STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, March 18, 2014

Hawa ndiyo wanasoka, makocha waliovuna fedha nyingi 2013

ronmessi622302_346025aJarida linaloheshimika kwa kiasi katika ulimwengu wa soka duniani ‘France Football’ leo hii limechapishwa listi ya wachezaji na makocha 20 wanaolipwa fedha nyingi ndani ya msimu mmoja.
Mapato ya wanasoka hao yamejumuishwa kutoka kwenye mishahara yao, na mikataba mbalimbali waliyonayo ya kibishara pamoja na bonasi wanazopata. Listi ipo kama ifuatavyo.

WACHEZAJI WALIONGIZA FEDHA NYINGI MIEZI 12 ILIYOPITA
  1. Lionel Messi – €41m
  2. Cristiano Ronaldo – €39.5m
  3. Neymar – €29m
  4. Wayne Rooney – €24m
  5. Zlatan Ibrahimovic – €23.5m
  6. Radamel Falcao – €21.2m
  7. Sergio Aguero – €19.7m
  8. Thiago Silva – €17m
  9. Eden Hazard – €16.8m
  10. Franck Ribery – €16.5m
  11. Fernando Torres – €16.2m
  12. Yaya TourĂ© – €16m
  13. David Silva – €15.5m
  14. Gareth Bale – €14.5m
  15. Bastian Schweinsteiger – €14.5m
  16. Luis Suarez – €14.2m
  17. Mario Gotze – €13.9m
  18. Philip Lahm – €13m
  19. Gianluigi Buffon €12.9m
  20. Blaise Matuidi €12.9m
WACHEZAJI WALIONGIZA FEDHA NYINGI MIEZI 12 ILIYOPITA
  1. Jose Mourinho – €17m
  2. Pep Guardiola – €15m
  3. Roberto Mancini – €14m
  4. Carlo Ancelotti – €13.5m
  5. Fabio Capello – €12m
  6. Marcelo Lippi – €11.5m
  7. Arsene Wenger – €9.6m
  8. Roberto Di Matteo – €8.2m
  9. Andre Villas-Boas – €6.9m
  10. Rafael Benitez – €6.8m
  11. Luciano Spalletti – €6.5m
  12. Jurgen Klopp – €6.5m
  13. David Moyes – €6.4m
  14. Manuel Pellegrini – €6.4m
  15. Walter Mazzarri €6.1m
  16. Gerardo Martino – €5.4m
  17. Antonio Conte – €5.4m
  18. Claudio Ranieri – €5.2m
  19. Laurent Blanc – €4.2m
  20. Jorge Jesus – €4m
*Villa-Boas na Di Matteo wanaonekana kushika nafasi nzuri kwenye listi kwa sababu bado wanalipwa mishahara yao na Chelsea pamoja na Tottenham bbada ya vilabu hivyo kuwavunjia mikataba yao

Zantel yaipiga tafu CHANETA Klabu Bingwa ya Netiboli EA

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgvIIqu2KQRtz5d2FzsbLsP2QOSKbCUpep8SuRKj5U-M_VlpLawEw_r0qz8yMGoiJ-4NlGwjXN8IdS09n2z21ZgHjJ6nf9zPrSzYaQU22pKMbcG6BcgOdmQb-mhVUEkb-DEB0ly4MvBXD0/s640/DSC00021.JPG
Katibu Mkuu wa CHANETA, Anna Kibira

 KAMPUNI ya mtandao wa simu za mkononi ya Zantel, imesikia kilio cha Chama cha Netiboli Tanzania (CHANETA) baada ya kutoa kiasi cha Sh. Mil 10 kufanikisha Fainali za Klabu Bingwa ya mchezo huo kwa Afrika Mashariki itakayoanza Jumamosi jijini Dar es Salaam.

CHANETA kwa kipindi kirefu imekuwa ikipiga la mgambo kuomba wadhamini na wafadhili kujitokeza kufanikisha michuano hiyo ambayo mpaka sasa timu 22 zimethibitisha kushiriki, zikiwemo klabu za Tanzania Bara na Visiwani.

