STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, March 7, 2015

Jonny Evance, Papiss Cisse wafungiwa England

http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2015/03/06/2652640E00000578-2983103-Evans_left_and_Cisse_clash_near_the_half_way_line_at_St_James_Pa-a-1_1425663667950.jpgBEKI wa Manchester United, Jonny Evance na Mshambuliaji wa Newcastle United, Papiss Cisse, wamefungiwa kwa kitendo chao cha kutemeana mate katika pambano lililochezwa majuzi.
FA iliwafungulia mashtaka wachezaji hao baada ya awali mwamuzi wa pambano hilo kutoliona tukio halisi ya wachezaji hao kujigeuza 'nyota'kwa kutemeana mate.
Evance aliyekanusha shtaka lake amefungiwa mechi sita wakati mwenzake amefungiwa mechi saba ikiwamo sita ya kosa hilo na moja kwa kosa alililowahi kulifanya hivi karibuni la kumpiga mtu kiwiko.
Awali Cisse alikubali  mashitaka yaliyotolewa na Chama cha Soka cha Uingereza-FA kwa kumtemea mate beki wa Manchester United Jonny Evans.
Nyota huyo mwenye umri wa miaka 29, aliomba radhi kutokana na tukio hilo lakini amekanusha kama alifanya kwa makusudi.

No comments:

Post a Comment