STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, December 23, 2014

News Alert! Idadi ya Waliokufa kwa Ebola yaongezeka

http://media4.s-nbcnews.com/i/newscms/2014_41/711201/141010-ebola-death-toll-1548_3d6ad58be94ec50e24fe731eef6a647c.jpgSHIRIKA la Afya Duniani, WHO linasema idadi ya waliofariki dunia kutokana na ugonjwa wa Ebola imeongezeka kupita watu 7,500 na idadi ya kesi zinafikia 20,000.
Takwimu mpya zilizotolewa Jumatatu zinaonyesha mwelekeo huko Liberia na Guinea ukionyesha kupungua katika maambukizo ya Ebola , wakati kesi za Sierra Leone zikiendelea kuongezeka. 
Hizo nchi tatu za Afrika magharibi zina karibu idadi ya vifo vyote vya Ebola barani Afrika.
Idadi ya waliofariki katika nchi nyingine iko pale pale huku kukiwa na vifo sita  Mali, nane Nigeria na kimoja Marekani. 
Spain na Senegal kila moja walikuwa na kesi moja ya ugonjwa huo lakini hakuna vifo.
Pia Jumatatu katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon amesema jumuiya ya kimataifa inahitaji kujiandaa vizuri zaidi kwa mlipuko ujao duniani ambao amesema ndio mtihani ambao kwa hakika utakuja.
VOA

Breaking Newz! Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini, Eliakim Maswi asimamishwa kazi! Nani atakayefuata?!

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjEvZHCa4G5UTNbP9yh47EU8Xdxl34rhZ6haSntr0VaTF6tvBGGoNVcuxYUtdhPu4ASsLnBrpUPFDwdMRFunlhSnSqd2c0bHWW0fYvW9IH1XZA1R-4MdTc7pfSdF6NOKMOjuuDyZmj-Xbma/s1600/maswi-sept30-2013.jpg
Al;iyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Eliakim Maswi
SAKATA la Akaunti ya Tegeta Escrow limeendelea kuzama na watu baada ya muda mfupi uliopita MICHARAZO kupata taarifa kwamba Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Eliakim Maswi  amesimamishwa kazi ili kupisha mamlaka kufanya uchunguzi juu ya tuhuma zinazomkabili.
Kusimamishwa kwa Maswi kumekuja ikiwa ni simu moja baada ya Rais Jakaya Kikwete kutangaza kumfuta kazi aliyekuwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Prof Anna Tibaijuka.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jioni hii kutoka Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Tanzania inasema kuwa Katibu Mkuu Maswi amesimamishwa kazi.
Taarifa hiyo inasema kuwa Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Yohana Sefue amemsimamisha kazi kwa muda Ndugu Eliakim Maswi,  Katibu Mkuu ya Wizara ya Nishati na Madini ili kupisha uchunguzi wa tuhuma dhidi yake kama ilivyoelekezwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete.
Uchunguzi huu ni moja ya hatua za utekelezaji wa maazimio nane yaliyotolewa na Bunge ambayo yalimtaka Rais Kikwete kuwawajibisha wahusika wote waliohusika na ubadhilifu wa pesa za Escrow.
Hii hapa taarifa kamili iliyotolewa na Kurugeni hiyo muda mfupi uliopita.
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

KATIBU Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Yohana Sefue, amemsimamisha kazi kwa muda Ndugu Eliakim Maswi,  Katibu Mkuu ya Wizara ya Nishati na Madini, ili kupisha uchunguzi wa tuhuma dhidi yake, kama ilivyoelekezwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete.
Balozi Sefue amemsimamisha kazi Ndugu Maswi kuanzia leo, Jumanne, Desemba 23, 2014, kwa kutumia madaraka aliyonayo kama Mamlaka ya Nidhamu kwa Watumishi wa Umma wanaoteuliwa na Rais, wakiwemo Makatibu Wakuu.
Taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Balozi Sefue mjini Dar es Salaam imesema kuwa amechukua hatua hiyo “Kwa mujibu wa Kifungu 4(3) (d) cha Sheria ya Utumishi wa Umma, Na. 8 ya mwaka 2002 (kama ilivyorekebishwa)” ambapo “Katibu Mkuu Kiongozi ndiye Mamlaka ya Nidhamu kwa Watumishi wa Umma wanaoteuliwa na Rais, wakiwemo Makatibu Wakuu.”
Badala yake, Balozi Sefue amesema kuwa Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Nishati na Madini, Mhandisi Ngosi C. Mwihava atakaimu nafasi ya Katibu Mkuu, Wizara ya Nishati na Madini, hadi uchunguzi dhidi ya Ndugu Eliakim C. Maswi utakapokamilika.
Taarifa hiyo ya Balozi Sefue pia imekariri kauli ya Rais Kikwete katika hotuba yake kwa Taifa jana, Jumatatu, Desemba 22, 2014 ambako Rais alisema:
“Kuhusu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, kwa vile ni Mtumishi wa Umma, anatawaliwa na Sheria na Kanuni za Utumishi wa Umma, hivyo nimeshaelekeza Mamlaka kuchunguza tuhuma zake na hatimaye ikibainika ana makosa hatua za kinidhamu zitachukuliwa.”
Ndugu Maswi, aliyekuwa Mwanasheria Mkuu Ndugu Frederick Werema pamoja na Mawaziri wawili walituhumiwa wakati wa Kikao cha Bunge kilichopita kuhusiana na Akaunti ya Tegeta Escrow.
Wakati huo huo, Rais Kikwete ameelekeza kuwa pamoja na hatua nyingine zinazochukuliwa, Shirika la Umeme (TANESCO) waendelee na majadiliano na IPTL kuhusu uwezekano wa kushusha tozo la uwekezaji (capacity charge) zaidi ya punguzo la awali lililopatikana kupitia Kituo cha Kimataifa cha Kusuluhisha Migogoro ya Kimataifa (ICSID).
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu – Dar es Salaam.
23 Desemba, 2014

