STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, August 22, 2014

Mtibwa Sugar, Polisi Moro kupimana ubavu kesho Morogoro

Polisi Moro
Mtibwa Sugar
TIMU za Mtibwa Sugar na Polisi Morogoro zinazojiandaa kushiriki ligi kuu ya Vodacom (VPL) zinatarajia kucheza kesho Jumamosi mechi ya majaribio ya mfumo wa tiketi za elektroniki.
Mechi hiyo itafanyika katika uwanja wa Jamhuri uliopo mjini Morogoro kuanzia saa 10 kwa kiingilio cha sh 1,000.
kwa mujibu wa taarifa iliotolewa na Afisa habari wa Shirikisho la soka nchini TFF Boniface Wambura alisema tiketi za mechi hiyo zitaanza kuuzwa leo kupitia mtandao wa M-Pesa, CRDB Simbanking na maduka 30 ya Fahari Huduma yaliyopo katika wilaya zote za Mkoa wa Morogoro.
Alisema mashabiki 100 wa kwanza watakaoanza kuingia uwanjani wapata jezi za timu ya Mtibwa Sugar na Polisi Morogoro.
Aliongeza kusema kusema tayari mechi ya majaribio ya tiketi za elektroniki imeshafanyika katika uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya ambapo timu za Tanzania Prisons na Mbeya City zilichuana na kutoka sare.
Alisema mechi nyingine za majaribio ya tiketi za elektroniki zinatarajiwa kuchezwa Agosti 30 mwaka huu.
Alisema katika uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga kutakuwa na mechi kati ya Coastal Union na Mgambo Shooting wakati katika Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba ni Kagera Sugar dhidi ya mabingwa wa Mkoa wa Kagera, Eleven Stars.
Wambura alisema Septemba 6 mwaka huu katika Uwanja wa Taifa kutakuwa na mechi kati ya Simba na Mtibwa Sugar.
Alisema mchezo wa ngao ya Jamii utakaozikutanisha timu ya Azam FC na Yanga afrika umepangwa kufanyika Septemba 13 katika Uwanja wa Taifa,uliopo jijini Dar es Salaam.
Mtibwa inatarajiwa kuanza ligi kwa kuikaribisha Yanga kwenye uwanja wa Jamhuri wakati Polisi Moro itakaribishwa tena katika ligi kwa kuumana na Azam kwenye uwanja wa Chamazi Septemba 20.
Wakati huo huo waamuzi wanaotarajia kuchezesha mechi za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) na Ligi Daraja la Kwanza (FDL) msimu huu watafanya mtihani wa utimamu wa mwili (physical fitness test) mwezi ujao.
Mtihani huo utahusisha waamuzi wa daraja la kwanza (class one) wakiwemo wale wenye beji za Shirikisho la Kimataifa la soka duniani (FIFA).
Alisema mbali ya mtihani huo unaotarajiwa kufanyika kabla ya Septemba 10 mwaka huu, kutakuwa na semina ya makamishna ambao watasimamia mechi za VPL na FDL.
Alisema waamuzi wote wanatakiwa kutumia muda uliobaki kufanya maandalizi kwa ajili ya mtihani huo.