Taarifa juu ya udhamini huo wa Zantel usome mwenyewe hapo chini: 

Zantel supports Tanzania Netball Association

Zantel Tanzania has handed over a support of 10 million Tanzania shillings to the Tanzania Netball Association (CHANETA) for the development of netball in the country.
Handing the cheque to the Permanent Secretary of the Ministry of Information, Youth, Culture and Sports, Honorable Sihaba Nkinga, Zantel Chief Commercial Officer, Sajid Khan said Zantel aims to support the development and prosperity of netball in the country.
‘As great supporters of sports fraternity in the country, we are happy to announce our support to the Netball association of Tanzania because netball is a very important game in Tanzania sporting landscape and it has good following in the country’ said Khan.
Khan further reiterated Zantel’s commitment towards supporting sports in the country, both at grassroots and professional level, through the sports associations and the ministry.
Speaking after receiving the cheque Nkinga expressed her appreciation towards Zantel for their generous support.
‘The involvement of Zantel will greatly contribute to the performance enhancement and development of Netball in Tanzania and will make the vision of CHANETA a reality’ said Nkinga.
Speaking at the event, CHANETA Chairman, Ana Kibira said Zantel’s support has come at the right time as they are in final preparation of the East Africa Netball Competition.
Kibira also noted that the sponsorship is a milestone for CHANETA and they are certain that the sponsorship will make it possible for netball to go far.
‘We thank Zantel for this great support, and we want to assure them their support will go direct in supporting our programs and general development of netball in Tanzania’ said Kibira.

Zantel has been in support of various sports in the country, and this is the second time they are sponsoring netball as last year they also did the same.

Newz Alert! Ajali mnbaya yatokea Morogoro


Chumba cha habari cha Globu ya Jamii hivi punde kimearifiwa na kutumiwa picha za tukio la ajali eneo la Mikese na Mdau Martin Mnyenyelwa,lakini hakutufahamisha kuhusiana na athari ya ajali hiyo akiwa kama shuhuda wa tukio hilo. Kulingana na tukio ya taarifa hii kuwa nyembamba,basi tuvute subira tutajuzana kadiri ya zitakavyokuwa zikiiingia kwenye chumba chetu cha habari 
CHANZO : MICHUZI BLOG








Mastaa Bongo Mpo! Ronaldo aokoa maisha ya mtoto

 
MADRID, Hispania
MWANASOKA bora wa dunia, Cristiano Ronaldo amedhihirisha kuwa ni mtu mwenye huruma baada ya kujitolea kulipa gharama za upasuaji wa mtoto mwenye umri wa miaka 10.

Mtoto huyo, Erik Ortiz Cruz, anasumbuliwa na matatizo mbalimbali ya kiafya na upasuaji ndio pekee utakaoweza kunusuru maisha yake.

Familia ya mtoto huyo imeshindwa kumudu gharama za matibabu ya mtoto huyo hospitali, ambapo gharama za kila kipimo ni pauni 5,020 za Uingereza na upasuaji ni pauni 50,240.

Kutokana na hali hiyo, Ronaldo ameguswa na jitihada zinazofanywa na familia hiyo kwa ajili ya kukusanya fedha za kulipia matibabu ya mtoto huyo na kuamua kubeba mzigo huo.

Awali, Ronaldo aliombwa kuchangia viatu na fulana ili vipigwe mnada kwa ajili ya kuchangia fedha za matibabu hayo, lakini aliamua kwenda mbali zaidi kwa kulipa gharama hizo.

Mapema mwaka huu, Ronaldo alisherehekea tuzo ya kuwa mwanasoka bora duniani na watoto wanaosumbuliwa na ugonjwa wa kansa, akitekeleza ahadi aliyoitoa mwaka jana alipohojiwa na kituo cha redio cha Hispania.

Ronaldo alikutana na watoto hao wakati wa kipindi cha redio hiyo cha Partido de la 12 Novemba mwaka jana na kusema, iwapo atashinda tuzo hiyo, atasherehekea nao.