Black &White Bash 55th Birthday Party ya Asia Idarous Khamsin ..Ndani ya M.O.G Bar (Nyumbani Lounge) Des 24

Na Andrew Chale
WABUNIFU wa Mavazi wachanga na chipukizi wamemwandalia Sherehe za kuzaliwa ya Mama wa Mitindo, Asia Idarous Khamsin, zitakazofanyika usiku wa Desemba 24, ndani ya ukumbi wa M.O.G Bar (Nyumbani Lounge) huku ikisindikizwa na Spice Modern Taarab pamoja na Mini fashion show.
Katika usiku huo maalum, kiingilio ni sh 5,000, huku vazi maalum likiwa Black & White, ambapo pia wadau watakaojumuika na Mama wa Mitindo, watapata burudani kali ya muziki kutoka kundi hilo la Spice Modern taarab, Dj Mapuu pamoja na  shoo ya ubunifu wa mavazi (Min fashion show) itakayopambwa na wabunifu wanaochipukia.
Usiku huo wa Black &White Bash 55th Asia Idarous Khamsin, pia itakuwa na Red Carpet na wadau watapiga picha na mastaa mbalimbali sambamba na pongezi za kunyakua tuzo ya ‘Life Time Achievement Swahili Fashion Week 2014’.

Arsene Wenger apumua kwa Ramsey, Arteta bado

http://singinthecheapseats.files.wordpress.com/2012/10/arteta-ramsey.jpg
Mmoja ananafasi ya kushuka dimbani mwishoni mwa wiki hii, mwingine atasubiri sana
WANAPUMUA! Wakati nahodha wa Arsenal, Mikael Arteta akidaiwa atachelewa kupona, kocha wa klabu huyo amesema kiungo Aaron Ramsey anaweza kuwa fiti kwa ajili ya mchezo dhidi ya Southampton.
Mechi hiyo itachezwa siku ya Mwaka Mpya na Arsene Wenger anaamini atapata fursa ya kumtumia kiungo huyo aliyetolewa katika mechi ya mwisho ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Galatasaray.
Arteta alipata majeruhi mwezi uliopita katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya pia dhidi ya Borussia Dortmund na Wenger amesema nahodha wake huyo anaendelea vyema.
Hata hivyo alisema pamoja na kuendelea vyema lakini atachelewa kidogo kuliko ilivyotegemewa lakini Ramsey anaweza kurejea katika mchezo dhidi ya Southampton. 
Ramsey alikuwa akirejea katika kiwango chake cha msimu uliopita akiwa amefunga mabao matatu katika mechi mbili kabla ya kutolewa wakati wa mapumziko katika mchezo dhidi ya Galatasaray hivi karibuni.
Wenger pia amebainisha kuwa Laurent Koscielny naye anakaribia kurejea katika kikosi cha kwanza na anaweza kuwepo katika kikosi chake kitakachocheza Jumapili ugenini dhidi West Ham Utd huko Upton Park.