Majanga yaanza mapema Arsenal, Arteta kuikosa Everton kesho

http://worldsoccertalk.com/wp-content/uploads/2013/08/mikel-arteta.jpg
MAJANGA yamezidi kuiandama Arsenal baada ya kiungo mkabaji wao, Mikel Arteta naye kuelekea chumba cha majeruhi kwa mechi mbili baada ya Jumanne kuumia kifundo cha mguu 'ankle' kwenye mechi ya kuwania kufuzu hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Besiktas ya Uturuki.
Nahodha huyo wa Arsenal alitolewa nje katika dakika ya 50 kwenye Uwanja wa Olympic Ataturk baada ya kuumia wakati akiwania mpira dhidi ya mshambuliaji wa zamani wa Chelsea Demba Ba.
Arsenal pia itamkosa Aaron Ramsey baada ya kutolewa nje kwa kadi mbili za njano katika kipindi cha pili kwenye mechi hiyo ya Uefa.
Arteta sasa ataikosa mechi ya Ligi Kuu England Jumamosi ugenini dhidi ya Everton pamoja na ile ya marudiano ya kuwania kufuzu hatua ya makundi Ligi ya Mabingwa Ulaya  dhidi ya Besiktas itakayopigwa Jumatano kwenye Uwanja wa Emirates.
Jana alitarajiwa kufanyiwa uchunguzi zaidi lakini ni wazi kabla ya hapo alishaelezwa kuzikosa mechi mbili zijazo.
Chumba cha majeruhi cha Arsenal tayari kimeanza kupokea wagonjwa baada ya Yaya Sanogo na Kieran Gibbs kuwa majeruhi na kuikosa mechi dhidi ya Besiktas ambayo walitoka sare tasa huko Istanbul.
Haitakuwa rahisi kwa Arsenal katika mechi hiyo ya marudiano dhidi ya Besiktas, na zaidi kutokana na kuwakosa Aaron Ramsey na Mikel Arteta, lakini haijawahi kutolewa katika mechi hizo za mchujo za Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Hata hivyo, Mesut Ozil, Per Mertesacker na Lukas Poldolski watakuwamo kwenye kikosi cha Arsenal jambo ambalo linamshawishi kiungo Jack Wilshere kwamba wataonesha tofauti kubwa.

Mshale wa Kifo wa Aisha Bui kutua sokoni Jumatatu

Kava la filamu mpya ya Aisha Bui iitwayo Mshale wa Kifo
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEinKiqzE2w-eoq8Y64WwU4ZrnrOpEBY3rF9-JIHsWMyNIf_X71G0wRs19pIRow8wwoml3cw3a2Vgje7Xo51CRC80y7Or770GCzJtsXbaHvyUmxdo9otrN4sbk6S00Pe4EPzQ5I6P9EuIFk/s1600/10482228_800152790017429_125002049025336857_n.jpg
Aisha Bui katika pozi
FILAMU mpya ya muigizaji nyota wa filamu nchini, Aisha Fat'hi 'Aisha Bui' iitwayo 'Mshale wa Kifo' inatarajiwa kuingia sokoni siku ya Jumatatu, huku mwanadada huyo akitamba kuwa kazi hiyo ni mwanzo wa uhondo kutoka kampuni yake ya Bad Girl Film's.
Akizungumza na MICHARAZO, Aisha Bui alisema filamu hiyo aliyoigiza na wakali kama Mzee Chilo, Gabo wa Zagamba na wengine itaingia sokoni Agosti 25, huku kampuni yake ya bad Girl ikijipanga kuandaa kazi nyingine kali zaidi na hiyo.
Aisha Bui, alisema japo filamu hiyo ni kazi yake ya kwanza kuiandaa, lakini kwa jinsi ilivyoandaliwa kwa umakini mkubwa ni wazi mashabiki watajua ujio wake mpya siyo wa kubahatisha.
"Naiachia filamu yangu Jumatatu, nawaomba mashabiki waniunge mkono kwa kununua nakala halisi, ili kuiwezesha kampuni ya Bad Girl kuendelea kuwapa uhondo zaidi, kuna makubwa yapo njiani kutoka kwangu," alitamba Aisha Bui.
Nyota huyo aliyecheza filamu mbalimbali ikiwamo ya Saturday Morning, Better Days, Not Without My Son, Continous Love, Revenge of Love, Mirathi, Pain of Love, Crazy Love na The Second Wife, alisema ndani ya filamu hiyo mpya inasimulia kisa cha mfanyabiashara wa dawa za kulevya ambaye anamlazimisha askari Polisi kumsaidia kupitisha mzigo wake.
Hata hivyo kazi haiwi rahisi na kuibua kashkash kwa binti wa askari huyo Myrine nafasi iliyochezwa na Aisha kufanywa kama chambo.
"Ni simulizi linalosisimua na kutia simanzi na bahati nzuri walioiigiza kuanzia mimi mwenyewe, Gabo, Mzee Chilo na wengine tumeitendea haki," alisema Aisha.