Afande kuzichezea Yanga, Azam kesho viingilio vyatajwa

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhNgRNeFylmsnnymnSCcIYonoCmcTVtwhsWiev1tkabvVA5Ap2gi4if2mY_-IqwoMi_WH02dJU5jQ9-6aM-B9yEX4V6UTWv1H6dujSz5nCGauRXz3Y3NDLejSHWxDEWpJxQZul65V3hJQzg/s1600/Yanga+Vs+Azam.JPG
Kesho shughuli itakuwa kama hii Taifa
REFA ambaye ni askari wa jeshi la Polisi Tanzania, Hashim Abdallah wa Dar es Salaam ndiye atakayechezesha mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kati ya Yanga na Azam itakayochezwa kesho Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 10.30 jioni.
Hashim atasaidiwa na Anold Bugado wa Singida, Florentina Zablon wa Dodoma na Lulu Mushi wa Dar es Salaam, wakati Kamisaa atakuwa Emmanuel Kavenga kutoka Mbeya na mtathimini wa waamuzi ni Alfred Rwiza wa Mwanza.
Tiketi kwa ajili ya mechi hiyo zitaanza kuuzwa saa 2 asubuhi katika magari maalumu kwenye vituo vya Shule ya Sekondari Benjamin Mkapa, Ubungo Terminal, mgahawa wa Steers uliopo Mtaa wa Samora/Ohio, OilCom Ubungo, Buguruni Shell, Dar Live- Mbagala, kituo cha daladala Mwenge na Uwanja wa Taifa.
Baada ya Saa 6:00 mchana mauzo yote yatahamia Uwanja wa Taifa ambapo milango kwa ajili ya mechi itakuwa wazi kuanzia saa 7.30 mchana.
Viingilio katika mechi hiyo vitakuwa sh. 30,000 kwa VIP A, sh. 20,000 kwa VIP B na C wakati viti vya rangi ya chungwa, bluu na kijani kiingilio ni sh. 7,000.

31 waitwa Ngorongoro Heroes


http://api.ning.com/files/B1324qSIT2YHP3VnpeUs2tV6urKULGbGsXIW0ivs62epVguIVD-y1Y2QLatDIYJg4xIYEO7CJ8*76ZSUaM*o62wepyIvErnO/NGORONGOROHEROESGLOBAL.jpgWACHEZAJI 31 wameteuliwa kujiunga na timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 20 (Ngorongoro Heroes) kwa ajili ya michuano ya Afrika ambayo fainali zake zitafanyika mwakani nchini Senegal.
Ngorongoro Heroes itakayokuwa chini ya Kaimu Kocha John Simkoko akisaidiwa na Mohammed Ayoub inaingia kambini kesho (Machi 19 mwaka huu) jijini Dar es Salaam kujiandaa kwa mechi ya kwanza dhidi ya Kenya itakayochezwa kati ya Aprili 4-6 jijini Nairobi.
Kikosi kinachounda timu hiyo ambayo itarudiana na Kenya kati ya Aprili 25-27 mwaka huu jijini Dar es Salaam kinajumuisha pia baadhi ya wachezaji walioonekana katika mpango wa ung’amuzi wa vipaji kwa ajili ya maboresho ya Taifa Stars.
Wachezaji walioitwa ni makipa Aishi Manula (Azam), Hamad Juma Hamad (Scouting- Temeke), Manyika Peter Manyika (Scouting- Ilala) na Mwinyi Hassan Hamisi (Mtende, Zanzibar).
Mabeki wa pembeni ni Ayoub Semtawa (Coastal Union), Edward Charles (JKT Ruvu), Frank Linus Makungu (Scouting- Rukwa), Gabriel Gadiel Michael (Azam), Hussein Mkongo (Ashanti United) na Ibrahim Said Mohamed (Chuoni, Zanzibar). Mabeki wa kati ni Bashiru Ismail (Tanzania Prisons), Faki Rashid Hakika (Ashanti United) na Pato Ngonyani (Majimaji).
Viungo ni Ally Nassoro (Coastal Union), Bryson Raphael (Azam), Farid Musa (Azam), Hamid Mohamed (Mbeya City), Hassan Mbande (Mtibwa Sugar), Ibrahim Mohamed Ibrahim (Scouting- Ilala), Idd Seleman (Ashanti United), Mohamed Issa Juma (Acudu, Afrika Kusini), Muhsin Ally Muhsin (Scouting- Kinondoni), Seleman Magoma (Scouting- Ruvuma) na Tumaini John (Scouting- Mwanza).
Washambuliaji ni Ally Salum Kabunda (Ashanti United), Ibrahim Hamad Hilika (Zimamoto, Zanzibar), Jafari Mwambusi (Mbeya City), Kelvin Friday (Azam), Ramadhan Bilal (Mlale JKT), Salum Abdilah Mineli (Ndanda) na Sibiank Lambard (Tanzania Prisons).

