STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, December 23, 2014

Arsene Wenger apumua kwa Ramsey, Arteta bado

http://singinthecheapseats.files.wordpress.com/2012/10/arteta-ramsey.jpg
Mmoja ananafasi ya kushuka dimbani mwishoni mwa wiki hii, mwingine atasubiri sana
WANAPUMUA! Wakati nahodha wa Arsenal, Mikael Arteta akidaiwa atachelewa kupona, kocha wa klabu huyo amesema kiungo Aaron Ramsey anaweza kuwa fiti kwa ajili ya mchezo dhidi ya Southampton.
Mechi hiyo itachezwa siku ya Mwaka Mpya na Arsene Wenger anaamini atapata fursa ya kumtumia kiungo huyo aliyetolewa katika mechi ya mwisho ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Galatasaray.
Arteta alipata majeruhi mwezi uliopita katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya pia dhidi ya Borussia Dortmund na Wenger amesema nahodha wake huyo anaendelea vyema.
Hata hivyo alisema pamoja na kuendelea vyema lakini atachelewa kidogo kuliko ilivyotegemewa lakini Ramsey anaweza kurejea katika mchezo dhidi ya Southampton. 
Ramsey alikuwa akirejea katika kiwango chake cha msimu uliopita akiwa amefunga mabao matatu katika mechi mbili kabla ya kutolewa wakati wa mapumziko katika mchezo dhidi ya Galatasaray hivi karibuni.
Wenger pia amebainisha kuwa Laurent Koscielny naye anakaribia kurejea katika kikosi cha kwanza na anaweza kuwepo katika kikosi chake kitakachocheza Jumapili ugenini dhidi West Ham Utd huko Upton Park.

No comments:

Post a Comment