyuma ya Liverpool iliwatanguliwa kwa pointi 51.
Mshambuliaji huyo kinda alifunga bao la kwanza dakika ya 34 kabla ya kuongeza la pili dakika ya 68 na wenyeji wanaopambana kuepuka kushuka daraja ilip[ata bao la kufutia machozi kupitia Sandro katika dakika ya 75.

Jonny Evance, Papiss Cisse wafungiwa England

http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2015/03/06/2652640E00000578-2983103-Evans_left_and_Cisse_clash_near_the_half_way_line_at_St_James_Pa-a-1_1425663667950.jpgBEKI wa Manchester United, Jonny Evance na Mshambuliaji wa Newcastle United, Papiss Cisse, wamefungiwa kwa kitendo chao cha kutemeana mate katika pambano lililochezwa majuzi.
FA iliwafungulia mashtaka wachezaji hao baada ya awali mwamuzi wa pambano hilo kutoliona tukio halisi ya wachezaji hao kujigeuza 'nyota'kwa kutemeana mate.
Evance aliyekanusha shtaka lake amefungiwa mechi sita wakati mwenzake amefungiwa mechi saba ikiwamo sita ya kosa hilo na moja kwa kosa alililowahi kulifanya hivi karibuni la kumpiga mtu kiwiko.
Awali Cisse alikubali  mashitaka yaliyotolewa na Chama cha Soka cha Uingereza-FA kwa kumtemea mate beki wa Manchester United Jonny Evans.
Nyota huyo mwenye umri wa miaka 29, aliomba radhi kutokana na tukio hilo lakini amekanusha kama alifanya kwa makusudi.

Kiingilio Simba, Yanga Buku 7 tiketi zaanza kuuzwa

Yanga
Simba
TIKETI za pambano la kesho kati ya Simba SC na Young African litakaofanyika kwenye dimba la Uwanja wa Taifa kuanzia majira ya saa 10 kamili za jioni zimeanza kuuzwa kama ilivyotangazwa na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).
Mchezo huo wa kesho utachezeshwa na mwamuzi Martin Saanya kutoka Morogoro, akisaidiwa na Soud Lila (DSM) mshika kibendera wa kwanza, Florentina Zabron (Dodoma) mshika kibendera wa pili, Mwamuzi wa akiba Israel Mjuni (DSM), na kamisaa wa mchezo ni Ame Santimeya (DSM).
Viingilio vya mchezo huo, VIP A sh. 40,000, VIP B sh. 30,000, VIP C sh. 20,000, Rangi ya Machungwa (Orange) sh. 10,000, huku Rangi ya Bluu na Kijani ikiwa ni sh. 7,000.
Tiketi zimeanza kuuzwa leo Jumamosi saa 2 kamili asubuhi katika vituo vya, Karume (Ofisi za TFF), Mgahawa wa Steers (Posta Mpya), Oilcom (Buguruni), BigBon (Kariakoo), Olicom (Ubungo), Dar Live (Mbagala), Uwanja wa Uhuru, Kivukoni (Ferry) na Makumbusho (kituo cha mabasi).
Magari yenye vibali maalum ndiyo yatakayoruhusiwa kuingia ndani ya uwanja kesho Jumapili kwa kupitia barabara ya Mandela na Uwanja wa Uhuru, barabara ya Chang'ombe itafungwa kuanzia saa 12 kamili asubuhi.
TFF inawaomba, wapenzi, washabiki na wadau wa mchezo kununua tiketi katika vituo vilivyotajwa ili kuepuka kuuziwa tiketi bandia, ili kuimarisha ulinzi na usalama wa mchezo, mashabiki wenye mabegi, silaha, vilevi na chupa za maji hawataruhusiwa kuingia navyo uwanjani.
Aidha katika mchezo huo TFF itatoa ujumbe maalum kupitia kwa wachezaji kuhamasisha juhudi za Taifa za kuzuia mauaji dhidi ya watu wenye ulemavu wa ngozi (Albino)

Azam yalipa kisasi JKT , Coastal yabanwa Tanga

Mfungaji wa bao pekee la Azam

BAO pekee kutoka kwa Mrundi, Didier Kavumbagu limeiwezesha mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara kulipa kisasi kwa JKT Ruvu.
Azam walipata ushindi huo kwenye uwanja wa Chamazi na kuifanya timu hiyo kuzidi kuwapumulia Yanga waliopo kileleni ambao kesho watashuka dimbani kuvaana na Simba.
Kavumbagu alifunga bao hilo lililokuwa la tisa kwake msimu huu katika ligi hiyo katika dakika ya 17 akiunganisha mpira wa krosi ya beki Shomari Kapombe na yeye kuufungwa kwa kichwa.
Azam imefikisha pointi 30, moja pungufu na ilizonazo Yanga yenye 31 ambao kesho watakuwa vitani dhidi ya Simba kwenye uwanja wa Taifa/ Kati mechi ya mkondo wa kwanza JKT Ruvu ndiyo iliyokuwa timu ya kwanzsa iliyovunja rekodi ya Azam ya kushinda mechi mfululizo 38 baada ya kuichapa bao 1-0.
Katika mchezo mwingine uliochezwa leo mabingwa wa zamani wa soka nchini, Coastal Union kwenye uwanja wao wa nyumbani wa Mkwakwani Tanga walilazimishwa sare ya mabao 2-2 na Kagera Sugar.
Mabao ya Coastal yalifungwa na Seleman Kibuta na Rama Salim wakati wageni walipata mabao yake kupitia kwa Atupele Green na Enock Kyaruzi.
Pambano jingine kati ya Polisi Moro dhidi ya Ruvu Shooting limeshindwa kufanyika mpaka siku ya Jumanne kutokana nna uwanja wa Jamhuri Morogoro kutumika na shughuli za sherehe za Siku ya Wanawake inayofikia kilele kesho Jumapili.