Liverpool yarudi kumwania 'mtukutu' Mario Balotelli

Balotelli enzi akiwa Manchester City
KLABU ya Liverpool wametangaza kukubali kuilipa AC Milan ada ya uhamisho ya paundi milioni 16 ili kuinasa saini ya mshambiliaji wa Italia, Mario Balotelli.
Mwezi uliopita, Brendan Rodgers alisema Liverpool haiwezi kumsajili Balotelli, lakini amebadili moyo wake.
Mapema leo Balotelli aliwaambia Sky Italia: “Leo itakuwa siku yangu ya mwisho Milanello.”
Nyota huyo kurudi England kutateka hisia za mashabiki wengi wa soka wakikumbuka vituko vyake akiwa Manchester City kabla ya kuondoka mwaka 2013.
Balotelli amejihusisha na matukio mengi ya utovu wa nidhamu hususani wakati akicheza ligi kuu England
Ndani ya uwanja, alioneshwa kadi nyekundu wakati Man City ilipochuana na Asernal mwaka 2012 na kufungwa.
Nje ya uwanja, alikuwa na matukio ya mengi ya ukutuku.
Moja ya tukio la kukumbukwa pia ni kitendo chake cha kuonesha fulana iliyoandikwa ‘Why Always Me?’ alipofunga goli kwenye mechi ya mahasimu wa Manchester ndani ya dimba la Old Trafford mwaka 2011.
Pia aliingia katika mgogoro na kocha wa City wakati ule, Roberto Mancini ndani ya uwanja wa mazoezi na kukunjana.
Zaidi alimchapa kibao Jerome Boateng.
Tangu aliporudi nchini Italia amefunga mabao 30 katika mechi 54, idadi sawa na aliyofunga akiwa na City katika mechi 80.
Si rahisi kusahau kuwa nyota huyu tayari ameshinda makombe manne katika mataifa mawili, ubingwa ligi na kombe la FA na Coppa Italia akiwa na umri wa miaka 24.

Di Maria aomba kuondoka Real Madrid

http://talksport.com/sites/default/files/styles/large/public/field/image/201308/angel_di_maria.jpg?itok=gPwE_rnHCARLO Ancelotti amebainisha kwamba Angel Di Maria anataka kuondoka Real Madrid na kwamba wanaangalia mpango wa kulimaliza suala lake kabla dirisha la usajili halijafungwa.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Argentina amepoteza namba katika kikosi cha kwanza Madrid kufuatia kutua kwa James Rodriguez na Toni Kroos katika kipindi hiki cha usajili na amedhamiria kutafuta namba kwingineko.
Di Maria amekuwa akihusishwa sana na PSG na Manchester United katika miezi kadhaa iliyopita, lakini mabingwa hao wa Ligue 1 walisema hivi karibuni kuwa hawana mpango wa kumsajili winga huyo kutokana na sababu za kiuchumi, na hivyo kuiachia Man U nafasi kubwa ya kumpata.
"Ameniomba kuondoka katika kipindi hiki cha usajili. Amekataa ofa ya klabu ya kubaki Madrid, hivyo tunatafuta suluhisho," Ancelotti alisema kwenye mkutano na waandishi wa habari.
"Tutapata suluhisho kwa Di Maria kabla ya dirisha kufungwa, lakini kwa sasa anabaki kuwa mchezaji wa Madrid. tuko katika hali ambayo mchezaji anatakiwa kujitafutia klabu mwenyewe.
"Kama Di Maria atashindwa kupata suluhisho mwenyewe, atabaki hapa. Tunamkaribisha na anaweza kuendelea kufanya kazi hapa. hakuna shida."
Nyota huyo mwenye umri wa miaka 26, aliyejiunga na Madrid akitokea Benfica katika kipindi hiki cha uhamisho cha 2010, ana mkataba na Madrid hadi 2018, lakini anaweza kuuzwa kwa euro milioni 60.