Airtel yakabidhi Mil 5 Tuzo za Mwanamakuka, Leila Mwambungu aibuka kidedea


Afisa Uhusiano wa Airtel, Jane Matinde (kushoto) akimkabidhi mfano wa hundi Mwenyekiti UWF na Mratibu wa Mradi wa Tuzo za Mwanamakuka Maryam Shamo wakati wa hafla ya Tuzo za Mwanamakuka 2014 ambapo Airtel Tanzania ni moja kati ya Wadhamini wa tuzo hizo ambazo Leila Mwambungu  aliibuka mshindi wa mwaka 2014. Wengine pichani kulia ni Mkurugenzi  Mkuu wa TWB Bi Margreth Chacha.
Afisa Uhusiano wa Airtel, Jane Matinde (kulia) akimpongeza mshindi wa tuzo ya Mwanamakuka 2014 Leila Mwambungu mara baada ya kutangazwa katika hafla iliyofanyika Escape One, Mikocheni Dar es Saalam.
Mshindi wa Tuzo za Mwanamakuka 2014, Leila Mwambungu akitoa shukrani zake mara baada ya kutangazwa katika hafla iliyofanyika Escape One siku ya Jumamosi. Kulia kwake ni Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya Wanawake Tanzania (TWB) Margreth Chacha.
KAMPUNI ya simu za mkononi ya Airtel, imekabidhi waandaaji wa Tuzo za Mwanamakuka, Umoja wa Wanawake Marafiki (UWF) kiasi cha Sh. Mil. 5 wakati wa hafla ya utoaji wa tuzo za Mwanamakuka-2014 zilizofanyika jijini Dar es Saalam, ambapo Leila Mwambungu aliibuka mshindi wa mwaka huu akiwabwaga washiriki wenzake tisa aliochuana nao.
Tuzo ya mwaka huu ilishirikisha washindi 10, watano wa mwaka 2012 na wengine wa mwaka 2013 kupima mafanikio yao kibiashara baada ya kunyakua tuzo na zawadi ya fedha katika shindano hilo lililoasisiwa mwaka juzi.
Mshindi huyo aliyekuwa mshindi wa pili wa tuzo za mwaka jana, aliibuka kidedea baada ya barua iliyoeleza alipotokea, alipo na malengo yake baada ya kushinda tuzo hiyo kutia fora na kumpa ushindi mbele ya wenzake.
Kampuni ya Airtel, imekuwa ikidhamini tuzo hizo tangu zilipoanzishwa safari hii ilikabidhi kiasi hicho cha fedha kupitia kwa Afisa Uhusiano wake, Jane Matinde aliyeeleza furaha waliyonayo kudhamini tuzo hizo kwa miaka mitatu mfululizo.
Matinde alisema Airtel wanajisikia faraja kuona wamekuwa sehemu ya kuleta mabadiliko kwa wanawake kupitia tuzo hiyo na kuahidi kuendelea kushirikliana na UWF kuhakikisha mabadiliko hayo yanawafikia wanawake wengi zaidi nchini.
“Tutaendelea kushirikiana na UWF, ili kuhakikisha tunawafikia wanawake wengi zaidi nchini,” alisema Matinde.
Kwa upande wa mshindi wa Mwanamakuka 2014, Leila Mwambungu alisema amejisikia furaha sana kushinda tuzo hiyo akidai hakuwa ametegemea na kuwashukuru waandaaji na wadhamini wake na kuomba waendelee kuwasaidia kuwakwamua wanawake nchini ambao wamejitosa kwenye shughuli za ujasiriamali.
"Naona fahari na furaha kuwa mshindi wa tuzo hizi za mwanamakuka kwa mwaka huu, napenda kuwashukuru sana waandaaji wa tuzo hizi kwa kuniona kupitia juhudi ninazoziweka katika kazi zangu na biashara zangu. Mpaka sasa nimeweza kuajiri watanzania kupitia biashara zangu. Kiasi nilichozawadiwa kitanisaidia kukuza zaidi mtaji wangu. Nashukuru sana," alisema mshindi huyo.
Naye Mwenyekiti UWF na Mratibu wa Mradi wa Tuzo ya Mwanamakuka, Mariam Shamo alisema tuzo hiyo inaendelea kukua na kuzidi kuiboresha na kudai lengo la shindano la mwaka huu lilikuwa kupima maendeleo ya washindi wao 10 kuona jinsi gani biashara zao zinavyosonga mbele baada ya kumzawadia aliyefanya vizuri zaidi.
"Tunashukuru sana Airtel kwa kushirikiana nasi miaka mitatu kwa sasa na tunaamini kuwa bado wataendelea kutoa mchango wao na kushirikiana nasi na kutuunga mkono kwa miaka mengine ijayo na kuhakikisha lengo letu la kumwinua mwanamke wa kitanzania linafikiwa," alisema Mariam.
Washiriki wa tuzo za mwaka huu walikuwa ni Tatu Ngao, Mwananne Msekalile, Sikudhani Daudi na Nasra Aziz walioshinda mwaka 2012 na Aziza Mbogolume, Leila Mwambungu, Theonistina Renatus, Maajab Yusufu na Agnes Daudi walioshinda mwaka 2013.