Cargliari yamtimua kocha wake kisa...!

http://cdn.bleacherreport.net/images_root/slides/photos/002/654/635/hi-res-153607730_crop_650x440.jpg?1349634469BAADA ya timu ya Cargliari iliyopo Ligi Kuu ya Italia, Serie A kufanya vibaya mfululizo, uongozi wa klabu hiyo umemtupia virago kocha wake, Zdenek Zeman.
Kocha Zeman ametimuliwa baada ya Cargliari kupata ushindi katika mechi mbili msimu huu, kitu ambacho kimeufanya uamuzi kusitisha mkataba na kocha huyo kutoka Jamhuri ya Czech.
KOcha huyo wa zamani wa AS Roma ametimuliwa wakati timu hiyo ikiwa katika nafasi ya 18 katika msimamo wa Serie A. 
Kipigo cha mabao 3-1 walichopata ugenini dhidi ya vinara Juventus Alhamisi iliyopita ndio ulikuwa mchezo wa mwisho kwa kocha huyo mwenye umri wa miaka 67. 
Katika taarifa yake klabu hiyo ilimshukuru kocha huyo kwa kipindi chote ambacho wamekuwa naye kwa miezi kadhaa na kumtakia kila la heri popote atakapokwenda. 
Kocha wa zamani wa klabu ya Al Jazira, Walter Zenga ambaye kwa sasa hana kibarua anapewa nafasi kubwa ya kuchukua mikoba ya Zeman.

Katibu Mkuu mpya wa Yanga aahidi makubwa Jangwani


TIBO
Katibu Mkuu wa Yanga, Dk Tiboroha akizungumza na waandishi wa habari, huku Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa klabu hiyo, Jerry Muro akiwa makini.

SIKU chache baada ya kutangazwa kushika nafasi ya Ukatibu Mkuu ndani ya klabu ya Yanga, Dk Jonas Tibohora aahidi makubwa kwenye klabu hiyo.

Dk, Tobohora akizungumza leo jijini alisema kuwa, ndoto yake ni kuona Yanga ikijiendesha kiuchumi.
Katibu mkuu huyo amesema anataka kuiongoza Yanga kujiendesha kiuchumi, katika mpango wake huo anataka kuanza kutengeneza kikosi imara cha ushindani ikiwa ni pamoja na kutengeneza mifumo bora ya soka la vijana klabuni hapo
Lengo kubwa la kuwekeza kwenye timu za vijana ni kujalibu kupunguza ghalama za kununua wachezaji kutoka nje,pia amesema sasa ni muda wa klabu hiyo kunufaika na nembo ya klabu hiyo kibiashara.

Dk Tobohora amechukua nafasi ya Beno Njovu aliyemaliza mkataba na kutotaka kuendelea kwa madai ya kutingwa na majukumu mengi binafsi.

Muhammad Ali anaendelea vyema hospitalini

http://worldsportss.com/wp-content/uploads/2014/10/Muhammad-Ali-101.jpgHALI ya Bingwa wa zamani wa Masumbwi Duniani kwa Uzani wa Juu, Muhammad Ali inaendelea vyema.
Msemaji wa gwiji huyo aliyekimbizwa hospitalini mwishoni mwa wiki kutokana na maradhi ya maambukizi katika mapafu, alisema Ali anaendelea vema. 
Msemaji huyo, Bob Gunnell amesema madaktari wanaomtibu Ali wana matumaini ya kumruhusu katika kipindi cha karibuni. 
Gunnell aliendelea kudai kuwa familia ya nguli huyo bado inaomba suala hilo kuachwa kuwa la binafsi na kushukuru maombi yote ya kumtakia heri. 
Ali, 72, bingwa wa wa zamani mara tatu wa uzito wa juu duniani ambaye anaugua ugonjwa wa kutetemeka au Parkinson alikimbizwa hospitali Jumamosi iliyopita. Ali aligundulika kuwa na Parkinson mwaka 1984, miaka mitatu baada ya kutangaza kustaafu masumbwi.

Salha Abdallah adai alili-miss Jukwaa

Salha katika pozi
Salha wa Hammer
MUIMBAJI mpya wa kundi la muziki wa taarab la Five Star, Salha Abdallah 'Salha wa Hammer' amesema kurejea kwake jukwaani kumemfanya kujisikia faraja kubwa kwa vile 'alilimisi' jukwaa hilo kwa muda mrefu.
Salha aliyekuwa akiliimbia kundi la King's Modern 'Wana Zima Taa', alikuwa kwenye likizo ya uzazi jambo lililomfanya asionekane jukwani kwa zaidi ya miezi minne na hivi karibuni alijiunga na kundi la Five Star lililozindua albamu yao mpya ya 'Kichambo Kinakuhusu' akiwa miongoni mwa waimbaji wa nyimbo za albamu hiyo.
"Kwa kweli 'nililimisi' sana jukwaa, nimejisikia faraja kurudi tena ulingoni. Naamini baada ya 'Kishtobe cha Mtaa' kuna kazi nyingine kali zaidi zinakuja," alisema Salha.
'Kishtobe cha Mtaa' ni wimbo alioimba mwanadada huyo ambaye ni mke wa muimbaji mwingine nyota wa miondoko ya taarab na mduara, Hammer Q.
Salha alisema mashabiki waliomkosa kwa muda mrefu ni fursa yao ya kujitokeza kwenye maonyesho ya kundi lake jipya kupata burudani.