Extra Bongo, Omar Tego kuwasindikiza Masai Safari Band

BENDI ya Extra Bongo 'Wazee wa Kizigo' wanatarajiwa kusindikiza uzinduzi wa albamu ya kwanza ya bendi ya Masai Safari utakaofanyika Agosti 30.
Uzinduzi wa albamu hiyo iitwayo 'Hakuna Kama Baba' utafanyika kwenye ukumbi wa Lunch Time na kwa mujibu wa Rais wa Masai Safari, Francis Mwaisela, Extra Bongo ni kati ya watakaowasindikiza siku hiyo.
Mwaisela alisema makundi mengine yatakayokuwapo ukumbini kuwapia tafu siku hiyo ni Coast Modern linaloongozwa na waimbaji ndugu, Omar na Maua Tego.
"Extra Bongo, Omar Tego na dada yake Maua Tego na wasanii wengine wa muziki wa kizazi kipya ndiyo watakaotusindikiza siku ya uzinduzi wa albamu yetu utakaofanyika Agosti 30," alisema Mwaisela.
Rais huyo wa Masai Band alizitaja nyimbo zilizopo katika albamu hiyo ni 'Hakuna Kama Baba', 'NJia Panda', 'Mikoni ni Kazi', 'Ndoa ni Mipango ya Mungu', 'Usiwasikilize Wambea,' na Kilio Changu'.
"Kwa sasa tupo kenye mazoezi makali kwa ajili ya uzinduzi huo ambao tumepania kuweka rekodi nchini," alisema Mwaisela

Tanzania All Stars watakawavaa Real Madrid kesho Taifa






Queen Darlin ageukia filamu, kuuza sura kwa Chekibudi



DADA wa nyota wa muziki wa kizazi kipya nchini, Diamond Platnumz, Mwajuma Abdul 'Queen Darling' anatarajiwa kuibuka kwenye anga za uigizaji baada ya kushirikishwa katika filamu iitwayo 'Kisebusebu'.
Filamu hiyo na muigizaji nyota nchini Nurdin Mohammed maarufu kama 'Chekibudi' imekamilishwa kurekodiwa hivi karibuni na inafanyiwa mchakato wa kuachiwa mwezi ujao.
Chekibudi aliiambia MICHARAZO kuwa, Queen Darling anayetamba na nyimbo kama 'Wajua Nakupenda', 'Maneno' na 'Wanatetemeka' pamoja na remix ya 'Nakomaa na Jiji', ameitendea haki filamu hiyo.
"Huwezi kuamini kama Queen Darling ni msanii wa muziki wa kizazi kipya kwa jinsi alivyotenda haki mbele ya kamera," alisema Chekibudi na kuongeza mbali na msanii huyio filamu hiyo pia ameiigiza yeye (Chekibudi), Tiko Hassan na wakali wengine.
Wasanii kadhaa wa bongofleva wamekuwa pia wakitamba katika Bongo Movie kama Snura, Shilole a.k.a Shishi Baby na Hemed Suleiman a.k.a PHD.

Babu Tale acharuka tuhuma za Diamond na Dawa za Kulevya

Diamond (kulia) akiwa na Meneja wake, Babu Tale na Aunty Ezekiel
BAADA ya chombo kimoja cha habari kuandika habari juu ya tuhuma za kujihusisha na dawa za kulevya kwa nyota wa muziki wa kizazi kipya nchini, Naseeb Abdul 'Diamond', Meneja wake Khamis Tale 'babu Tale' ameamua kufunguka na kuwachana walioandika habari hiyo kama anavyosomeka hapo chini;
"Tunalipwa milioni 20 show moja, tunalipwa dola elfu 25,000 show moja, hii ni zaidi ya madawa ya kulevya. “We get more money from music, sio kwenye madawa ya kulevya, hatufanyi hizo biashara na kama wanahisi sisi tunafanya tunawaruhusu watufanyie investigation hata kwa muda wa miaka kumi ina maana tunavyopita pale airport hawana vifaa vya kutuchunguza? Ipo wazi hata Global walishindwa kufanya kazi na sisi kwa sababu sisi ni wakubwa.
Sasa leo hii tunauza madawa ya kulevya kwa sababu tunakomaa kwenye bei zetu. “September tunafanya show kubwa ya Unplugged na msanii wa kwanza hapa kufanya ile show ni Diamond na ile show hawalipi hela ya kis**e.
Wataendelea kuona watu wanauza madawa ya kulevya, hakuna msanii wa Tanzania anayefanya show kwa walau dola elfu 10,000 ni Diamond peke yake wengine ni dola 2000, 2500 elfu 3,000 mwisho.
Tuna show Marekani show kumi na tano (15), show kumi na tano dola elfu ngapi? Na kwa hapa Tanzania hatufanyi show chini ya dola elfu 15,000.”