Chelsea kuifuta machozi England leo Ligi ya Mabingwa Ulaya?

CHELSEA leo inatarajiwa kuvaana na Galatasaray, ambapo mashabiki wa England wanataka kuona kama watawafuta machozi baada ya timu zao mbili za Arsenal na Manchester City ziking'olewa kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Timu nyingine ya England itakayoshuka dimbani kesho ni Manchester Unitd ambayo imewakatisha tamaa mashabiki wao kwa mwenendo wao mbaya na hivyo kutokuwa na tumaini nao kama watavuka 16 Bora na kuingia Robo fainali dhidi ya Olympiacos ya Ugiriki waliowanyoa 2-0 ugenini wiki mbili zilizopita.
Chelsea iliyoambulia sare ya 1-1 inavana na Gala, huku mshambuliaji wake wa zamani Didier Drogba hajui ni kwa namna gani ataweza kucheza kwa hamasa kubwa katika Uwanja wa Stamford Bridge  katika mechi hiyo ya leo.
Drogba alitwaa ubingwa wa England mara tatu, Kombe la FA mara nne, Kombe la Ligi mara mbili na ubingwa ulioweka kumbukumbu Ligi ya Mabingwa Ulaya 2012 akifunga penalti ya mwisho akiwa na Chelsea kwenye mechi ya fainali dhidi ya Bayern Munich katika Uwanja wa Allianz Arena.
Alifunga mabao 157 katika mechi 341 alizoichezea Chelsea kati ya 2004-12 huku akichaguliwa kama mchezaji wa kiwango cha juu zaidi katika historia ya klabu hiyo.
"Ni klabu ambayo nimepata uzoefu wa kila kitu," Drogba aliiambia tovuti ya UEFA (www.uefa.com). "Nimepata uzoefu wa kiwango cha juu, mechi kubwa na imenipa fursa ya kuwa karibu na wachezaji bora duniani.
"Ni kipindi maalumu kwangu kwa sababu sijui ni kwa vipi morali wangu utakuwa. Ninakubaliana kabisa kuhusu hili," alisema jijini Istanbul baada ya kutoka sare ya 1-1 na Chelsea.
Jose Mourinho alionekana akikaribia kumwaga chozi baada ya kupewa mapokezi mazuri katika awamu yake ya pili Stamford Bridge mwanzoni mwa msimu lakini anaamini Drogba anastahili heshima zaidi kutoka kwa mashabiki.
"Nadhani ninaruhusiwa kusema kwamba nitapata mapokezi mazuri kwa sababu ninajua mashabiki wa Chelsea na uhusiano wetu ulivyo wa kipekee," alisema Drogba.
"Itakuwa ni vizuri kuwaona kwa mara nyingine. Ninamtazamo wa mbeleni katika hilo."
Mourinho alimnunua Drogba na kumpeleka Stamford Bridge akitokea Olympique Marseille ambapo waliweza kushirikiana vema katika kufanya makubwa.
