STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, October 18, 2014

Simba, Yanga debe tupu, Azam yaua, Mtibwa yabanwa

Mpambano wa watani ulivyokuwa uwanja wa Taifa leo
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgnGI0Fa_A1fReGNq630wAe-HUeAeC3CnzyXNWI0OAPfBgI-aka3Ybg_uU2XVpZaMurdewSapeGfrEvocd18umDQjB5vFdhDmsHEVhTWCSFg3rp4vfk7e-UZaT1IRvH4QtZHSFcKp6a8H7v/s1600/Picha+Simba.JPGhttps://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgNPa5lzs3_DyhJWIBPQ4eR7PVVwEV7kBsmZgbFj2NkFWHudak-xT3RA29hwYq_es9UcaOF5fj0I9w9hmoY_GT4jyCWZ2zMxmOX1zN7vws4XBFeRVRUgqalCm9eoug3LZYGSjq7wMFA9_PP/s1600/Yanga+leo+1.JPGWAPINZANI wa jadi wa soka Tanzania, Simba na Yanga zimeshindwa kutambiana katika pambano lao lililochezwa jioni hii kwenye uwanja wa Taifa, licha ya tambo za mapema kabla ya mchezo huo, huku Azam wakijikwea kileleni mwa msimamo wakiipiku Mtibwa Sugar waliobanwa mjini Morogoro.
Simba na Yanga ambazo zilikamiana na kutambiana kwa wiki kadhaa sasa, walishindwa kufungana katika pambano lililoshuhudia mtoto wa nyota wa zamani wa Mtibwa, Yanga na Taifa Stars, Manyika Peter, kipa Peter Manyika Jr aking;ara kwa kuinyima Yanga mabao kwenye uwanja huop wa Taifa.
Timu zote ilifanya kosa kosa za hapa na pale na has akwenye kipindi cha pili huku makocha wao, Marcio Maximo wa Yanga na Patrick Phiri wa Simba wakifanya mabadiliko ya wachezaji bila kuleta tija hadi dakika 90 za pambano lililochezeshwa vema na mwamuzi Israel Mujuni Nkongo.
Kwa matokeo hayo Yanga imefikisha pointi 7 na kushuka hadi nafasi ya nne wakiwapisha Coastal Union kukalia nafasi hiyo baada ya jioni ya leo kushinda mabao 2-0 dhidi ya Mgambo na kufikisha idadi kama hiyo ya pointi ila ikiwa na uwiano tofauti ya mabao, huku watani zao hiyo ikiwa ni sare yao ya nne msimu huu na ikifikisha mechi ya 10 katika ligi bila kuonja ushindi imefikisha pointi nne.
Katika mechi nyingine za ligi hiyo, Azam waliwafyatua Mbeya City nyumbani kwao kwenye uwanja wa Sokoine kwa bao 1-0 na kufikisha idadi ya mechi 38 bila kupoteza katika Ligi Kuu..
Bao hilo liliwekwa kimiani na beki wake wa kati, Aggrey Morris kwa mkwaju wa adhabu kwenye dakika ya 19 na kuifanya mabingwa watetezi hao kukwea kileleni wakifikisha pointi 10 sawa na Mtibwa Sugar ambao walilazlmishwa suluhu mjini Morogoro na ndugu zao Polisi Moro kwenye uwanja wa Jamhuri.
Azam na Mtibwa zote zimefungana idadi ya pointi zikiwa na 10 kila moja, huku wakiwa na mabao sita kila moja na kufungwa moja, isipokuwa kiherufi Azam inawatangulia Wakata Miwa.
Kutoka Mkwakwani Tanga, Coastal Union imezidi kujiongezea pointi baada ya kuilaza Mgambo JKT kwa mabao 2-0.
Mabao ya washindi yalifungwa na Rama Salim kwa mkwaju wa penati kabla ya Kennedy Masumbuko kuongeleza la pili kwenye kipindi cha pili.
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEheu2S3fe_9FoFd7hnk3AwEiXmoOP2ulk9Y13fiRJl12EdBwVuaIaC0y1ulilytUphp2lKiDBXt3tJkB_gfKPzweV4tFKqdIhBe-kGqjPOH6NhkBOCD0sjIxEJ00LhbAeNd57i_xQ_Yrxkh/s1600/20140913_160438.jpg
Ndanda waliopigwa nyumbani na Ruvu Shooting

Nayo timu ya Ruvu Shooting wakiwa ugenini mjini Mtwara wamewatoa nishai wenyeji wao Ndanda Fc kwa kuwalaza mabao 3-1, mabao ya washindi yakiwekwa kimiani na Juma Nade, Abdurahman Mussa na Mathew. ilihali Kagera Sugar wakiwa nyumbani wamelazimishwa suluhu ya kutofungana na Stand United.
Ruvu waliovunja mwiko wa kutofunga bao lolote katika ligi ya msimu huu kwa kuilaza Ndanda mabao 3-1
Mtibwa iliyobanwa mbavu na Polisi na kutoka suluhu

No comments:

Post a Comment