STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, March 7, 2015

Real Madrid yazmishwa ugenini, Sevilla yaua

Karim Benzema (left) and Cristiano Ronaldo look on as the Bilbao team celebrate scoring in the first half
HAWAAMINI KAMA WAMETUNGULIWA!
Bilbao striker Inaki Williams (second left) tries to keep the ball away from the approaching Madrid player Asier Illaremendi 
Hata Bale alishindwa kuibeba Real Madrid leo kwa Athletic Bilbao
KLABU ya Real Madrid imechezea kichapo cha bao 1-0 ugenini mbele ya Athletic Bilbao katika mfululizo wa Ligi Kuu ya Hispania (La Liga) huku Sevilla wakishinda ugenini mabao 4-3 dhidi ya Deportivo la Coruna.
Bao pekee lililowazamisha Mabingwa wa Ulaya, liliwekwa kimiani kwa kichwa na Aduriz katika dakika ya 26 akimalizia kazi nzuri ya Mikel Rico.
Madrid ilikuwa na wakali wake wote akiwamo Cristiano Ronaldo, Gareth Bale, Karim Benzema, Isco, Ton Kroos na wengine ilishindwa kabisa kufuruka kwa wenyeji na kukubali kichapo hicho kilichowafanya wasaliwe na pointi zao 61 na kutoa nafasi kwa wapinzani wao wakuu Barcelona kuwapiku kama watashinda katika mechi yao ya kesho. Barcelona wana pointi 59,wakiwa wana mchezo mmoja pungufu zaidi ya Real Madrid.
Katika mchezo mwingine wa mapema, Deportivo la Coruna wakiwa nyumbani walizamishwa mabao 4-3 na Sevilla, huku kwa sasa pambano la ligi hiyo Elche ikiwa nyumbani inaongoza bao 1-0 dhidi ya Almeria na baadae Granada itaikaribisha Malaga.

No comments:

Post a Comment