Newz Alert! Simba yapata pigo Zenji wakiiwinda Kagera Sugar

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhrM2-h9AiqcqsrWvWx9Jx0JTltliwtnjqzkQ-O2YA5w54Gyk592pkskTvj6KPw09h0s8OSRGPQmfqtbaw9apfIAYHhhHGH9QFdR9kBYCH7nCtKpa10ZmrCRGaZMycXiFOwAfZuLmm5hbE/s1600/DSC_0919.JPG
Elias 'Magoli' Maguli (kushoto)
WAKATI wakiwa katika maandalizi ya 'kuiua' Kagera Sugar katika mechi yao ya Ligi Kuu Tanzania itakayochezwa siku ya Ijumaa, Simba imepata pigo katika kambi yake visiwani Zanzibar baada ya mshambuliaji wake nyota Elias 'Magoli' Maguli kuumia kifundo cha mguu.
Simba ambao wamekimbilia Zenji siku ya Jumapili kwa ajili ya kujaindaa na pambano hilo dhidi ya Kagera litakalochezwa kwenye uwanja wa Taifa, itamkosa Maguli katika pambano hilo kwa kuapata majeraha.

Maguli ambaye aliitungua Yanga wakati timu yake wakiizamisha kwa mabao 2-0 kwenye pambano la Nani Mtani Jembe-2 lililochezwa Desemba 13, aliumia kifundo hicho wakati wa mazoezi na hivyo kumweka nje ya dimba mpaka apone.
Kukosekana kwa Maguli, mmoja wa wachezaji wenye vipaji na nguvu kubwa awapo uwanjani ni mtihani kwa Simba ambayo inakabiliana na timu ngumu inayonolewa na kocha Mganda Jackson Mayanja ambao mara kadhaa wamekuwa wakiisumbua timu hiyo kwenye uwanja huo wa Taifa.
Pia Simba ipo katika hati hati ya kupata huduma za nyota wake wa Kiganda, Emmanuel Okwi ambaye yupo nchini kwao kwa ajili ya maandalizi ya kufunga ndoa.
Ligi Kuu Tanzania Bara iliyokuwa imepumzika tangu NOvemba 9 itaendelea tena Ijumaa kwa pambano moja kati ya Simba na Kagera Sugar na kuendelea siku zinazofuaata kwa michezo kama ifuatavyo:
JUMAMOSI:
Mtibwa Sugar vs Stand United
Prisons-Mbeya vs Coastal Union
JKT Ruvu vs Ruvu Shooting

JUMAPILI:
Mbeya City vs Ndanda Fc
Polisi Moro vs Mgambo JKT
Yanga vs Azam

Chelsea haishikiki England, yainyoa Stoke City kwao x2



Diego Costa akitafuta bao langoni mwa wenyeji Stoke City

Costa akichuana na wachezaji wa Stoke City

Cesc Fabregas akishangalia bao lake
MABAO mawili yaliyowekwa kimiani katika kila kipindi kimeiwezesha Chelsea kupata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Stoke City na kwenda kula sikukuu ya Krismasi ikiwa kileleni kwa mara ya nne sasa.
Vijana Jose Mourinho wakiokuwa ugenini katika uwanja wa Britania, walipata ushindi huo uliowafanya wazidi kujikita kileleni mwa msimamo wakiwa na pointi 42, tatu zaidi ya walizonazo mabingwa watetezi ambao waliwakamata Jumamosi baada ya kuizabua Crystal Palace mabao 3-0.
Nahodha John Terry aliiandikia Chelsea bao la kuongoza dakika mbili tu baada ya kuanza kwa mchezo huo akiunganisha mpira wa kona na kiungo nyota wa Hispania ambaye anaongoza kwa kutengeneza mabao 12 mpaka sasa ndani ya Chelsea aliiandika bao la pili dakika ya 78 kabla ya kumalizika kwa pambano hilo.
Ligi hiyo inatarajiwa kuendelea tena siku ya Ijumaa ambayo itakuwa Boxing Day kwa vinara hao kushuka dimbani kuumana na West Ham United kwenye uwanja wa Stanford Bridge.
Mechi nyingine siku hiyo ni kama zifuatavyo:
Burnley v  Liverpool Crystal Palace  v Southampton  
Everton v Stoke City
Leicester City v  Tottenham Hotspur
Manchester United  v  Newcastle United 
Sunderland   v   Hull City       
Swansea City  v   Aston Villa 
West Bromwich Albion v  Manchester City
Arsenal  v  Queens Park Rangers