STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, March 18, 2014

Mastaa Bongo Mpo! Ronaldo aokoa maisha ya mtoto

 
MADRID, Hispania
MWANASOKA bora wa dunia, Cristiano Ronaldo amedhihirisha kuwa ni mtu mwenye huruma baada ya kujitolea kulipa gharama za upasuaji wa mtoto mwenye umri wa miaka 10.

Mtoto huyo, Erik Ortiz Cruz, anasumbuliwa na matatizo mbalimbali ya kiafya na upasuaji ndio pekee utakaoweza kunusuru maisha yake.

Familia ya mtoto huyo imeshindwa kumudu gharama za matibabu ya mtoto huyo hospitali, ambapo gharama za kila kipimo ni pauni 5,020 za Uingereza na upasuaji ni pauni 50,240.

Kutokana na hali hiyo, Ronaldo ameguswa na jitihada zinazofanywa na familia hiyo kwa ajili ya kukusanya fedha za kulipia matibabu ya mtoto huyo na kuamua kubeba mzigo huo.

Awali, Ronaldo aliombwa kuchangia viatu na fulana ili vipigwe mnada kwa ajili ya kuchangia fedha za matibabu hayo, lakini aliamua kwenda mbali zaidi kwa kulipa gharama hizo.

Mapema mwaka huu, Ronaldo alisherehekea tuzo ya kuwa mwanasoka bora duniani na watoto wanaosumbuliwa na ugonjwa wa kansa, akitekeleza ahadi aliyoitoa mwaka jana alipohojiwa na kituo cha redio cha Hispania.

Ronaldo alikutana na watoto hao wakati wa kipindi cha redio hiyo cha Partido de la 12 Novemba mwaka jana na kusema, iwapo atashinda tuzo hiyo, atasherehekea nao.

No comments:

Post a Comment