"Wakati Chelsea ikifikiria kunisajili, alikuwa ni Mourinho ambaye alikuja kuniona," alisema mchezaji huyo (36)- "Alisema, 'kama unataka kuwa mshmbuliaji mkubwa kama Thierry Henry ama Ruud van Nistelrooy, unapaswa kuja na kucheza chini yangu.
"Ni kweli nilikuwa mchezaji mzuri nikiwa Ligi ya Ufaransa lakini alinifanya kuwa mmoja kati ya wachezaji bora Ulaya. Ndiyo maana mimi, kwa Jose tunaweza kwenda sambamba hadi mwisho wa dunia.
Miamba hiyo ya Uturuki ni timu inayokuja kwa kasi, hivyo Chelsea itahitaji kufuta makosa yake baada ya Jumamosi kuangukia kichapo dhidi ya Aston Villa.
Ronaldo kuendelea kuweka rekodi Ulaya leo?
Katika mechi nyingine ya leo vinara wa Hispania, Real Madrid,  itakuwa inakamilisha ratiba yake ya kusonga mbele dhidi ya Schalke 04 baada ya mechi ya awali kuibuka na ushindi wa mabao 6-1 ugenini.
Katika mechi ya leo Real inatarajia kumpa nafasi Isco kuonyesha thamani yake baada ya kushindwa kupata namba ya kudumu chini ya Carlo Ancelotti tangu alipojiunga na timu hiyo kwa fungu kubwa akitokea Malaga.
Isco alikuwa ni biashara kubwa sokoni msimu uliopita baada ya kuiwezesha Malaga kutinga hatua ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Hata hivyo, Ancelotti anaamini bado Isco anaweza kuzoea nafasi mpya anayochezeshwa, kama ilivyokuwa kwa Mholanzi Clarence Seedorf.
"Anahamasisha kupata namba ya kuanza kikosi cha kwanza. Kwa sasa ninamuamini. Mwanzoni alikuwa kama ilivyokuwa kwa Seedorf ambaye baadaye alipata uzoefu na kuwa mchezaji muhimu kwa Milan," Ancelotti alisema mapema mwezi huu.
Kivumbi kingine cha ligi hiyio kuhitimisha timu mbili za mwisho za kutiunga robo fainali zitachezwa kesho kwa mechi kati ya Manchester United itakuwa nyumbani kuikaribisha Olympiakos Piraeus kwenye Uwanja wa Old Trafford, ikiwa inaugulia kipigo cha mabao 3-0 ilichopewa wikiendi na Liverpool.
Pambano jingine litakuwa kati ya wanafainali wa mwaka jana, Borussia Dortmund itakuwa nyumbani nchini Ujerumani kuivaa Zenit St Petersburg waliowanyonyoa kwao mabao 2-0.
Timu za Bayern Munich ya Ujerumani, Barcelona ya Hispania, PSG ya Ufaransa na Atletico Madridi zenyewe tayari zimetangulia hatua hiyo baada ya kiushinda mechi zao wiki iliyopita.

