STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, March 18, 2014

Rooney alizwa na mwaka wa shetani Man Utd

WAKATI Kocha wa Manchester United, David Moyes akikata tamaa kwa timu yake kumaliza nne bora katika Ligi Kuu England msimu huu, mshambuliaji wa timu hiyo, Wayne Rooney amesema kipigo cha mabao 3-0 walichokipata nyumbani dhidi ya Liverpool ndicho kibaya zaidi kwenye kipindi chake cha soka.
Steven Gerrard alifunga mara mbili kwa njia ya penalti kabla ya Luis Suarez kutupia la tatu huku Nemanja Vidic akitolewa nje kwa kadi nyekundu.
"Ulikuwa wakati mgumu. Ni moja kati ya siku mbaya zaidi kutokea kwangu katika maisha yangu kisoka. Liverpool inastahili pongezi kwa kucheza vizuri," Rooney aliiambia MUTV.

No comments:

Post a Comment