STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, October 18, 2014

Real Madrid yatuma salamu Liverpool, yaua 5-0 Ronaldo afunga 2

James Rodriguez
'Wauaji' wengine wa Real Madrid leo ni hawa watatu
Cristiano Ronaldo
Ronaldo akishangilia mabao yake
MWANASOKA Bora wa Dunia, Cristiano Ronaldo ameendelea kutupia mabao kambani baada ya jioni ya leo kufunga mabao mawili wakati Real Madrid wakipata ushindi mnono ugenini dhidi ya Levante kwenye Ligi Kuu ya Hispania, La Liga.
Ronaldo aliyefikisha mabao 15 katika mechi  ya nane, alianza kuaiandikia wageni bao kwa mkwaju wa penati dakika ya 13 baada ya Juanfran kufanyiwa madhambi na Javier Hernandez 'Chicharito' kufunga bao la pili katika dakika ya 38 akimalizia kazi nzuri ya James Rodriguez 'James Bond' .
Ronaldo alirudi tena kambani katika dakika ya 61 kwa kuaindikia Real Madrid bao la tatu akimalizia kazi ya Isco na James Bond akafunga bao la nne dakika ya 66 kwa kazi nzuri ya Ton Kroos na isco akamalizia kazi kwa kufunga bao la tano dakika nane kabla ya pambano hilo kumalizika kwa pande la Chicharito.
Ushindi huo wa Madrid uliowafanya wapunguze pengo la pointi na vinara Barcelona ni kama salamu kwa wapinzani wao wa Ligi ya Mabingwa Ulaya, Liverpool ya England watakaoumana nao siku ya Jumatano.
Katika mechi nyingine Athletic Bilbao ikiwa nyumbani ililazimishwa sare ya 1-1 dhidi ya Celta Vigo na kwa sasa Barcelona wapo nyumbani wakiumana na Elber na m atokeo bado ni 0-0.

No comments:

Post a Comment