Ngassa, Niyonzima warejea Yanga, Dida akiwakosa Azam

WAKATI winga machachari Mrisho Ngassa akianza kujifua na wenzake mjini Bagamoyo kwa ajili ya mechi yao ya kesho dhidi ya Azam, kipa tegemeo wa Yanga kwa sasa, Deo Munishi 'Dida' ataikosa mechi hiyo ya Ligi Kuu Tanzania Bara kutokana  na jeraha la mkono.
Kwa mujibu wa  Daktari wa timu hiyo, Juma Sufiani, Dida hatakuwamo katika kikosi chao cha kesho ingawa wachezaji waliokuwa wagonjwa,  Mrisho Ngassa na Haruna Niyonzima wenyewe wameanza kujifua.
"Niyonzima (Haruna) na Ngasa (Mrisho) wamerejea kikosini na wameshaanza kujifua lakini tutamkosa kipa Dida katika mechi yetu inayofuata kutokana na kusumbuliwa na maumivu ya mkono," alisema Sufiani.
Niyonzima alikuwa anakabiliwa na malaria, huku Ngasa akisumbuliwa na majeraha ya nyama za paja na Twite (ruhusa).
Wakati Yanga hali ikiwa hivyo kuelekea kwenye mchezo wao wa kesho ambao unasubiriwa kwa hamu kubwa na mashabiki kuona nani atakayemtambia mwenzake, wapinzani wao waliowafungwa mabao 3-2 katika mechi ya kwanza pia watawakosa wachezaji kadhaa ambao ni majeruhi.
Meneja wa Azam , Jemedari Said aliwataja wachezaji hao ni Haji Nuhu, Joseph Kimwaga ambao wanauguza magoti.
Jemedari alisema wachezaji wengine wote wapo fiti kwa ajili ya mechi hiyo ambayo wanahitaji kushinda ili kutimiza ndoito zao za kutwaa ubingwa baada ya misimu miwili wakiishia kukamata nafasi ya pili nyuma ya Simba na Yanga.
Azam, inaoongoza ligi hiyo kwa kuwa na pointi 43 baada ya majuzi kuifumua Coastal Union kwa mabao 4-0, huku Yanga ikikamata nafasi ya pili baada ya kuambulia sare na Mtibwa japo wanalinga pointi na Mbeya City waliopo nafasi ya tatu wakiwazidi mabao ya kufunga na kufungwa.

Ruvu Stars waachia tatu, wajipanga kurekodi video

Roggert Hegga enzi akiwa Twnaga Pepeta
BENDI mpya wa muziki wa dansi ya Ruvu Stars, imekamilisha kurekodi nyimbo zao tatu mpya na tayari wameanza kuzisambaza kwenye vituo vya redio kwa ajili ya kuchezwa hewani.
Mmoja wa viongozi na muimbaji wa bendi hiyo yenye maskani yake Mlandizi, Pwani Rogert Hegga 'Catapillar', alisema wamemaliza kurekodi nyimbo hizo katikati ya wiki iliyopita na tayari baadhi ya vituoi zimeanza kuzirushwa hewani wakijiandaa kurekodi video zake.
Hegga alizitaja nyimbo zilizorekodiwa ambazo ndizo zinazoitambulisha bendi hiyo kwa mashabiki wa muziki wakiwa wanataka kurejesha enzi za bendi za majeshi kutamba nchini ni pamoja na 'Network Love' utunzi wa  Mhina Panduka 'Baba Danny' a.k.a Toto Tundu, 'Jua Kali' wa Kuziwa Kalala na 'Spirit' ambao ni utunzi wake (Hegga).
"Tumeshakamilisha kurekodi nyimbo zetu za utambulisho na tumeshasambaza na baadhi ya vituo zimeanza kuzicheza," alisema Hegga.
Mtunzi na muimbaji huyo wa zamani wa bendi kadhaa maarufu nchini ikiwamo ya African Stars, Mchinga Sound, G8 Wana Timbatimba na Extra Bongo, alisema vibao hivyo ni mwanzo wa maandalizi ya kupakua albamu yao na kuwataka mashabiki wasubiri kupata uhondo zaidi.
"Mashabiki wajiandae tu kupata burudani, nyimbo hizi zitaleta mapinduzi makubwa katika muziki wa dansi kwani zimeenda shule na studio tuliyorekodia ni bab'kubwa," alisema.
Baadhi ya wanamuziki wanaounda bendi hiyo inayomilikiwa na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) ni Khadija Mnoga 'Kimobitel', Hamis Amigolas, Hegga, Victor Mkambi, Mhina Panduka na wengine waliotoka bendi kadhaa za jijini Dar es Salaam.